Mungu ndio anapanga kama kesho utaishi ama huishi, Yakobo 4:15, na siku zako ameshaziandika, Zaburi 139:16.
Lakini hii si kusema alichofanya ni kibaya, ipendeze isipendeze kwetu, kazi ya Mungu haina makosa. Torati 32:4
Mungu ameshapanga siku zako za kuishi lakini wewe ndiye wa kuamua na amekupa uwezo wa kuamua.
Nitakupa mfano, utakapokuwa na baba yako anayekuhimiza ufuate njia nzuri na ukakataa na kufuata njia zako mbaya, je, utasema baba yako ndiye aliyeyasababisha? Mungu anatuwazia mema lakini utakapoamua kufuata njia zako mbaya hawezi kukuzuia ndiyo maana ukapewa ufahamu wa kuchagua jema na baya.
Kwenye hiyo Torati 32:4 inasema Mungu ni mwaminifu, asiye na uovu, mwenye haki na adili, mtu mwenye sifa hizo anaweza akakutakia mabaya? Jibu ni hapana.