Misri, Algeria, Tunisia, Morocco, Sudan, Libya, ziko bara gani? Raia wake, wawe manjano, kijivu au buluu, ni wa bara gani? Raia wa bara la Afrika wanaitwaje kwa neno moja? Au unataka kutuambia wao ni makaburu waliowavamia wenyeji wa nchi hizo kama ilivyofanyika Afrika ya Kusini? Kama ni hivyo, hao wenyeji wa nchi zote hizo ndani ya Afrika wamekimbilia wapi na lini?Ina maana Wasaudia, Walebanon, Wayemen, Waimarati, Wasyria, Waqatar sio Waasia kwa sababu ni Waarabu? Kama ni hivyo Waarabu kwao wapi hasa? Hivi Mbilikimo si Waafrika kwa sababu ni Wakongo? Au ulikusudia Wamisri si Waafrika halisi kwa sababu ni Waarabu? Kwani mtu hawezi kuwa raia wa nchi au bara moja lakini mwenye asili ya nchi au bara jengine? Hao unaosema si Waafrika, asili yao wapi?Kama weusi ndio Uafrika, ina maana Mkapa ni Mwafrika zaidi kuliko Jakaya?