Filipo Lubua
JF-Expert Member
- Nov 18, 2011
- 339
- 578
Wadau,
naombeni muniwie radhi ila leo sina budi kuwadisi waandishi wa habari wa Tanzania. Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa eti Waandishi Wanakutana na Dola Kujadili Usalama
Unakwenda kujadili usalama wako na mtu huyohuyo anayeuhatarisha? Dola hiyo hiyo iwapigao mabomu, iwatekao na kuwamwagia tindikali, iwapigao risasi na kusema iliwadhania ni majambazi, dola hiyohiyo iwacharangayo mapanga, iwatoboayo macho! Dola hiyohiyo?
Tangu lini panya wakakaa kikao cha usalama na paka? Au vipi swala na simba wakakaa kikao kwa ajili ya kujadili usalama? Hilo lawezekana?
Waandishi wa Tanzania hawajaungana! Alimwagiwa tindikali Kubenea na mwenzake Ndimara Tegambwage kucharangwa mapanga, waandishi walikaa kimya na sikuona la maana walilofanya kulaani kuteswa kwao! Likafungiwa gazeti la Mwanahalisi, sijaona la maana walilofanya kuilaani serikali! Akauawa Mwangosi kwa bomu, sijaona la maana walilolifanya kuilaani serikali! Alipigwa Risasi Mhariri wa Business Times, hakuna la maana walilolifanya! Sasa eti Kibanda, Mwenyekiti wao, ametobolewa jicho na kung'olewa meno eti wanakaa na dola kujadili amani!!! Amani ipi?
Hawa ndio wasaliti wa Absalomu Kibanda! Ndio wasaliti wa Kubenea; Hawa ndio wasaliti wa Mwangosi; Hawa ndio wasaliti wa taaluma nzima ya uandishi wa habari.... Badala ya kuchukua hatua madhubuti, wanabaki tu kuandikaandika vimakala vya kuilaani serikali!! Makala! Pachimbeni pachimbike! Hivyo ndivyo amani yenu itakavyopatikana na wala si kukaa meza moja na dola ambayo ndo yawatendea vitendo viovu!! Nasema pachimbeni; pachimbeni pachimbike!!
naombeni muniwie radhi ila leo sina budi kuwadisi waandishi wa habari wa Tanzania. Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa eti Waandishi Wanakutana na Dola Kujadili Usalama
Unakwenda kujadili usalama wako na mtu huyohuyo anayeuhatarisha? Dola hiyo hiyo iwapigao mabomu, iwatekao na kuwamwagia tindikali, iwapigao risasi na kusema iliwadhania ni majambazi, dola hiyohiyo iwacharangayo mapanga, iwatoboayo macho! Dola hiyohiyo?
Tangu lini panya wakakaa kikao cha usalama na paka? Au vipi swala na simba wakakaa kikao kwa ajili ya kujadili usalama? Hilo lawezekana?
Waandishi wa Tanzania hawajaungana! Alimwagiwa tindikali Kubenea na mwenzake Ndimara Tegambwage kucharangwa mapanga, waandishi walikaa kimya na sikuona la maana walilofanya kulaani kuteswa kwao! Likafungiwa gazeti la Mwanahalisi, sijaona la maana walilofanya kuilaani serikali! Akauawa Mwangosi kwa bomu, sijaona la maana walilolifanya kuilaani serikali! Alipigwa Risasi Mhariri wa Business Times, hakuna la maana walilolifanya! Sasa eti Kibanda, Mwenyekiti wao, ametobolewa jicho na kung'olewa meno eti wanakaa na dola kujadili amani!!! Amani ipi?
Hawa ndio wasaliti wa Absalomu Kibanda! Ndio wasaliti wa Kubenea; Hawa ndio wasaliti wa Mwangosi; Hawa ndio wasaliti wa taaluma nzima ya uandishi wa habari.... Badala ya kuchukua hatua madhubuti, wanabaki tu kuandikaandika vimakala vya kuilaani serikali!! Makala! Pachimbeni pachimbike! Hivyo ndivyo amani yenu itakavyopatikana na wala si kukaa meza moja na dola ambayo ndo yawatendea vitendo viovu!! Nasema pachimbeni; pachimbeni pachimbike!!