Aina kuu tatu za ulevi wa pombe

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,238
12,753
Ulevi wa pombe haupo wa aina moja. Kuna aina kuu tatu.

1. Hamu kali ya pombe. Ulevi wa aina hii ni ule ambao mtu anakuwa na hamu kali sana ya pombe kiasi kwamba hawezi kufanya wala kuwaza jambo lingine mpaka aipate.

2. Kushindwa kujizuia kutoendelea kunywa. Mlevi wa aina hii akianza kunywa hajui kusema imetosha. Mtu wa hivi anaweza kuwa hana hata hamu ya pombe. Anaweza kwa muda mrefu asifikirie wala kunywa pombe. Lakini mara tu aanzapo kunywa huwa hawezi kujizuia. Atakunywa hadi atazima. Kama alikuwa na pesa ni mpaka ziishe.

3. Aina ya tatu ni pombe kutawala mwili. Mlevi wa aina hii ni kuwa mwili wake hauwezi kufanya kazi bila pombe. Mtu wa aina hii akikosa pombe anakuwa kama mgonjwa. Mtu wa hivi akikosa pombe anaweza hata kufa.

Unaufahamu ulevi wa aina gani?
 
Ulevi wa pombe haupo wa aina moja. Kuna aina kuu tatu.

1. Hamu kali ya pombe. Ulevi wa aina hii ni ule ambao mtu anakuwa na haku kali sana ya pombe kiasi kwamba hawezi kufanya wala kuwaza jambo lingine mpaka aipate.

2. Kushindwa kujizuia kutoendelea kunywa. Mlevi wa aina hii akianza kunywa hajui kusema imetosha. Mtu wa hivi anaweza kuwa hana hata hamu ya pombe. Anaweza kwa muda mrefu asifikirie wala kunywa pombe. Lakini mara tu aanzapo kunywa huwa hawezi kujizuia. Atakunywa hadi atazima. Kama alikuwa na pesa ni mpaka ziishe.

3. Aina ya tatu ni pombe kutawala mwili. Mlevi wa aina hii ni kuwa mwili wake hauwezi kufanya kazi bila pombe. Mtu wa aina hii akikosa pombe anakuwa kama mgonjwa. Mtu wa hivi akikosa pombe anaweza hata kufa.

Unaufahamu ulevi wa aina gani?
Namba mbili.
tupe na suluhisho tafadhari.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ya pili nimekumbuka kuna mmama alikuwa amepanga jirani yangu. Yeye anapiga hata miezi mitatu hajaonja pombe. Anapendezaa ananawirii.

Balaa lake siku mtu amspoil hata na chupa moja. Ndio anakuwa kafungulia .. hapo atakunywa pombe na kuzunguka na barabara na kucheza mziki hata wiki nzima. Atakonda atapauka hadi huruma. Akiacha kunywa pombe baada ya hiyo wiki anakuwa hoii anaumwaa hata kutoka ndani hawezi.
 
Acha maneno mengi wewe
IMG_20230424_152902_025.jpg
 
Namba mbili inanihusu. Naweza Kaa hata wiki mbili siku niyatimbe naweza Kaa hata siku mbili ndo nipate hamu ya kula. Kuna siku nimeyatimba nililala masaa kumi na tisa bila kujitambua kiufupi nlikua Kama nmekufa kwa huo muda
 
Mimi ulevi wangu ni kunywa juice nakunywa weee mpaka nakunywa tena.

Nachanganya , passion, embe, karoti, ndizi mbivu na nanasi aisee.
 
Ulevi wa pombe haupo wa aina moja. Kuna aina kuu tatu.

1. Hamu kali ya pombe. Ulevi wa aina hii ni ule ambao mtu anakuwa na hamu kali sana ya pombe kiasi kwamba hawezi kufanya wala kuwaza jambo lingine mpaka aipate.

2. Kushindwa kujizuia kutoendelea kunywa. Mlevi wa aina hii akianza kunywa hajui kusema imetosha. Mtu wa hivi anaweza kuwa hana hata hamu ya pombe. Anaweza kwa muda mrefu asifikirie wala kunywa pombe. Lakini mara tu aanzapo kunywa huwa hawezi kujizuia. Atakunywa hadi atazima. Kama alikuwa na pesa ni mpaka ziishe.

3. Aina ya tatu ni pombe kutawala mwili. Mlevi wa aina hii ni kuwa mwili wake hauwezi kufanya kazi bila pombe. Mtu wa aina hii akikosa pombe anakuwa kama mgonjwa. Mtu wa hivi akikosa pombe anaweza hata kufa.

Unaufahamu ulevi wa aina gani?
Namba 2 nna uhakika imeenda na wengi
 
Back
Top Bottom