Aina gani ya socket switch itanitanifaa kwa matumizi haya?

Aina gani ya socket switch itanitanifaa kwa matumizi haya?

G M S

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2011
Posts
502
Reaction score
53
Natumia hita kila baada ya wiki kadhaa inayeyuka, nimejaribu kuweka pamoja na multi plug ya tronic ila bado imeyeyuka je nitumie ipi jamani? Kuna jamaa kanishauri nijaribu socket switch ambayo ni round! Msaada wenu plz?
 
Pole sana! Kwanza soma hita ina watts ngapi? Kama ina 1,800w/220v ambayo utapata 8.18Amps. Hapo utakuwa na chini ya 13Amps ambayo ni rating ya kawaida kwenye switch socket. Ukitumia top plug na switch socket ya 15A si vibaya mwingine itakuwa bora. Kikubwa hakikisha wire wa heater, switch socket na top plug vyote ni original ili kuondoa heating kwenye wire na hivyo vifaa vingine.
 
Usitumie mult plug kwenye hiyo hita chomeka direct kwenye socket na hakikisha vyote ni original.
 
Pole sana! Kwanza soma hita ina watts ngapi? Kama ina 1,800w/220v ambayo utapata 8.18Amps. Hapo utakuwa na chini ya 13Amps ambayo ni rating ya kawaida kwenye switch socket. Ukitumia top plug na switch socket ya 15A si vibaya mwingine itakuwa bora. Kikubwa hakikisha wire wa heater, switch socket na top plug vyote ni original ili kuondoa heating kwenye wire na hivyo vifaa vingine.

Mkuu kinadharia (concept) uko sahihi, ila kwa kuongezea tuu hapo katika hizo calculation uliyomwambia ajaribu kufanya. Ni kwamba umeme wa majumbani ni A.C hivyo anatakiwa aubadili kwenda katika RMS(root mean square) standards za vyote current na Voltage ndio atakuwa sahihi zaidi.

Voltage RMS 〓 0.707 * Voltage in A.C
 
Pole sana! Kwanza soma hita ina watts ngapi? Kama ina 1,800w/220v ambayo utapata 8.18Amps. Hapo utakuwa na chini ya 13Amps ambayo ni rating ya kawaida kwenye switch socket. Ukitumia top plug na switch socket ya 15A si vibaya mwingine itakuwa bora. Kikubwa hakikisha wire wa heater, switch socket na top plug vyote ni original ili kuondoa heating kwenye wire na hivyo vifaa vingine.

heater yenyewe imeandikwa 10/16 A
af ni watt 1500/220v ilikuwa inanitisha hyo 10 over 16A ila naona huenda ipo katikati ila haijafika 16A ILA KINGINE MSAADA NTAJUAJE SOCKET SWITCH NI 15A NA MADUKANI WANATOFAUTISHA KWA MAJINA?
 
heater yenyewe imeandikwa 10/16 A
af ni watt 1500/220v ilikuwa inanitisha hyo 10 over 16A ila naona huenda ipo katikati ila haijafika 16A ILA KINGINE MSAADA NTAJUAJE SOCKET SWITCH NI 15A NA MADUKANI WANATOFAUTISHA KWA MAJINA?

Hiyo 10/16A ni range as umeme huwa unaflactuate sana. Ila hapo mkuu mathematically, heater yako inakula approximately 13.7 Amperes katika mazingira ya kawaida kwa maana kwamba.

Power. 〓 Vrms * Irms
1500w 〓 0.707 Vac * 0.707 Iac
1500w 〓 0.5 (Vac * Iac)
3000w 〓 220 * Iac
Finally,
Iac 〓 13.64A.

Kwa hiyo kazi uliyonayo hapo ni kuhakikisha socket unayoitafuta inasupport hiyo rating ya current.

Sidhani socket inayosupport amperes 15 itafaa sana. Kwa maana inabidi utafute inayozidi amperes 16 ili uwe safe zaidi.
 
Tofauti kati ya switch socket ya 13A na 15A ni hizo plug zake 3.13A zipo flat na 15A zipo round na ni kubwa kiasi.
 
Kaka unachanga Habari! Ina maana hiyo heater yake haifai hata kwa plug na switch socket ya 15A?
Fanya hesabu hii kwanza!
P = V * I
P=X
V=220V
I=15A

Soln;
P = 220 * 15
P = 3300W

3300 - 1500= 1800watt

Umeelewa?
 
0.707 umetumia fomula gani kuipata mkuu?

Mkuu factor ya 0.707 derivation yake ni ndefu kidogo, ambapo siwezi kuiweka hapa. Hiyo ni factor ambayo inahusianisha RMS quantity(either voltage ama current) na A.C quantity (either quantity).

Katika mfumo wa umeme, kuna kitu kinaitwa A.C na D.C hope unazijua hizi terminology. A.C ni umeme unaoflactuate kutokana na muda unavyokwenda. Bali D.C hubaki steady kadri muda unavyokwenda.

Ili kupata kiasi cha power ambayo device hutumia, D.C system hutumika katika mahesabu yake kwa kuwa quqntities (voltage na current) katika DC huwa hazibadilikibadiliki kadri muda unavyokwenda.

Ila katika A.C system inabidi tubadili parameters kwa kuwa itakuwa ni uongo ukachukua na kuzitumia kama zilivyo kwa kuwa haziko steady. Hivyo basi kwa lugha rahisi inabidi zitafutiwe wastani na huo wastani ndio utumike katika mahesabu.

Hivyo basi RMS ni kizio/mfumo unaojaribu kuoanisha quantities za A.C as if zingekuwa D.C ili uweze kupata uhalisia ni kiasi gani haswa cha umeme kitatumika kimahesabu. Kwa lugha nyingine RMS ni kama wastani.

Hivyo basi 0.707 ndiyo factor ambayo ikizidishwa katika peak value ya A.C quantity (voltage or current). Huofanya ioanike na Quantity za D.C. Hope hapo mkuu umenipata.
 
Umesomeka ila point hapa mtoa mada moja kwa moja ameelekea kwenye AC power na si DC power. Kwa nilivyoelewa ufafanuzi wako umezama sana kwenye DC na AC kuliko kumsaidia mtoa mada.
 
Tuko pamoja mkuu, hayo yalikuwa ni maelezo tuu katika kile ulichouliza, ila solution ya tatizo la G spanner ni kwamba ajaribu kutafuta socket ambazo zinasuport current kubwa zaidi ya 16A.
 
Mkuu kinadharia (concept) uko sahihi, ila kwa kuongezea tuu hapo katika hizo calculation uliyomwambia ajaribu kufanya. Ni kwamba umeme wa majumbani ni A.C hivyo anatakiwa aubadili kwenda katika RMS(root mean square) standards za vyote current na Voltage ndio atakuwa sahihi zaidi.

Voltage RMS 〓 0.707 * Voltage in A.C

Mkuu siku zote Rating ya Vifaa vinavyotumia A.C wanatumia RMS values so huna Haja Kufanya conversions. Kwahiyo mkuu Makbel yupo sahihi kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Natumia hita kila baada ya wiki kadhaa inayeyuka, nimejaribu kuweka pamoja na multi plug ya tronic ila bado imeyeyuka je nitumie ipi jamani? Kuna jamaa kanishauri nijaribu socket switch ambayo ni round! Msaada wenu plz?

Mkuu nilitaka nikushauri ila maelezo yameniacha njia panda sijaelewa ni kitu gani kati ya heater na socket kinachoyeyuka. Kama ni Heater ni sehemu gani inayeyuka?
 
Mkuu nilitaka nikushauri ila maelezo yameniacha njia panda sijaelewa ni kitu gani kati ya heater na socket kinachoyeyuka. Kama ni Heater ni sehemu gani inayeyuka?

kinachoyeyuka ni socket switch mkuu! Mara nyingine pamoja na multiplug kwahyo tatizo ni socket switch na huwa inaskika harufu kabisa na mwisho wa siku hata on/of button inaganda kabisa kutokana na kuwa imeyeyuka na kuganda ni hvyo!
 
kinachoyeyuka ni socket switch mkuu! Mara nyingine pamoja na multiplug kwahyo tatizo ni socket switch na huwa inaskika harufu kabisa na mwisho wa siku hata on/of button inaganda kabisa kutokana na kuwa imeyeyuka na kuganda ni hvyo!
Ok nimekupata sasa tatizo lako litakuwa kati ya Haya hapa(Assumption: Unatumia Immersion Type water Heater)
1.Heater itakuwa inatumika mda mrefu na ku draw current kubwa kupita uwezo wa socket, na hivyo kusababisha heat ambayo inmelt hiyo socket
2.Socket haishikani vizuri na plug na hivyo kutengeneza cheche wakati ikifanya kazi.
3.Heater nyingi za zamani huwa zina draw current kubwa pale unapowasha hii husababisha cheche na baada muda huweza kuyeyusha button ya kuwashia.(Kwa sababu hazina Thermostat)
Ushauri wa bure ni bora ubadili hiyo Heater na ujipatie Heater za Kisasa yenye Thermostat kwani kukabiliana na hiyo heater unaweza ingia unnecessary cost, Lakini kama utaona ugumu then Jaribu kununua switch socket ya Ampere 15 huwa zina matundu ya duara, Na pia Ubadilishe Plug ya Heater na Plug ya 15A inayoendana na hiyo switch socket, Na pia utafute Inline switch ya Ampere 15 ambayo utaifunga ktk waya wa Heater. Then unakuwa unawasha Swith socket kwanza ndo inafuatia inline switch.
 
mtoa mada usichanganywee na hao mainjinia hapo juu na vimahesabu vingiiiii,, lkn mwisho wa siku magorofa yanaporomoka, fanya kitu kimoja nenda tronic pale moro road, waambie naomba dp switch 15am, tafuta fundi akufungie ahakikishe isiwe loose. hitter yako ni ndogo yani yakawaida hiyo inatosha.
 
Teh teh teh heater ya watt 1500 ukaifungie D.P switch? Kama anataka kuchomoa na kuweka hiyo heater amuite fundi tena? Idea yako nzuri lakini kwa rating ya 1500watt bado top plug ya 13A na 15A itafanya kazi vyema.
 
mtoa mada usichanganywee na hao mainjinia hapo juu na vimahesabu vingiiiii,, lkn mwisho wa siku magorofa yanaporomoka, fanya kitu kimoja nenda tronic pale moro road, waambie naomba dp switch 15am, tafuta fundi akufungie ahakikishe isiwe loose. hitter yako ni ndogo yani yakawaida hiyo inatosha.
unampoteza mwenzako.
 
Mzee kama vp achana na heater tafuta jagi mm na2mia jagi cunguzi socket ila kama upo dom jagi halifai kwan maji ni ya chumvi yanaliua mapema.
 
Back
Top Bottom