Ajali mbaya leo asubuhi Dar es salaam

Ajali mbaya leo asubuhi Dar es salaam

Mnyenz

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2014
Posts
4,903
Reaction score
13,287
Ajali mbaya imetokea leo asubuhi baada ya gari ndogo kuhama njia na kutumbukia kwenye mtaro na kisha kuwaka moto na kuteketea maeneo ya kati ya Africana na Mbuyuni(Bagamoyo road).

Ndani ya gari kulikua na mtu mmoja tu, inasemekana dereva alikuwa katika mwendo kasi kisha kwa mbele ikatokea gari nyingine ambayo ilikuwa ikivuka kuenda upande wa pili (Mwenge) hapo ndio dereva wa hili gari katika kufanya juhudi za kukwepa akaingia mtaroni na baada ya muda gari ikalipuka kwa moto na kuteketea yote.

Mungu ampumzishe kwa Amani.

Chanzo: Mimi na Baadhi ya mashuhuda.
attachment.php
 

Attachments

  • 1414301937708.jpg
    1414301937708.jpg
    138.4 KB · Views: 5,010
Jamaa kaisha kwa moto mpaka kichwa kimepasuka,nimeshuhudia pia wakati inawaka mpaka ilipozimwa. So sad
 
Ni kweli ya kusikitisha lakini hao moto chini na moto bati ni wapo wengi hao na sijui hawa wanajiamini kivipi au roho zinauzwa madukani ndo kujiamini hivo tena kila siku hayo hayo tuu
 
Msilaumu sana eti dereva alikuwa mlevi. Kwa mwendo kasi inawezekana na inapotokea dalili ya ajali kila dereva ana panic na kuchukua maamuzi ya haraka. Na kila amuzi la haraka lina matokeo yake kulingana na mhusika alivyo sharp kupata the best or the worst quick option. Hakuna kulaumiana hapa hasa kama wewe ni dereva. Rest in Peace ndugu.
 
Duh,kweli katangulia huyo ...madreva jamani ni bora uchelewe kazini lakini ujari uhai wako vinginevyo utakufa na kuacha simanzi kwa jamaa
 
Kwa comment nyingi hapo juu mwanangu mdogo <5yrs angesema "Pumbafu alah!", watu hatukuwepo hatuji kilichojiri, na wala hatujui huyo dereva alikuwa anakimbilia wapi lakini sisi tunatoa hukumu na maneno ya kejeli. Kumbuka ajali haina kinga jamani ingawa tunatikiwa tuchukue tahadhari, pia kumbuka waweza kuta ni jamaa yako halafu umeishabwabwaja maneno kama ya baadhi ya comments hapo juu.
 
RIP dereva. Daah ila hii njia inaita sana asee. yaani kila ukikanyagia waona kama gari haiendi hasa pale bondeni.
 
Habari za asubuhi, kuna ajali imetokea hapa maeneo ya africana mbezi asubuhi hii ambapo gari dogo aina ya mark x limeparamia kingo la daraja na kuteketea kabisa pamoja na dereva wake ambaye naye ametaketea kabisa na baadhi ya viuongo vyake viko bado eneo la ajali. Hivyo kama kuna mtu ambaye anawasiwasi wa kupotelewa na rafiki au ndugu mwenye gari kama hilo afike eneo la tukio kwa ajili ya kuvisitiri baadhi ya viungo ambavyo polisi walivisahau ndani ya gari la marehemu.
attachment.php

attachment.php
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1414310546.784274.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1414310546.784274.jpg
    120.7 KB · Views: 6,922
  • ImageUploadedByJamiiForums1414310595.730203.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1414310595.730203.jpg
    152.5 KB · Views: 11,218
Back
Top Bottom