Airtel wapandisha gharama

Airtel wapandisha gharama

Aisee, Leo nimeshtushwa sana na bundle za Airtel. Nimezoea weka bundle za wiki kwa Tsh.6000 na zaidi ni hiyo 2GB.
Sasa Leo nakuta Tsh.6000 napata 500MB:A S 13: Jamani!!

Sasa basi kihesabu/Kiuchumi, 2GB kwa wiki ni sawa na 285mb kwa siku.:hand:
Ukiweka kila siku bundle ya Mb250 kwa Tsh.850, unakuwa palepale. Utatumia Tsh.5950 na utapata 1.75GB
Au weka kila siku bundle ya Mb300 kwa Tsh 1000, Utatumia Tsh.7000 na kupata 2.5GB.

Sawa na kusema:
Airtel wameongeza Shs. 1000 na kuongeza Mb100 au wamepunguza mb250 na kutoa Tsh.50.:A S 112:

Sasa basi waturudishie bundle yetu ya wiki kwa shs.7000 kwa 2.2GB, Tuwe pamoja. Hii itapunguza usumbufu tu. :sad:

Tuko sawasawa?
 
Ndugu wanajamvi ule mtandao uliojitangaza kama baba lao nadhani unaanza kuchoka.
Hawa jamaa wamebadili pakeji kama ifuatavyo:
Vifurushi Vya Siku
1. sh 399 unapata Dk 7 + 50 SMS + 20MB
2. sh 499 unapata Dk 13 + 300 SMS + 125MB
3. sh 649 unapata Dk 20 + 450SMS + 150MB
4. sh 849 unapata Dk 25 + 500SMS + 250MB
5. sh 999 unapata Dk 30 + 1000SMS + 300MB

VIfurushi Vya Mwezi:
1. sh 9999 unapewa Dk 200 + 500SMS + 500MB
2. sh 19999 unapewa Dk 450 + 1500SMS + 1Gb
3. sh 34999 unapewa Dk 800 + 2500SMS +1.5Gb

Tusubiri kule hakatwi mtu!!!!

Mlitarajia nini kutoka kwa #DogoLao na #Haitoshi ?

Wenzao Vodacom ni #KilioBombastic !
 
Duh nimenunua juzi bundle imeisha cjui imeishaje

unashangaa? tcra ndio kwanzaaaaaa wanachekelea minoti yao. nyie wenyewe si mliamini kwamba hao ndio baba lao na yatoshaaaaa? duuuh! pole weee! sasa wajua kwamba ni dogo lao na haitoshiiii? poleeee!
 
Wakati wa Nyerere tukitaka simu za nje tunakwenda "extelecom" ukisema u book kwa simu ya nyumbani unaweza kukaa mwezi hujapata simu, na bei ya chini ilikuwa 3000 kwa dakika 3, fikiria 3,000 ya mwaka 1980 ilikuwaje.

Sasa hivi hizi bei na hata zinapopanda na kushuka kwa ushindani, kwa sisi wa zamani, bado tunaona ni neema.

Madhara ya kutowajali watu wenye kipato cha chini!!!!!!
 
Madhara ya kutowajali watu wenye kipato cha chini!!!!!!

Wakati wa Nyerere walikuwa hawapo wenye vipatoo vya chini? tena tulikuwa masikini wa mwisho duniani na bei za kupiga simu ndio kama nilivyokuwekea. Enzi hizo ukiwa na simu ya nyumbani unaonekana wa maana kweli kweli. Leo mna neema hata wale wa kipato cha chini ya kima cha chini wana simu na wanadunda kama kawaida.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom