Ajali mbaya Inyala Mkoani Mbeya, idadi ya waliofariki yafikia watu 19

Nasema Uongo Ndugu Zangu

JF-Expert Member
Apr 28, 2020
279
773
gari ajali.jpg
Ajali mbaya imetokea katika eneo la Inyala mkoani Mbeya baada ya lori la mafuta kufeli breki na kugonga basi la abiria na gari ndogo na kusababisha vifo vya watu kadhaa na majeruhi. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

FB_IMG_1660646001533.jpg

---
Watu nane wamefariki Dunia na wengine ambao idadi yao haijafahamika wakijeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea leo Jumanne, Agosti 16 katika eneo ya Shamwengo karibu na kituo cha mafuta Inyala mkoani Mbeya.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Urlich Matei amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo, akieleza kuwa gari la kKampuni ya Evarest Frech Ltd likiwa na kontena la mchanga lilifeli breki na kuligonga basi la Super Rojas lililokuwa likitoka Mbeya kwenda Njombe.

“Waliopoteza maisha ni nane japokuwa bado idadi rasmi haijajulikana ila baadaye taarifa ya daktari itaeleza kwa ujumla, ila majeruhi wamesambazwa kwenye hospitali tofauti ikiwamo Igawilo na Mkoa,” amesema Kamanda Matei.

-------
UPDATES

MBEYA: AJALI YA INYALA, WALIOFARIKI WAFIKIA 19
ldadi ya vifo katika ajali iliyotokea Leo Agosti 16, 2022 imefikia Watu 19 ambapo majeruhi wawili kati ya 10 hali zao inaelezwa kuwa ni mbaya.

Awali taarifa ya ajali hiyo iliyohusisha Lori lililobeba mchanga kisha kufeli breki na kugonga magari matatu katika maeneo ya Shamwengo, Kata ya Inyala Mkoani Mbeya ilidaiwa waliofariki Dunia ni wanne.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Urlich Matei amethibitisha idadi hiyo ya vifo 19.
 
Kwa hiyo mgezuia break za malori zisifeli hapo Inyala. Suala muhimu ni Malori, magari ya abiria na gari nyinginezo kufanyiwa ukaguzi wa mara kwa mara.
Haha !!
ukaguzi wa mara kwa mara ? Pia haisaidii, pananguka mqgari mapya kabisa hapo,

Kuanzia uyole hadi unafika igawa ni kipande cha kuomba mungu tu , barabara ni finyu na sio rafiki.

Gari bovu ni hatari sana , lakini barabara mbovu ni hatari zaidi
 
Ajali mbaya imetokea katika eneo la Inyala mkoani Mbeya baada ya lori la mafuta kufeli breki na kugonga basi la abiria na gari ndogo na kusababisha vifo vya watu kadhaa na majeruhi. Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Ahsante Mzee Kinana kwa kutufurusha barabarani, tumezoea katika majukumu mapya, hatuna shida.
View attachment 2325321
Lini traffic walisaidia kuzuia ajali?

Hopeless kabisa wakati nyie ndo mlisababisha ajali ziwe nyingi kwa kuruhusu magari chakacu yaingie barabarani baada ya kuomba buku mbili ya rushwa.
 
Inyala pipeline panahitaji dual carriage ways
Trafiki wa kinana watasema na hii wangeweza kuzuia kama wangalikuwepo barabarani.
Mimi nilisikia Mh Kinana akishauri trafiki wapungue mijini, hakusema wapungue barabarani
Japo ajali kama hiyo haihusiani na trafiki kwani huwezi kucheki breki ukajua kuwa baada ya muda haitashika
 
Ni kweli kabisa. Napafahamu mahali hapo ni barabara ya hovyo kupata kutokea. lakini pia wangepapanua wakaweka na climbing lane na parking ya dharura kwa malori.
Ndio maana mkuu barabara zetu ndio tatizo kubwa, mengine ni mengineyo, mimi ningekua waziri wa mawasiliano hizi pass zote ndani ya T1 ningefanya yafuatayo:kabla hujaanza kushuka kitonga pass ningejenga compossory stop kwa magari yote above 10T,yaani ukifika pale lazima usimame, hii itasaidia to slow down momentum ya vehicles hizi, hivyo hivyo kwa Inyala Pass;,pia ningejenga arrester ili kudeal na magari yaliyo fail breaks, Zambia wanazo hasa kuelekea border ya Chilundu, yaani ukipata break failure unalielekeza gari upande wa arrester (imetengenezwa zaidi kwa mchanga na kokoto);
 
Back
Top Bottom