Ajali mbaya Kibamba - Dar

Ajali mbaya Kibamba - Dar

Barabara zetu ni noma hazifai yaani hizi ajali hazitokaa na kuisha kamwe,

Barabara zinajengwa finyu, zina mashimo ,mabonde kona mbaya zingine zinateleza wakati wa mvua hawaweki viangalisho vya hatari za uterezi,

wanaweka alama za uongo mfano kimbia speed zaidi ya 50 lakini unakutana na bonge la shimo barabarani hiko ndio kilinikuta juzi nikiwa speed 140 ktk maeneo ya kuingia Magu ukiwa umetokea njia ya sirari yaani utadhani hilo ni tego lao hilimradi gari lianguke majambazi yaje kuchukua fedha wagawane na hao wanaoacha mashimo kwenye barabara huku wakiyatizama na wakati ni jukumu lao kuyafukia hayo mashimo.

Tuvumilie tu! kamwe hatutokuwa na amani mpaka kufa kwetu!!! tofauti na Nchi zigine wanakula neema tu!

Mema ya Nchi tutayasikilizia tu kwa jirani zetu!

Rest in peace.
 
Kuna jamaa hapa ofisini ameiona hiyo wakati anapita eneo la tukio anasema hakuna mtu anaweza kutoka mzima. Kwa kawaidia daladala linabeba watu zaidi ya 30 hadi 40 mida na asubuhi - My GOD.

ooh my nazidi kuteseka moyoni !
 
Mimi nadhani ni vema serikali ikazuia malori kusafiri mchana, inaweza kupunguza ajali za malori na mabasi (ingawa hii haihusiani)
 
imebidi nimpigie simu wife ''kuhakikisha kama yupo salama''!....hii barabara natamani kuhama mbezi
 
aaaagh...ngoja nimcheki switii maana anakaa mitaa ya kibamba ,kasalimika kweli
 
Inasikitisha sana. Hawa madereva wa malori mara nyingi wanakuwa wazembe na wengine wanakuwa wamechoka mno na hata kusinzia barabarani. Pole sana kwa wafiwa na majeruhi.
 
mimi nadhani ni vema serikali ikazuia malori kusafiri mchana, inaweza kupunguza ajali za malori na mabasi (ingawa hii haihusiani)

mkuu umeongea hoja yenye maana kubwa!!!!
Malori yasafiri usiku magari ya abiria yasafiri mchana.
Lakini tatizo lingine kubwa ni madereva kutokuwa makini kabisa ktk uendeshaji sijui ni uchovu wa kazi au makusudi.
Hawa wa daladala utakuta anaamka saa 10 alfajiri analala saa 6 usiku atapumzika saa ngapi?
Madereva wanaoendesha mabasi ya mkoani utakuta anaanza safari saa 12 asubuhi mpaka kuimaliza safari ni usiku saa 1 .
Dereva huyohuyo anatakiwa alirudishe basi kesho yake tena safari ianze saa 12 asubuhi mpaka saa 1 usiku
atampuzika saa ngapi?
Ni kampuni chache zenye kuwapa mapumziko madereva wao mfano dar express, sumry, scandinavia na hood ,ndio maana husikii ajali ktk hizi kampuni.
Hizi kampuni zinaajiri madereva makini!
 
poleni sana wandugu na majeruhi kwa ujumla mungu yupo pamoja nanyi atawapa rehema na baraka tele
 
Sasa tukisema Malori yasafiri usiku tu mchana yatakuwa yanapaki wapi Yalabi toba,

Maloli yana haki kama magari mengine issue ni kuboresha njia na kufufua Treni maana Malori yamekuwa mengi baada ya usafiri wa treni kuondolewa na wamiliki.

Chamsingi Lori litoke Dar likielekea labda tuseme Babati unadhani itamchukua sikungapi mpaka afike babati maana barabara ni mbaya kama barabara zingekuwa nzuri Madereva wamabasi/malori wangekuwa hawachoki na pia wangekuwa hawana haraka maana kwenye njia mbaya sehemu ya nusu saa unaweza tembea saa 4 mpaka 5 sasa wewe unateemea hizi hajari zitaisha kweli wakati mtu katembea kipande kibovu sasa akiona kabarabara kametulia lazima hasira zake ziishie hapo.
 
Poleni ndugu zangu wote mliofiwa, na mliopatwa na umauti, Mungu awapumzishe
 
i am told kwamba HAKUNA ALIYEPONA


Ohh Lord have mercy!!!!!!!!! Ni jana tu, tulikuwa tunamaumivu ya ajali ya hekima lakini kabla hilo halijapoa tena msumari wa moto juu ya kidonda. Mungu tusaidie!!!!!!!!!!!!

Wafiwa Mungu awape faraja yake yeye mwenyewe.
 
Inasikitisha sana. Hawa madereva wa malori mara nyingi wanakuwa wazembe na wengine wanakuwa wamechoka mno na hata kusinzia barabarani. Pole sana kwa wafiwa na majeruhi.

KWANZA POLENI WAFIWA

lakini hilo la Madereva wa Maroli kuwa wazembe sio kweli kabisa, Nadhani hawa ndio miongoni mwa Madereva walio makini zaidi kuliko wa Mabasi na Madaladala, sina uhakika na hii ajali ni nani mwenye makosa

lakini chamuhimu sio kutafuta nani mwenye makosa bali ni kuangalia chanzo cha ajali na kutafutia collective actions

1: hiyo Barabara ya Morogoro ni nyembamba sana
2: ni kitu cha ajabu kukuta highway ina bumps, nadhani hii ni Tanzania tu na mara nyingi ni chanzo kikubwa cha ajali
3: speeding, especially kwa Madaladala kuwahi vichwa
4: Fatigue kwa hao madereva (Daladala na Maroli)
5: wengi wa hao Madereva (Daladala) sio compitent na wengi ni wa vijiweni tu kwa kiasi kikubwa na mara nyingi wanajua kuondoa gari bila kuwa na extra skills (defensive driving)
6: carelessness
 
Poleni sana jamani. Mungua awape subira na awatie nguvu katika kipindi hiki.
 
Back
Top Bottom