Surya
JF-Expert Member
- Jun 7, 2015
- 9,761
- 15,577
Katika kueleza makundi haya mawili ya waamini wa imani ijulikanayo kama Wakristo (maana yake wafuasi wa Yesu) kumekua bado na mzozo mkubwa hadi leo hii kuhusu mambo Muhimu sana kuhusu imani au dini hii.
1. Sheria (Torati)
2. Neema (Kuokolewa kwa imani)
Binafsi nimefatilia sheria sana sheria ambazo Waebrania wanazichukulia kama sheria za Mungu.
Kuhusu neema iliyoletwa na Yesu Kristo.
Waebrania 7:11-12
11 Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo); kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?
12 Maana ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike.
TUNAPATA MAKUNDI MAWILI:
1. Wanaotaka sheria zote ziendelee kufatwa.
2. Na wanaosema sheria sio lazima tena. Kwanza ni nyingi na ngumu kuzishika zote.
Wagalatia 2:16
hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.
Sheria (Torati)
Katika Torati (vitabu vitano vya kwanza vya Biblia, yaani Musa), kuna aina mbili za "amri" ambazo mara nyingi hujadiliwa:
Amri Kumi (Decalogue): Hizi ndizo amri kuu zinazojulikana na wengi, ambazo Mungu alimpa Musa kwenye Mlima Sinai. Zimeorodheshwa katika kitabu cha Kutoka 20:1-17 na Kumbukumbu la Torati 5:6-21. Hizi kumi ndio msingi wa maadili na sheria nyingi.
Amri Zote (Mitzvot): Kijadi, Wayahudi wanaamini kwamba Torati ina jumla ya amri 613 (zinazojulikana kama "Mitzvot 613"). Hizi 613 zinajumuisha amri kumi na sheria nyingine nyingi zinazohusu nyanja mbalimbali za maisha, kama vile ibada, sheria za kijamii, chakula, usafi, na kadhalika. Amri hizi 613 zimegawanywa katika amri chanya (mambo ya kufanya) na amri hasi (mambo ya kutokufanya).
Kwa hivyo, jibu fupi ni kwamba kuna Amri Kumi ambazo ni muhimu sana na zinazojulikana sana, lakini kwa ujumla, mila ya Kiyahudi inafundisha kuwa kuna amri 613 katika Torati.
Sheria zilizovyunjwa na wanafunzi wa Yesu.
1. Kufanya kazi siku ya sabato.
2. Kuchangamana na wasio wayahudi.
3.
Hadi Yesu kuondoka bado Petro alikuwa anaaamini kwamba Kujazwa roho mtakatifu ni haki ya wayahudi peke yao, mataifa mengine haiwahusu.
Huitaji Torati kujua Mungu hapendi nini na anapenda nini mfano mzuri,
Isaka na ibrahimu waliishi vipi na kuwa karibu na Mungu kipindi ambacho torati haikuwepo bado ???
Kanisa la leo haliwezi kuhubiri neema (grace) kwani ulaji wao wa sadaka unatokana na sheria iliyotolewa na Musa katika Torati kuhusu matoleo, na ikumbukwe kuwa Mungu aliagiza matoleo kutoka katika Shamba na Mifugo, ambao walitokana na Ardhi ambayo Mungu kawapa.
Sasa wewe Mkristo wa leo unaambiwa toa fungu la Kumi na huku hakuna Ardhi umepewa kama urithi.
Petro atetea sio lazima Kutahiriwa
(Hapa kanisa lilifanya na kikao kupata maamuzi)
Matendo ya Mitume 15:10-11
10 Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua.
11 Bali twaamini kwamba tutaokoka kwa neema ya Bwana Yesu vile vile kama wao.
Niulize Swali
Kwanini mbaraka wa Isaka kwa mwanaume wa kwanza wa kiume uliweza kuibiwa na mtoto wa pili ambaye ni Yakobo ??
Inawezekana vip mbaraka kuibiwa ?? unaiba nguvu za Mungu ??
Yakobo alikuwa Muongo na Tapeli na alishindana na Ndugu yake tangu tumboni, akamshika kisigino pacha wake ambaye ni kaka yake.
kumvuta kisigino ilikuwa ni ishara.
Bado Mungu anajionesha na Kusema Nimempenda Yakobo bali Esau nimemkataa.
Upo kundi gani.
1. Kuwa mshika sheria, au
2. Kuwa msikivu na mtii.
3. Vyote viwili.
Nimewasikiliza wahubiri wakubwa duniani waalimu na Manabii
Je unawajua wahubiri wakubwa duniani na misimamo yao kuhusus Sheria na Neema ???
1. Billy Graham
2. Myles Munroe
Kwasasa manabii wakubwa dunia na maarufu ninao wajua na waofundisha mambo mazito.
1. Prophet Ubert Angel
2. Prophet Lovy Elias
3. Prophet Passion Java
Hawa wote ni manabii Giants kutoka Afrika, kama baba yake wa kiroho na Musa alikuwa Muafrika, na Musa akaowa Mkushi.
Bila kuwasahau waalimu wazuri.
1. Apostle Miz Mzwakhe Tancredi (South Africa)
2. Paul S. Joshua.
3. Prophet David Rauf
Huwezi kuongeza Nguvu au viwango vyako vya kiroho, Bila kumuelewa Mungu kwa usahihi zaidi.🙏🏾
1. Sheria (Torati)
2. Neema (Kuokolewa kwa imani)
Binafsi nimefatilia sheria sana sheria ambazo Waebrania wanazichukulia kama sheria za Mungu.
Kuhusu neema iliyoletwa na Yesu Kristo.
Waebrania 7:11-12
11 Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo); kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?
12 Maana ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike.
TUNAPATA MAKUNDI MAWILI:
1. Wanaotaka sheria zote ziendelee kufatwa.
2. Na wanaosema sheria sio lazima tena. Kwanza ni nyingi na ngumu kuzishika zote.
Wagalatia 2:16
hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.
Sheria (Torati)
Katika Torati (vitabu vitano vya kwanza vya Biblia, yaani Musa), kuna aina mbili za "amri" ambazo mara nyingi hujadiliwa:
Amri Kumi (Decalogue): Hizi ndizo amri kuu zinazojulikana na wengi, ambazo Mungu alimpa Musa kwenye Mlima Sinai. Zimeorodheshwa katika kitabu cha Kutoka 20:1-17 na Kumbukumbu la Torati 5:6-21. Hizi kumi ndio msingi wa maadili na sheria nyingi.
Amri Zote (Mitzvot): Kijadi, Wayahudi wanaamini kwamba Torati ina jumla ya amri 613 (zinazojulikana kama "Mitzvot 613"). Hizi 613 zinajumuisha amri kumi na sheria nyingine nyingi zinazohusu nyanja mbalimbali za maisha, kama vile ibada, sheria za kijamii, chakula, usafi, na kadhalika. Amri hizi 613 zimegawanywa katika amri chanya (mambo ya kufanya) na amri hasi (mambo ya kutokufanya).
Kwa hivyo, jibu fupi ni kwamba kuna Amri Kumi ambazo ni muhimu sana na zinazojulikana sana, lakini kwa ujumla, mila ya Kiyahudi inafundisha kuwa kuna amri 613 katika Torati.
Sheria zilizovyunjwa na wanafunzi wa Yesu.
1. Kufanya kazi siku ya sabato.
2. Kuchangamana na wasio wayahudi.
3.
Hadi Yesu kuondoka bado Petro alikuwa anaaamini kwamba Kujazwa roho mtakatifu ni haki ya wayahudi peke yao, mataifa mengine haiwahusu.
Huitaji Torati kujua Mungu hapendi nini na anapenda nini mfano mzuri,
Isaka na ibrahimu waliishi vipi na kuwa karibu na Mungu kipindi ambacho torati haikuwepo bado ???
Kanisa la leo haliwezi kuhubiri neema (grace) kwani ulaji wao wa sadaka unatokana na sheria iliyotolewa na Musa katika Torati kuhusu matoleo, na ikumbukwe kuwa Mungu aliagiza matoleo kutoka katika Shamba na Mifugo, ambao walitokana na Ardhi ambayo Mungu kawapa.
Sasa wewe Mkristo wa leo unaambiwa toa fungu la Kumi na huku hakuna Ardhi umepewa kama urithi.
Petro atetea sio lazima Kutahiriwa
(Hapa kanisa lilifanya na kikao kupata maamuzi)
Matendo ya Mitume 15:10-11
10 Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua.
11 Bali twaamini kwamba tutaokoka kwa neema ya Bwana Yesu vile vile kama wao.
Niulize Swali
Kwanini mbaraka wa Isaka kwa mwanaume wa kwanza wa kiume uliweza kuibiwa na mtoto wa pili ambaye ni Yakobo ??
Inawezekana vip mbaraka kuibiwa ?? unaiba nguvu za Mungu ??
Yakobo alikuwa Muongo na Tapeli na alishindana na Ndugu yake tangu tumboni, akamshika kisigino pacha wake ambaye ni kaka yake.
kumvuta kisigino ilikuwa ni ishara.
Bado Mungu anajionesha na Kusema Nimempenda Yakobo bali Esau nimemkataa.
Upo kundi gani.
1. Kuwa mshika sheria, au
2. Kuwa msikivu na mtii.
3. Vyote viwili.
Nimewasikiliza wahubiri wakubwa duniani waalimu na Manabii
Je unawajua wahubiri wakubwa duniani na misimamo yao kuhusus Sheria na Neema ???
1. Billy Graham
2. Myles Munroe
Kwasasa manabii wakubwa dunia na maarufu ninao wajua na waofundisha mambo mazito.
1. Prophet Ubert Angel
2. Prophet Lovy Elias
3. Prophet Passion Java
Hawa wote ni manabii Giants kutoka Afrika, kama baba yake wa kiroho na Musa alikuwa Muafrika, na Musa akaowa Mkushi.
Bila kuwasahau waalimu wazuri.
1. Apostle Miz Mzwakhe Tancredi (South Africa)
2. Paul S. Joshua.
3. Prophet David Rauf
Huwezi kuongeza Nguvu au viwango vyako vya kiroho, Bila kumuelewa Mungu kwa usahihi zaidi.🙏🏾