Agizo la Magufuli laibua utata

Agizo la Magufuli laibua utata

Kiongozi, usiwe kama huishi Tanzania au huifahamu nchi yetu; unataka kusema amri zote zinazotolewa huko majeshini huwa ni za halali tu? Kwenye nchi corrupted kama hii kinachoangaliwa ni cheo kwanza, uhalali wa amri tupa kule.
Mkuu BAK with due respect naona chanzo chako cha habari hakisemi ukweli wa jambo hili. Masuala yote ya kijeshi hata utoaji amri yanafuata utaratibu. Amri zitatolewa vipi, na nani na kwa namna gani vyote viko kwenye utaratibu huo na Amri zilizotajwa kwenye utaratibu ni zile zinaoitwa "AMRI HALALI" na siyo kila amri, hivyo ni upotoshaji kwamba eti afande anaweza akamwambia mhasibu ambaye ni mwanajeshi kwamba "Lipa malipo haya na akalipa" hiyo si kweli hata kidogo. Pia ni vizuri ukafahamu kuwa katika Jeshi kuna utaratibu mzuri tu uliyowekwa kwa mwanajeshi kuhoji amri ambayo anafikiri si halali.
 
Swala la kujiuliza mleta mada, ni kwanini jpm kaamua iwe hivi!!!!!???.

Sio kuleta hitimisho moja kwa moja.yanaoyoendelea huko wakiwepo hao watumishi raia wasiopokea amri na maafande ni ya kutapisha.

Waache waende kwanza.
 
Umenifurahisha mkuu, hivi wewe ni Mungu kujua roho ya unayemuweka kama kiongozi? Kwa vile hatujui ya mbele katika maisha kinga si 100%. Kinga zipo za Vetting etc ila kama nilivyosema huwezi kujua kwa asilimia zote kama unayemwamini anaaminika. Hivyo TIBA ya mapema ni muhimu nayo ni kutumbuliwa kabla ya kumaliza kipindi chake. Heri nusu shari kuliko.... (malizia)
Unajua sehemu moja ndiyo una-miss!!! Hilo suala la TIBA lipo pale pale bali kujali ikiwa Mwajiriwa husika ni askari au raia! Hata akiwa raia, huyu nae Auditor ambae unaamini ni daktari atakutana nae! Hata akiwa askari, nae atakutana na auditor!

Kinyume chake, Mwajiriwa Raia hawajibiki kwa amri za kijeshi kv yeye ni mwajiriwa wa mtu mwingine kabisa! Kwahiyo hapa kabla ya kufikiria tiba, tayari umeweka kinga... kinga isipofua dafu ndipo inakutana na tiba! Kinyume chake, Mwajiriwa Askari anawajibika kwenye military chain of command! Unless awe jasiri kweli kweli lakini huyu hana kinga!!

So, it's up to you ulale kwenye neti lakini hata mbu wakikuotea nje ya noti unafahamu kwamba kuna mseto au usilale kwenye neti kv tu unafahamu kuna mseto!!
 
Majeshi Yanaundwa Kwa Sheria, Au Niseme Miswada ya Sheria huletwa bungeni kuunda au kuufanyia mabadiliku mfumo au Taasisi iliyoundwa Kisheria. Nafikiri hata Sherehe za Uhuru zipo Kisheria, Lakini Zikafungiwa Tucheki ama vipi! I wish Watanzania Wangeshituka Kuwa Kwake uhuru uliopiganiwa Miongo Mingi kwa Mateso mengi, Machozi na Damu, Kwake haikuwa Kitu cha maana sana, Ndio Maana sio Jambo Kubwa kwake Kuminya Uhuru wa Demokrasia, Wa habari na Mawazo! Huo Ndio Ukweli
 
Naona umepinda kweli! Zamani mtu akikuuliza so wati unamjibu so dasti. Pole sana haya ninayoyaeleza yanakuzidi kimo naomba niishie hapa
Huna lolote wewe! Jibu, nimeshakwiba 500 Million pale na wewe Auditor unakuja na kugundua kuna irregularities... so what?! Jibu swali hilo! Taasisi husika zitanipeleka mahakamani? Let's go dude... wote wanaoiba wanafahamu kwamba sooner or later litabumbulika tu but they don't give a shit about hao ma-auditors! So, unless kama unataka kuniambia jambo jipya lakini kwamba eti kuna auditors ni kichekesho!!!
 
Huo ni uongo uliopitiliza...muhasibu yeyote akishajua dili inaela atatoa tu hayo malipo...tunawaona huku kwenye maofisi..suala hapa siyo ujeshi au uraia ndugu yangu...ni uwezo wa mtu kuzingatia ethics za kaz yake...
Unless kama hujanisoma kwenye posts zingine! Nimeshasema kabla kwamba hata huku uraiani wapo wafanyakazi kadhaa wanaotii amri zisizo halali! Lakini hapa kuna mambo mawili! Mosi, kuna kutii kwa sababu unafahamu hapa kuna kula! Hiyo ndiyo hoja yako na wala sio hoja inayozungumzwa hapa! Pili, kuna kutii kwa sababu unamhofia bosi wako... kv ndie mwajiri wako!! Sasa ikiwa utii wako unatokana na kumuogopa mwajiri wako; Raia aliye jeshini anakuwa insulated kv mwajiri wake sio Jeshi au wizara husika! Na ndio maana nikatoa mfano wa District Council Auditors... ili nao wawe insulated, Mwajiri wao hakuwa Halmashauri bali Hazina unless wawe wamebadilisha miaka ya karibuni!
 
tunaomba ata mahospitali madaktari ndio wawe wahasibu,mabenki wahasibu wawe walinzi polisi watolewe ili kusiwe na mwingiliano kabisa!! Kilamtu asimamie chake fulu
 
Pia napata wasiwasi kuwa hata Baraza la Mawaziri halishirikishwi kwenye haya matamko na maamuzi.

Mkuu baraza la mawaziri kwa sasa halina kazi lipo tu kwa sababu katiba inataka hivyo lakini kutekeleza wajibu wake ikiwemo kumshauri mkuu wa nchi hiyo hakuna tena maana hashauriki. Kwa mfano ujenzi wa uwanja wa ndege wa chato unafikiri baraza la mawaziri lilishirikishwa kufanya maamuzi? Na mkandarasi tayari yuko site hivi sasa!
 
Hili lilishajadiliwa kwa kina sana umuhimu wa RAIA ndani ya majeshi na kumbuka wengine sio tu RAIA kisa amevaa kiraia ila wengine ni RAIA wa kijeshi na ngumu kumtambua kwa jinsi walivyopikwa na kuiva ktk mafunzo.

Athari za kuwaondoa raia jeshini zitakuja kuonekana mbele ya safari

Ushauri,tuangalia upya namna ya kutekeleza agizo la Mh Rais ili huo mpango mpya usilete madhara.
Baada ya miaka mitano au kumi, serikali itahitajika kufanyiwa ukarabati mkubwa ili iweze kurudi katika hali ya kawaida!
 
Hii ni cheap politics. Kwa mtu asiyejua utawala atakubaliana Na hoja hizi mufilisi. JPM yupo right ni shida sana kuongoza mtu asiyewajibika kwako. Pili hata Account Officer katika taasisi yeyote anaweza kuagiza hayo malipo yakalipwa ila kuna auditor. Auditor akija ndiye Kiboko ya accounting officer hata awe IGP. Refer lugumi case
kwa hyo unataka wawe wanaiba na kufanya ufisadi kwanza ndo auditor aje? du kweli mufilisi


Wewe mleta mada ni MWONGO. Ni mmoja ya waathilika wa maamuzi hiyo. Polisi/JWTZ wana wataalam wa kada zote. Wacha waendeshe mambo yao kadiri ya ethics zao. Hoja ya matumizi mabaya ya amri haina mashiko hata kidogo. Naamini kabisa kwa agizo la raisi la kuwaondoa raia kwenye vyombo vya usalama, fedha zitasimamiwa kwa nidhamu kubwa zaidi kuliko kuweka raia ambao hufanya ufisadi mkubwa, na hivyo kuchafua sifa ya majeshi yetu. Utaratibu wa kuweka raia kusimamia fedha kwenye vyombo vya usalama haufai, na hakuna hoja ya msingi kufanya hivyo. Raia wote watoke. Naunga mkono agizo la RAISI JPM. Wafanyakazi raia waliowengi ni mafisadi.Waende wakafanye ufisadi uraiani.
Note: Mimi ni raia wa kawaida,siyo mwanajeshi. Napenda mambo yote ya jeshi yaendeshwe na wanajeshi wenyewe, ili kulinda hadhi ya jeshi. Hawa raia tubaki nao mitaani.

wewe mwanajeshi ana mambo meng sana ya kufanya ikiwemo kupambana awe anahudhuria kozi za kijesh ili apande cheo! kumuweka kwenye positions za kiraia hzo zitawaathiri wengi sana!
 
Nadhani kuna sababu kubwa kwa nini waasisi wetu walitaka raia washike nafasi nyeti. Imagine mwanajeshi daktari. Rais azingatie.
 
Actually hii ina maana kubwa sana kiulinzi na usalama, hasa kunakuwepo na siri ambazo zinaweza kuvuja kama raia ni wafanya kazi katika idara za ulinzi...Wafanya kazi ktk idara za ulinzi ni jambo jema kwa nchi zenye utawala bora na demokrasia lakn kwa Tz ambayo inaelekea gizani hao raia wanaofanya kazi watakuwa kauzibe kwa maamuzi...tupige kelele kukemea hili kwa sababu tukinyamaza viongozi waandamizi wa serikali wanaimba wimbo mmoja hata kama wanajua athari za mambo haya wanaamua kunyamaza ili kulinda vitumbua vyao...soon itakula kwao
 
kwa hyo unataka wawe wanaiba na kufanya ufisadi kwanza ndo auditor aje? du kweli mufilisi




wewe mwanajeshi ana mambo meng sana ya kufanya ikiwemo kupambana awe anahudhuria kozi za kijesh ili apande cheo! kumuweka kwenye positions za kiraia hzo zitawaathiri wengi sana!
Je, position za kiraia ni uhasibu tu? Mbona kuna madaktari, madvocate, marubani n.k. katika jeshi la Polisi? Fanya utafiti ndipo ujenge hoja.
 
“Mhasibu askari anapokaidi maagizo au amri anaadhibiwa kijeshi, lakini kwa raia hiyo haiwezekani,” kimesema
Ni uongo mtupu Eti hawezi kuoji uongo mtupu.. Ata awa Raia walikua wakiambiwa lipa na boss wao labda RPC au IGP hakuna anaebisha.. Mnatoa sababu za kijinga sana
 
Actually hii ina maana kubwa sana kiulinzi na usalama, hasa kunakuwepo na siri ambazo zinaweza kuvuja kama raia ni wafanya kazi katika idara za ulinzi...Wafanya kazi ktk idara za ulinzi ni jambo jema kwa nchi zenye utawala bora na demokrasia lakn kwa Tz ambayo inaelekea gizani hao raia wanaofanya kazi watakuwa kauzibe kwa maamuzi...tupige kelele kukemea hili kwa sababu tukinyamaza viongozi waandamizi wa serikali wanaimba wimbo mmoja hata kama wanajua athari za mambo haya wanaamua kunyamaza ili kulinda vitumbua vyao...soon itakula kwao
mwalimu alikuwaga analeta vijana wake pros kwenye hzo idara wakawa wanamsaidia sana kwenye kupata habari!

sasa wanaondolewa tusubiri vituko
 
Nimesoma koote ili nimeelewa sana hapo kwenye maandishi ya rangi n yekundu, naogopa kuambiwa nimedhalilisha jeshi
 
Huu msamiati wa "kijeshi" kwa polisi sijui maana yake nini? Halafu waandishi ni makanjanja sana! Habari inahusu polisi waovwanasema majeshi. Hivi wanajua wanachokiandika kweli?
 
Back
Top Bottom