Baada ya upotoshaji mkubwa kufanywa bungeni na watu wasio itakia nchi yetu mema wakiwa wameongozwa na Tundu Lissu. Sasa watu hao wamepata aibu ya mwaka baada ya Ikulu kusambaratisha upotoshaji wao.
Tundu Lissu na genge lake la waongo wamekuwa wakipotosha bungeni kuwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar haupo kisheria kisa hakuna hati ya muungano huo. Jambo ambalo limepingwa vikali na Ikulu tena kwa kutoa uthibitisho wa uwepo wa hati hiyo ya muungano.
Lissu na genge lake la wahuni watafute uongo mwingine, maana huu wa upotoshaji juu ya hati ya muungano hauna tena soko. Tuipe pongezi Ikulu kwa kukata mzizi wa fitina.
Mambo haya yanapaswa kujibiwa na si kutuletea MIPASHO kwenye masuala ya kitaifa!!!
(d) Katika kitabu chake kiitwacho 50 Years of
Independence: A ConcisePolitical History of Tanzania,
kilichochapishwa Januari ya mwaka huu 2014, MzeePius
Msekwa, Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM na
Katibu Mtendaji wake wa kwanzaamesema yafuatayo
kuhusu mambo yaliyofanyika baada ya Makubaliano ya
Muunganokusainiwa:
(i) Tarehe 26 Aprili, 1964, yaani Siku ya Muungano, Rais
Nyerere alitungaPresidential Decree (Amri ya Rais)
iliyoitwa The Transitional ProvisionsDecree, 1964, yaani,
Amri ya Masharti ya Mpito ya mwaka 1964,
iliyochapishwakatika Gazeti la Serikali la siku hiyo. Amri
hiyo iliwabadilisha watuwaliokuwa watumishi wa Serikali
ya Jamhuri ya Tanganyika na kuwafanya watumishiwa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Mahakama Kuu ya
Tanganyika iligeuzwa kuwaMahakama Kuu ya Jamhuri ya
Muungano; na nembo ya taifa ya Jamhuri ya
Tanganyikailigeuzwa kuwa nembo ya taifa ya Jamhuri ya
Muungano.
(ii) Tarehe hiyo hiyo, Rais Nyerere alitunga Amri
nyingine ya Rais iliyoitwaThe Interim Constitution
Decree, 1964, yaani, Amri ya Katiba ya Muda ya
mwaka1964. Amri hii iliitangaza Katiba ya Tanganyika
kuwa ndiyo Katiba ya Muda yaJamhuri ya Muungano.
Kifungu cha 4 cha Amri hii ndicho kilichoipatia
Serikaliya Muungano majukumu kuhusu mambo yote ya
Muungano katika Jamhuri ya Muunganoyote na vile vile
kwa mambo yasiyokuwa ya Muungano kwa upande wa
Tanganyika.
(iii) Tarehe 15 Juni 1964 Mwalimu Nyerere alitunga
Amri nyingine tena iliyoitwaThe Transitional Provisions
(No. 2) Decree, 1964, yaani, Amri ya Masharti yaMpito
(Na. 2) ya mwaka 1964. Amri hii ilielekeza kwamba
mahali popote ambaposheria zilizopo zimetaja jina la
Tanganyika basi jina hilo lifutwe na badalayake jina la
Jamhuri ya Muungano liwekwe. Vile vile, Amri hiyo
ilielekeza,mahali popote ambapo Serikali ya Tanganyika
imetajwa, au kwenye jambo au kituchochote ambacho
kwa namna yoyote kinamilikiwa au kinahusishwa na
Serikalihiyo, basi itachukuliwa kuwa ni Serikali ya
Jamhuri ya Muungano ndiyoiliyotajwa.
(iv) Kwa maneno ya Mzee Msekwa mwenyewe:
Tanganyika was thus decreed out ofexistence. The
cumulative effect of these legislative measures was that
thepolitical entity which was Tanganyika, was decreed
totally out of existence.That is the reason why even the
name of the geographical unit formerly known
asTanganyika, had to be changed to Tanzania Mainland.
Tafsiri ya maneno haya nikwamba uhai wa Tanganyika
ulitolewa kwa njia hiyo ya amri. Athari za jumla zaAmri
hizi ni kwamba eneo la kisiasa ambalo ndio ilikuwa
Tanganyika lilitolewauhai wake moja kwa moja kwa
amri. Hii ndiyo sababu hata jina la eneo lakijiografia
lililojulikana zamani kama Tanganyika ilibidi libadilishwe
na kuwaTanzania Bara.
2. Vitendo vya kuivika Jamhuri ya Tanganyika joho la
Muungano na kuigeuza kuwandio Jamhuri ya Muungano
hakikuwa na uhalali wowote kwa mujibu wa
Makubalianoya Muungano:
(a) Aya ya (v) ya Hati ya Makubaliano ya Muungano
ilitamka wazi kwamba sheriazilizopo za Tanganyika na za
Zanzibar zitaendelea kutiliwa nguvu katika
maeneoyao.... Kwa maana hiyo:
(i) Rais Nyerere hakuwa na mamlaka yoyote kwa mujibu
wa Makubaliano ya Muunganowala chini ya Katiba na
Sheria za Tanganyika ya kugeuza sheria zote za
Jamhuriya Tanganyika kuwa sheria za Jamhuri ya
Muungano hata kwa mambo yasiyokuwa yaMuungano;
(ii) Rais Nyerere hakuwa na mamlaka yoyote kwa
mujibu wa Makubaliano yaMuungano wala kwa mujibu
wa Katiba na Sheria za Tanganyika ya
kuwageuzawatumishi wote wa Jamhuri ya Tanganyika
kuwa watumishi wa Jamhuri ya Muunganohata kwa
mambo yasiyokuwa ya Muungano;
(iii) Rais Nyerere hakuwa na mamlaka yoyote kwa
mujibu wa Makubaliano yaMuungano au kwa mujibu wa
Katiba na Sheria za Tanganyika ya kugeuza
MahakamaKuu ya Tanganyika kuwa Mahakama Kuu ya
Jamhuri ya Muungano;
(iv) Rais Nyerere hakuwa na mamlaka yoyote kwa
mujibu wa Makubaliano yaMuungano au kwa mujibu wa
Katiba na Sheria za Tanganyika ya kugeuza Nembo
yaTaifa ya Jamhuri ya Tanganyika kuwa Nembo ya Taifa
ya Jamhuri ya Muungano.Nembo za Taifa, yaani Bibi na
Bwana inayotumika hadi leo hii ni Nembo yaTaifa ya
Jamhuri ya Tanganyika!
(v) Rais Nyerere hakuwa na mamlaka yoyote kwa
mujibu wa Makubaliano ya Muunganoau kwa mujibu wa
Katiba na Sheria za Tanganyika ya kufuta matumizi ya
jina laTanganyika katika sheria zote za Jamhuri ya
Tanganyika au katika mambo au vituvyote vilivyokuwa
vinamilikiwa ama kuhusishwa na Jamhuri ya Tanganyika
hata kwamambo yasiyokuwa ya Muungano ya
Tanganyika;
(vi) Rais Nyerere hakuwa na mamlaka yoyote kwa
mujibu wa Makubaliano yaMuungano au kwa mujibu wa
Katiba na Sheria za Tanganyika ya kutoa uhai wa nchiya
Tanganyika kwa njia ya Amri ya Rais au kwa njia
nyingine yoyote ya kisheriana kuigeuza kuwa Jamhuri ya
Muungano.