Airtel wameniibia kamisheni yangu ya mwezi wa nane

ajent45

Senior Member
Mar 20, 2017
158
162
Mimi ni wakala na nina laini za uwakala za mitandao yote: Tigo, Voda, Halotel, na Airtel. Sasa, kwenye hizi laini, Airtel ndiyo wanaongoza kwa kunipa kamisheni kubwa. Hii ni kwa sababu huku kwetu kuna wateja wengi wa mtandao huu. Pia, nina laini za lipa kwa simu kwa mitandao ya Voda, Tigo, na Airtel, ambazo ninazitumia.

Mwezi wa nane, Tigo wamenipa 77,000, Voda 78,000, Halotel 17,000, na Airtel nilishazoea kupata laki na chenji, lakini nakuta wamenipa 7,000. Nimeuliza kwa watu, eti kosa hela za lipa kwa simu kwa Airtel huwa naamishia laini ya uwakala, na majina yanafanana. Sasa, mbona mitandao mingine majina yanafanana na hawana shida na mimi? Napiga kazi na nategemea hapa, lakini wao wananiletea huu upuuzi.

Nilipiga huduma kwa wateja, na wao hawajui. Dah! Nimepigwa, naomba msaada.
 
kila siku wanatuma message kwa leo mara umepata 3000 mara 2700 mara 4000 halafu mwezi unaisha unanipa 7000 hizi hela zinaenda wapi nilizoambiwa nimepata kila siku huu ni wizi aiseee inauma sana unamweka mtu dukani unategemea upate hela wao wanaleta mambo ya hivyo aisee
 
Haya Maisha haya sikia simulizi kwa mwenzio omba yasikukute. Huenda kuna mtu ulimuhaidi kabisa hela lakini mchongo umebuma.
 
Ilishawahi noteka kwenye line ya tigo...nilikuwa na line mbili za uwakala tigo...kivumbi kinakuja ...nimepiga kazi hadi tarehe 30 line inasoma nina 180000 nyingine inasoma 104000 kamisheni imekuja kutoka nikapata 50000/ kwenye line ya 180000 na hiyo nyingine 104000 wakiniletea kama ilivyosoma.. nikawapigia simu hawana maelezo mara maelezo mazuri mara nimpigie wakala wangu mkuu nikachoka...mwezi unaofuatia wakaramba tena kilichofuatia ile line siitumiagi kabisa. Nikasema bora waifungie tu.mtu ushajiwekea malengo yako then wanakuharibia...
 
Ilishawahi noteka kwenye line ya tigo...nilikuwa na line mbili za uwakala tigo...kivumbi kinakuja ...nimepiga kazi hadi tarehe 30 line inasoma nina 180000 nyingine inasoma 104000 kamisheni imekuja kutoka nikapata 50000/ kwenye line ya 180000 na hiyo nyingine 104000 wakiniletea kama ilivyosoma.. nikawapigia simu hawana maelezo mara maelezo mazuri mara nimpigie wakala wangu mkuu nikachoka...mwezi unaofuatia wakaramba tena kilichofuatia ile line siitumiagi kabisa. Nikasema bora waifungie tu.mtu ushajiwekea malengo yako then wanakuharibia...

Fraud za lipa kwa simu ulzokua unafanya…ulifanya kupita kawaida.unalipisha watu alaf unatoa kwenye lain yako

Bila shaka kwenye lain hyo ya 180,000 hyo ndio kamishen kubwa kulko zote ulzowah kupata kwenye lain hyo…walidetect wakakubain wakakulamba kischo halali
 
Mimi ni wakala na nina laini za uwakala za mitandao yote: Tigo, Voda, Halotel, na Airtel. Sasa, kwenye hizi laini, Airtel ndiyo wanaongoza kwa kunipa kamisheni kubwa. Hii ni kwa sababu huku kwetu kuna wateja wengi wa mtandao huu. Pia, nina laini za lipa kwa simu kwa mitandao ya Voda, Tigo, na Airtel, ambazo ninazitumia.

Mwezi wa nane, Tigo wamenipa 77,000, Voda 78,000, Halotel 17,000, na Airtel nilishazoea kupata laki na chenji, lakini nakuta wamenipa 7,000. Nimeuliza kwa watu, eti kosa hela za lipa kwa simu kwa Airtel huwa naamishia laini ya uwakala, na majina yanafanana. Sasa, mbona mitandao mingine majina yanafanana na hawana shida na mimi? Napiga kazi na nategemea hapa, lakini wao wananiletea huu upuuzi.

Nilipiga huduma kwa wateja, na wao hawajui. Dah! Nimepigwa, naomba msaada.

Kwa uzoefu wangu,hakuna mtando unaoibia mtu kamishen hata siku 1

Moja/zote kat ya hizi n sababu ya kutolipwa kamishen

1.unagawa miamala kupita kawaida (too mucha)unakuta laki unaiweka mara 2/3 na kila siku

2.fraud za lipa unazojilipisha kwenye lain yako ya lipa airtel na unaitoa kweny till yako uwakala…usajili unafanana na wakichek n namba hyo tu ndio inatoa hela kila siku na muda uleule


Nm…hakuna pesa rahisi kijana,fuata taratibu za kutoa huduma.
 
Nenda Kwa wakala wako mkuu ndo anauhusika sio airtel ndio maana hata ulipopiga huduma Kwa wateja hawajui...!! Lazima utambue jinsi line za uwakala zinafanyaje kazi kiongozi
 
Nenda Kwa wakala wako mkuu ndo anauhusika sio airtel ndio maana hata ulipopiga huduma Kwa wateja hawajui...!! Lazima utambue jinsi line za uwakala zinafanyaje kazi kiongozi

Mfundishe humu kwa maelezo zaidi itasaidia wengi wanaosoma.

N.b. Mimi sifanyi hii biashara
 
Fraud za lipa kwa simu ulzokua unafanya…ulifanya kupita kawaida.unalipisha watu alaf unatoa kwenye lain yako

Bila shaka kwenye lain hyo ya 180,000 hyo ndio kamishen kubwa kulko zote ulzowah kupata kwenye lain hyo…walidetect wakakubain wakakulamba kischo halali
Hapana mkuu napataga zaidi ya hiyo mkuu...hiyo ni kawaida sana...ilivyobaki moja inapiga mpaka 250000 kwa mwezi...
 
Fraud za lipa kwa simu ulzokua unafanya…ulifanya kupita kawaida.unalipisha watu alaf unatoa kwenye lain yako

Bila shaka kwenye lain hyo ya 180,000 hyo ndio kamishen kubwa kulko zote ulzowah kupata kwenye lain hyo…walidetect wakakubain wakakulamba kischo halali
Sina line ya lipa yanyewe usajili wangu
 
Kwa uzoefu wangu,hakuna mtando unaoibia mtu kamishen hata siku 1

Moja/zote kat ya hizi n sababu ya kutolipwa kamishen

1.unagawa miamala kupita kawaida (too mucha)unakuta laki unaiweka mara 2/3 na kila siku

2.fraud za lipa unazojilipisha kwenye lain yako ya lipa airtel na unaitoa kweny till yako uwakala…usajili unafanana na wakichek n namba hyo tu ndio inatoa hela kila siku na muda uleule


Nm…hakuna pesa rahisi kijana,fuata taratibu za kutoa huduma.
Cha msingi ona wapi faida ni kubwa zaidi,Mimi voda commission ya mwezi august ilikuwa 670000 Nimekatwa nikaambulia 210000,kwangu Mimi sikuumia sana Kwani kupitia lipa nimetengeneza mil 3.3,na nilivyowapigia simu wakaniambia Huwa nagawa miamala nikasema ok maisha yaendelee
 
Back
Top Bottom