cha kuongezea kwa nini hati hiyo ilifichwa mpaka kamati zimemaliza kujadili hizo kanuni mbili ? ndo wazitoe sasa jibu ni moja hawakutaka mapungufu yaliyomo katika mkataba huo yajadiliwe na kamati!!!!!!Naamini kuna na wengine ambao kama ulivyo wewe, hamkumwelewa Tundu Lissu alikuwa anasema nini. Ila kwa tuliomwelewa anachokifanya kinakubalika.
Kupatikana kwa hati ya Muungano siyo kitu kigumu kiasi cha serikali bila aibu kudai iko UN! Kwamba mnataka tueleweje? Ukipangishwa nyumba Mkataba anakaa nao mwenye nyumba au?
Chochote ambacho kilisemwa ni baada ya kigugumizi cha Serikali kuitoa hati hiyo, hata pale ambapo iliombwa na Kamati za bunge maalum la katiba! Ni serikali ya ajabu na iliyojaa upuuzi inayoweza kufanyia mzaha hata swala kama hilo. Vinginevyo ni wazi kuwa nia ya serikali haikuwa njema kwa kuificha hati hiyo.
Hata sasa, pamoja na kutolewa kwa hati hiyo kila mwenye akili timamu anapaswa kujiuliza hati hiyo ilikuwa wapi? Na huko ilikokuwa ilikuwa inafanyiwa nini ndo itolewe leo? Ni kweli Watanzania wanapaswa kuiamini hati hiyo? je! HATI HIYO ILIYOTOLEWA PAMOJA NA KUFICHWA KOTE HUKO NI HATI HALISI NA HALALI?
Nasikitika tu kuwa pamoja na mwamko walio nao Watanzania wengi, bado kuna wanaofikiria kama wewe out there!
Hati ya Muungano inaonesha nchi zilizoungana ni Tanganyika na Zanzibar. Lissu hapo ana point nzuri sana. Jee, Tanganyika iko wapi?
Lissu hawezi ingia mitini. Alichokifanya ni kutafuta njia ya kumtoa nyoka pangoni ili ampige rungu la kichwa. Kumbuka wajumbe wengi wa CCM walikuwa wanazungumzia misingi ya kuanzishwa muungano ilindwe kulingana na makubaliano ya awali ya waasisi wake. Sasa ndio ( kama hati hiyo ni halali) tutakapo ona kuwa muungano huu uliopo sasa ambao serikali ya Zanzibar imeshajitenga kuwa sio misingi ile ya awali kwa hiyo yale aliyosema Warioba ndiyo yanayopaswa kufanywa sasa katika kuunda katiba mpya.
Nakuhakikishia usione Lissu na wenzie wanacheka ukadhani ni machizi, wameshajua wapi pa kuwapiga bao. Maana sidhani kama hayo yaliyofanyika siku za karibuni yako kwenye hati ya makubaliano ya awali. Tatizo la wale wanaofata msimamo wa Chama na kutukana na kuzomea wanaiga style ya kasuku tuu.
Sent from my iPad using JamiiForums
Kwani Nyerere au Karume Ndio walinunua Tanzania? Kwani sahihi zao zina kitu gani cha kufanya Muungano ni halali?
Watanzania wapige kura watakao onekana ni wengi ndo tuamini Muungano vinginevyo sahihi ya nyerere na Karume havitoshi kuhalalisha muungano.
aliyepata aibu ni serikali. Kwa nini haikutoa hiyo hati mapema? Imeombwa mara mia kidogo lakini mara tunaambiwa iko UN, mara mahakama kuu - yaani usanii tu. Maji yamefika shingoni ndo wanaileta. Wao ndo wamepta aibu
Kama ujui kusoma hilo sio tatizo langu.
Jambo la kufanya ni kuwalaumu wazazi wako ambao wameshindwa kukusomesha.
Who knows, huenda hata wazazi wako hawakwenda shule so hawakuona umuhimu wa ikukupeleka shule.
aibu ya kwenu nyinyi wewe mbulumundu! Kama ndio yenyewe mliificha weeee, kwa miaka 50 tena kama chupi ili mje mlazimishwe kuivua na huyo lissu?tundu lissu na genge lake la waongo wamekuwa wakipotosha bungeni kuwa muungano wa tanganyika na zanzibar haupo kisheria kisa hakuna hati ya muungano huo. Jambo ambalo limepingwa vikali na ikulu tena kwa kutoa uthibitisho wa uwepo wa hati hiyo ya muungano.
[COLOR=#ff0000 said:PATIENT ZERO[/COLOR];9251858]Kama ujui kusoma hilo sio tatizo langu.
Jambo la kufanya ni kuwalaumu wazazi wako ambao wameshindwa kukusomesha.
Who knows, huenda hata wazazi wako hawakwenda shule so hawakuona umuhimu wa ikukupeleka shule.
cha kuongezea kwa nini hati hiyo ilifichwa mpaka kamati zimemaliza kujadili hizo kanuni mbili ? ndo wazitoe sasa jibu ni moja hawakutaka mapungufu yaliyomo katika mkataba huo yajadiliwe na kamati!!!!!!