Habarini!, kuna ndugu yangu alichukua simu airtel kwa mkopo...simu yake ilipata hitilafu kidogo na akawarudishia ili waitengeneze...wakamuahidi baada ya wiki 3 watamrudishia...akalipa gharama ya matengenezo huku akiendelea kulipa malipo ya siku...mwezi wa pili sasa yaani ana wiki 6 sasa hawajamrudishia simu na wanamtaka aendelee kulipia....amewafata mara 4 na anajibiwa kuwa Bado haijafika...na asipolipa malipo ya siku anapigiwa simu wakimkosa anapigiwa aliyemdhamini kumsihi afanye malipo na simu wanayo wenyewe airtel. Ameona anatapeliwa waziwazi na kuniomba nimsaidie ila Mimi Sina hata pa kuanzia japo nimemjibu nitawatafuta airtel hewani ...
Naombeni msaada anayejua inatakiwa afanye Nini hapa alipofikia, anadai inaenda wiki ya Saba...asipolipa anapigiwa simu anatishwa...na Ile simu alipoirudisha airtel walimwambia atoe laini yake na atoe password zote za simu ndipo akawakabidhi...
Mwenye uelewa anisaidie afanye Nini katika hili?
NB: simu Hadi sasa amebakiza miezi 2 kumaliza mkopo
Naombeni msaada anayejua inatakiwa afanye Nini hapa alipofikia, anadai inaenda wiki ya Saba...asipolipa anapigiwa simu anatishwa...na Ile simu alipoirudisha airtel walimwambia atoe laini yake na atoe password zote za simu ndipo akawakabidhi...
Mwenye uelewa anisaidie afanye Nini katika hili?
NB: simu Hadi sasa amebakiza miezi 2 kumaliza mkopo