Airtel na kifo cha Sharo Milionea

Airtel na kifo cha Sharo Milionea

CharmingLady

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2012
Posts
18,304
Reaction score
12,997
Nilikuwa naangalia taarifa ya habari, mara wakaonesha lile tangazo la AIRTEL MONEY aliloshiriki Marehemu Sharo Milionea na Mzee Majuto.

Je ni haki kuendelea kulionesha lile tangazo??????
 
Si halali. Kwa mila za kitanzania, bado watu wana machungu. Wangeacha kwanza wazazi wamalize kuomboleza. Airtel , chunga msijekujikuta mmewaudhi wateja badala ya kuwavuitia. Hamtapata hasara kwa kutorusha hilo tangazo
 
Airtel wako kimkataba zaidi, hata hivyo tangazo bado lina mvuto na ndiyo maana wanasema vigezo na masharti kuzingatiwa. Kwa hiyo mpaka muda wa mkataba uishe.
 
Mie mwenyewe nilistuka sana nilipoliona hilo Tangazo! Kwa mtazamo wangu hii siyo sawa.........
 
Mie mwenyewe nilistuka sana nilipoliona hilo Tangazo! Kwa mtazamo wangu hii siyo sawa.........

Sio sawa hata kidogo..... hata kama kisheria wako sawa ila kimaadili haipendezi......

Wapi my lawyer Ruttashobolwa, sheria inasemaje????
 
Last edited by a moderator:
Haiko sawa, nilishangaa jana kuliona, aah ngoja wanasheria wwaje watwambie.
 
Lazima waliomba ridhaa ya familia ya marehem, halafu ni njia iliyobaki ya kumuenzi sharo, kuonesha uwezo wake wakati wa uhai wake. Mi natamani siku nikifa, kama kuna mambo nimewafanyia watanzania, basi yatangazwe na wengine waige u-machachari wangu. Good job shalo...tutakukumbuka kwa hilo shalo men, ingawa umekufa, lakini mambozi yako yatabaki kuwa kumbukumbu mhimu sana kwa vizazi vijavyo
 
Pia inawezekana hapo kwenye kituo cha tv mrushamatangazo alijisahaua akalidumbukiza..!! Ni matumain yetu airtel watakuwa wameshatoa taarifa mapema ya kuzuiwa hilo tangazo lisionyeshwe!!
 
Back
Top Bottom