Aibu kwa Waandishi wa Habari na Udhalilishaji wa Taaluma yao

Filipo Lubua

JF-Expert Member
Nov 18, 2011
339
578
Wadau,

naombeni muniwie radhi ila leo sina budi kuwadisi waandishi wa habari wa Tanzania. Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa eti Waandishi Wanakutana na Dola Kujadili Usalama

Unakwenda kujadili usalama wako na mtu huyohuyo anayeuhatarisha? Dola hiyo hiyo iwapigao mabomu, iwatekao na kuwamwagia tindikali, iwapigao risasi na kusema iliwadhania ni majambazi, dola hiyohiyo iwacharangayo mapanga, iwatoboayo macho! Dola hiyohiyo?

Tangu lini panya wakakaa kikao cha usalama na paka? Au vipi swala na simba wakakaa kikao kwa ajili ya kujadili usalama? Hilo lawezekana?

Waandishi wa Tanzania hawajaungana! Alimwagiwa tindikali Kubenea na mwenzake Ndimara Tegambwage kucharangwa mapanga, waandishi walikaa kimya na sikuona la maana walilofanya kulaani kuteswa kwao! Likafungiwa gazeti la Mwanahalisi, sijaona la maana walilofanya kuilaani serikali! Akauawa Mwangosi kwa bomu, sijaona la maana walilolifanya kuilaani serikali! Alipigwa Risasi Mhariri wa Business Times, hakuna la maana walilolifanya! Sasa eti Kibanda, Mwenyekiti wao, ametobolewa jicho na kung'olewa meno eti wanakaa na dola kujadili amani!!! Amani ipi?

Hawa ndio wasaliti wa Absalomu Kibanda! Ndio wasaliti wa Kubenea; Hawa ndio wasaliti wa Mwangosi; Hawa ndio wasaliti wa taaluma nzima ya uandishi wa habari.... Badala ya kuchukua hatua madhubuti, wanabaki tu kuandikaandika vimakala vya kuilaani serikali!! Makala! Pachimbeni pachimbike! Hivyo ndivyo amani yenu itakavyopatikana na wala si kukaa meza moja na dola ambayo ndo yawatendea vitendo viovu!! Nasema pachimbeni; pachimbeni pachimbike!!
 
Wadau,

naombeni muniwie radhi ila leo sina budi kuwadisi waandishi wa habari wa Tanzania. Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa eti Waandishi Wanakutana na Dola Kujadili Usalama wanakutana na dola kujadili usalama!

Unakwenda kujadili usalama wako na mtu huyohuyo anayeuhatarisha? Dola hiyo hiyo iwapigao mabomu, iwatekao na kuwamwagia tindikali, iwapigao risasi na kusema iliwadhania ni majambazi, dola hiyohiyo iwacharangayo mapanga, iwatoboayo macho! Dola hiyohiyo?

Tangu lini panya wakakaa kikao cha usalama na paka? Au vipi swala na simba wakakaa kikao kwa ajili ya kujadili usalama? Hilo lawezekana?

Waandishi wa Tanzania hawajaungana! Alimwagiwa tindikali Kubenea na mwenzake Ndimara Tegambwage kucharangwa mapanga, waandishi walikaa kimya na sikuona la maana walilofanya kulaani kuteswa kwao! Likafungiwa gazeti la Mwanahalisi, sijaona la maana walilofanya kuilaani serikali! Akauawa Mwangosi kwa bomu, sijaona la maana walilolifanya kuilaani serikali! Alipigwa Risasi Mhariri wa Business Times, hakuna la maana walilolifanya! Sasa eti Kibanda, Mwenyekiti wao, ametobolewa jicho na kung'olewa meno eti wanakaa na dola kujadili amani!!! Amani ipi?

Badala ya kuchukua hatua madhubuti, mnabaki tu kuandikaandika vimakala vya kuilaani serikali!! Makala! Pachimbeni pachimbike! Hivyo ndivyo amani yenu itakavyopatikana na wala si kukaa meza moja na dola ambayo ndo yawatendea vitendo viovu!! Nasema pachimbeni; pachimbeni pachimbike!!

Labda wanaenda kuomba msamaha! (They go for reconciliation)
 
Wadau,

naombeni muniwie radhi ila leo sina budi kuwadisi waandishi wa habari wa Tanzania. Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa eti Waandishi Wanakutana na Dola Kujadili Usalama wanakutana na dola kujadili usalama!

Unakwenda kujadili usalama wako na mtu huyohuyo anayeuhatarisha? Dola hiyo hiyo iwapigao mabomu, iwatekao na kuwamwagia tindikali, iwapigao risasi na kusema iliwadhania ni majambazi, dola hiyohiyo iwacharangayo mapanga, iwatoboayo macho! Dola hiyohiyo?

Tangu lini panya wakakaa kikao cha usalama na paka? Au vipi swala na simba wakakaa kikao kwa ajili ya kujadili usalama? Hilo lawezekana?

Waandishi wa Tanzania hawajaungana! Alimwagiwa tindikali Kubenea na mwenzake Ndimara Tegambwage kucharangwa mapanga, waandishi walikaa kimya na sikuona la maana walilofanya kulaani kuteswa kwao! Likafungiwa gazeti la Mwanahalisi, sijaona la maana walilofanya kuilaani serikali! Akauawa Mwangosi kwa bomu, sijaona la maana walilolifanya kuilaani serikali! Alipigwa Risasi Mhariri wa Business Times, hakuna la maana walilolifanya! Sasa eti Kibanda, Mwenyekiti wao, ametobolewa jicho na kung'olewa meno eti wanakaa na dola kujadili amani!!! Amani ipi?

Badala ya kuchukua hatua madhubuti, mnabaki tu kuandikaandika vimakala vya kuilaani serikali!! Makala! Pachimbeni pachimbike! Hivyo ndivyo amani yenu itakavyopatikana na wala si kukaa meza moja na dola ambayo ndo yawatendea vitendo viovu!! Nasema pachimbeni; pachimbeni pachimbike!!

Sioni ubaya Mkuu. Panya kukaa na paka ni moja ya mikakati ya kumshinda paka. Kwanza utaiona taswira ya huyo paka yukoje? ana mapungufu gani? Ni mzee au kijana? ni mnafiki au ni mkweli? Kumbuka mbinu za mwanafalsafa Socrates za kumjua mtu kwa kumuuliza MASWALI-DADISI.
 
Sioni ubaya Mkuu. Panya kukaa na paka ni moja ya mikakati ya kumshinda paka. Kwanza utaiona taswira ya huyo paka yukoje? ana mapungufu gani? Ni mzee au kijana? ni mnafiki au ni mkweli? Kumbuka mbinu za mwanafalsafa Socrates za kumjua mtu kwa kumuuliza MASWALI-DADISI.

Yawezekana, ila mbona matukio yamekuwa mengi sana? Tangu Kubenea hadi leo, si haba nduguye!
 
For the record ni kitu kizuri waandishi wamefanya.....

Mwisho wa siku bado hii ni nchi yenye mifumo rasmi japo dhaifu lakini ndio nchi yetu tena na sidhani kama walikuwa na kwingine kwa kwenda.

Ila kwa mambo uliyoyataja kweli waandishi wa habari wetu ni wanafiki sana na wachumia tumbo hadi kusalitiana!!
 
-Waandishi hawa wa Tanzania sijui!!tatizo kila mmoja anajiona yuko salama,mpaka pale linapomkuta
yeye ndipo wanajua kumbe hatuko salama.
-Waandishi hawa ambao wanaandamana halafu jukwaa la wahariri wanamwalika Nchimbi ndiye aje
kupokea maandamo ya kupinga kuuawa mwenzao na askari walio chini ya huyo Nchimbi!!
-Waandishi wa hawa wa Tanzania ambao kwa sasa ukipiga simu kwenye chombo cha habari kuwa
kuna tukio au mikutano ya jamii wanataka waahidiwe kila mmoja si chini ya 50,000 ndipo waje na
watoe hiyo habari!!
-Waandishi ambao walimwambia Kubenea alijitakia, kwa kutoa habari za uoenevu juu ya raia!!!
-Waandishi wa Tanzania ukombozi wao baaado sana kwani hawajajitambua'

 
Wajinga njaa zimewajaa tumboni. Hata Jerry Mulo nasikia walimlipua wenyewe kwa Wenyewe hata hii ya kibanda wako kimya.
 
Nimesoma mapaka naisi moyo unaumwa kwani vitu viumiza sanaaaaaaaaaaa ( afande mshuti )
 
Hawajui kuwa Kesi ya Jerry Muro ilibambikwa na polisi?TIDO MHANDO jee?siku zote dola na media huwa havikai chungu kimoja,vinginevyo uwe mtumwa
 
yataka moyo kuwakubali wanahabari wa Bongo!!!
napita tuu mkuu.
:crying:
 
Kaangalieni youtube ya lwakatare ndo mjue mchawi wa waandishi wa habari ni nani
 
Watanzania kwa ujumla wetu tuna tatizo la "kiasili" ambalo ni common kwa watanzania wote!Sisi watanzania kwa ujumla wetu pamoja na hao waandishi wa habari ni watu ambao hatuna asili ya kuwa na sauti na nguvu ya pamoja kama umma wa watanzania katika kupinga na kupambana na udhalimu wa serikali yetu na kibaya zaidi matukio yanakuja na kupita na tunaona sawa tu!Huu udhaifu ndio serikali wanaoutumia kututawala kwa mtindo huu wa "kimafya".

Tusipobadilika, hata nchi itauzwa!
 
Wadau,

naombeni muniwie radhi ila leo sina budi kuwadisi waandishi wa habari wa Tanzania. Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa eti Waandishi Wanakutana na Dola Kujadili Usalama wanakutana na dola kujadili usalama!

Unakwenda kujadili usalama wako na mtu huyohuyo anayeuhatarisha? Dola hiyo hiyo iwapigao mabomu, iwatekao na kuwamwagia tindikali, iwapigao risasi na kusema iliwadhania ni majambazi, dola hiyohiyo iwacharangayo mapanga, iwatoboayo macho! Dola hiyohiyo?

Tangu lini panya wakakaa kikao cha usalama na paka? Au vipi swala na simba wakakaa kikao kwa ajili ya kujadili usalama? Hilo lawezekana?

Waandishi wa Tanzania hawajaungana! Alimwagiwa tindikali Kubenea na mwenzake Ndimara Tegambwage kucharangwa mapanga, waandishi walikaa kimya na sikuona la maana walilofanya kulaani kuteswa kwao! Likafungiwa gazeti la Mwanahalisi, sijaona la maana walilofanya kuilaani serikali! Akauawa Mwangosi kwa bomu, sijaona la maana walilolifanya kuilaani serikali! Alipigwa Risasi Mhariri wa Business Times, hakuna la maana walilolifanya! Sasa eti Kibanda, Mwenyekiti wao, ametobolewa jicho na kung'olewa meno eti wanakaa na dola kujadili amani!!! Amani ipi?

Hawa ndio wasaliti wa Absalomu Kibanda! Ndio wasaliti wa Kubenea; Hawa ndio wasaliti wa Mwangosi; Hawa ndio wasaliti wa taaluma nzima ya uandishi wa habari.... Badala ya kuchukua hatua madhubuti, wanabaki tu kuandikaandika vimakala vya kuilaani serikali!! Makala! Pachimbeni pachimbike! Hivyo ndivyo amani yenu itakavyopatikana na wala si kukaa meza moja na dola ambayo ndo yawatendea vitendo viovu!! Nasema pachimbeni; pachimbeni pachimbike!!

Mkuu Filipo Lubua ulichokiandika ndo ukweli kabisa, nashindwa kuelewa kwa nini hawa waandishi wa habari hawajitambui, yumkini hili limetokana na shule za kuunga -unga bila kufuata mitaala inayo eleweka, hata kama ndivyo bado haitoshi kwanini wasijifunze kutokana na makosa? Kwa nini wasiangalie wenzao wa nchi zingine wanachukua hatua gani yanapotokea matatizo kama haya yanayowakuta? Kwa mfano leo nimesikiliza taarifa ya habari, waandishi na wamiliki wa vyombo vya habari vya binafsi nchini Mali wamegoma kutangaza habari yoyote ile kwa sababu kiongozi wao amekamatwa na vyombo vya dola.
 
Back
Top Bottom