ZALEOLEO
Senior Member
- Oct 11, 2011
- 116
- 18
Airtel kama mnaipenda kampuni yenu bora mkirudishe kitengo chenu cha customer care mikononi mwenu,hao ndugu zenu kampuni ya SPANCO mlowapa kitengo cha customer care kazi inawashinda,kwanza inawalipa wafanyakazi mishahara ya kitoto,hivi kweli maisha ya sasa unaweza kumpa mtu mshahara wa sh 150,000? ikikatwa kodi inabaki 130,000! rate ya watu kuacha kazi iko juu na nyny chini ya hao SPANCO mnaajiri tu,floor imejaa watu mpk AC zimekufa sasa yanatumika mafeni,hv jengo kubwa kama lile unaweza kutumia feni kweli? nafasi zenyewe wanapeana kwa kujuana,wafanyakazi wanaongozwa na watu wasiojitambua hata kidogo,kiongozi hajui majukumu yake,mtu atakayewaita ni vibaraka wa wa wahidi wala sitashangaa! huduma zinazotolewa ni mbovu kupita maelezo na wala sio kosa la wahudumu sababu ni kwamba hao SPANCO wanataka wingi wa takwimu za simu zilizopokelewa kwa siku na wala hawaangalii ubora wa huduma! kampuni inajifia kifo kisicho na kilio!