Ajali mbaya: Basi la Sumry laua 14 huko Singida!

Ajali mbaya: Basi la Sumry laua 14 huko Singida!

Poleni wafiwa.
Ajali zinakatisha maisha ya watu sana siku hizi!!
 
hivi ni 14 au 19 maana nimesikia RFA wamesema 19 na majeruhi 8...
 
Huyu Sumry naye amezidi uchawi jamani. Yaani mabasi yake hakuna miezi miwili kupita bila kusikia ajali ya Sumry. Hachukuliwi hatua kwa kuwa mtoto wa mkulima ana hisa zake pale!

Nilitegemea jf members wanafikiri zaidi GT, kumbe watu wanafikiri kiwangu hiki cha UCHAWI!!! Kwanini watu tusifikiri zaidi kidogo kujua mazingira yaliyosababisha ajali ambayo itasaidia siku za mbeleni kuliko tukawa wavivu au tukajizuia na kuishia hapo kwenye uchawi. Sasa itafika wakati kila ajali jibu litakua UCHAWI au KAFARA?.
 
Nilitegemea jf members wanafikiri zaidi GT, kumbe watu wanafikiri kiwangu hiki cha UCHAWI!!! Kwanini watu tusifikiri zaidi kidogo kujua mazingira yaliyosababisha ajali ambayo itasaidia siku za mbeleni kuliko tukawa wavivu au tukajizuia na kuishia hapo kwenye uchawi. Sasa itafika wakati kila ajali jibu litakua UCHAWI au KAFARA?.

hayo ni maoni yake pia vitu kama hvo vipo na vinatokeaga sana tu R.i.p wote
 
Watanzania wengi sana wanapoteza maisha na ajali za barabarani. Poleni sana wafia
lakini pia madereva tuwe makini sana, na wananchi wawe makini.
 
jamani poleni hilo basi lilikuwa linatokea wapi kwenda wapi pengine kuna ndugu zetu humo
Mkuu uliishia kusoma title tu? Ni Sumri ikitokea Kigoma kwenda Dar ktk kijiji cha Ikungi Mkoani Singida. May their souls R.I.P
 
Imetokea usiku huu ajali mbaya maeneo ya Ikungi, Singida ikilihusisha basi la Sumry linalosafiri kati ya Kigoma-Dar.

Inasemekana mwendesha baiskeli alikuwa akivuka barabara lori likamgonga ghafla wanakijiji wamejaa kushangaa tukio na askari akipima ajali ndipo likatokea basi la Sumry na kugonga watu kumi na tatu pamoja na askari ni wa 14 mpaka sasa ndio idadi kamili ya waliopoteza maisha.

Mungu awalaze mahali pema Amina.

==========
ZAIDI:
==========
Vipi basi halijapigwa kiberiti
 
Iyo sehemu inaonyesha kwanza ni highway..!!
Pili basi lilikuwa kwenye Mwendo mkali ..!!
Hatulaumu ila Askari wazembe Kwa hilo lililotokea..
Wangechukua tahadhari mapema kulingana na sehemu yenyewe..!!
Ather ways Mungu azilale roho ZA marehemu mahali pema peponi..!!
 
Japokuwa askari alikuwa na wajibu wa kuwaondoa watu barabarani, lakini wananchi nao walipaswa kujua barabara ni eneo hatari sana. Askari angefanya kazi ngapi sasa?Wananchi wajifunze kutokukaa barabarani kushangaa ajali pindi zinapotokea ajali. Vinginevyo maafa haya yataendelea sana tu.
 
Nilikuwa naogopa kusema ukweli huu, wengi wataangamia

Haijalishi Mkuu ..!!
Hata Ulaya huwa wanashangaa
Tatizo ni Polic kwanini hawakuchukua tahadhari Kama nchi zingine..!!?
Usipende kulaumu tu Mkuu ..
Angalia source
 
Inakuwaje askari anapima ajali huku wanakijiji wakimshangaa barabarani? Kwanini askari huyo hakwambia hao with watoke?
 
Sasa itafikia 80% ya vifo vya watanzania kusababishwa na ajali za barabarani.....mungu awalaze pema peponi.
 
Hii inafanana na ile ya Rufiji https://www.jamiiforums.com/habari-...9-zaidi-ya-watu-20-wafa-ajalini-rufiji-2.html

lamini hakuna hatua. Askari hawakuchukua tahadhari kuwaondoa watu na kuweka alama mbali kuzuia magari mengine.

Kwa wale waliopitia mafunzo ya first aid wanajua kwamba hatua ya kwanza baada ya ajali ni kutengeneza mazingira ya kuhakikisha kwamba ajali hiyo haisababishi ajali nyingine. Nina imani hao jamaa zetu hawakuweka alama za kuonyesha watumiaji wengine wa barabara kwamba mbele kuna ajali hivyo waje wakiendesha pole pole.

RIP waliopoteza maisha.

Tiba
 
Back
Top Bottom