Agha Khan kufanya upasuaji wa kurekebisha maumbile bure kwa wanawake 25

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,745
218,335
Lakini kwanini mambo haya yamekuja ghafla hivi?

Taarifa kamili hii hapa.

=====

Hospitali ya Aga Khan kwa kushirikiana na Shirika la Reconstructing Women International (RWI) na Hospitali ya Taifa Muhimbili, inatarajia kufanya upasuaji kurekebisha maumbile kwa wanawake na wasichana 25 kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Upasuaji huo utakuwa bure na unatarajia kuanza kesho Jumanne Novemba 28 hadi Desemba 2, 2023 ukiwa na lengo la kurejesha uwezo wa kutembea kwa watu ambao wanamatatizo yaliyotokana na majeraha makubwa ya moto, ajali za barabarani kasoro za kimwili na wahanga wa ukatili wa kijinsia.

Upasuaji utasimamiwa na timu ya madaktari wa kimataifa wa upasuaji wa kurekebisha maumbile kutoka Marekani, Canada, na Ulaya wakishirikiana na madaktari wa Hospitali za Aga Khan Dar es Salaam, Muhimbili, Bugando, na Mnazi Mmoja ya Zanzibar.

Daktari Mwandamizi wa Upasuaji wa Aga Khan, Dk Athar Ali amesema programu hiyo ambayo kwa mwaka huu ni ya nane tangu kuanza kwake inalenga kurejesha utendaji wa kimwili ili kuwezesha na kuboresha maisha ya wanawake na wasichana wa Tanzania.

Screenshot 2023-11-27 144141.png
 
shape muhimu huwezi ukawa kama moja

shape⌛ is key
Nani kasema ?
Yaani maoni yako na kile ww unapenda ndo iwe key Kwa Kila mtu ? Mdogo angu vipi?🤣
Usisahau Kila mwanaume ana test yake....laa sivyo
hao flat ,wasio na shep kabisa wasingekua wanawenza ,na kuolewa kabisa.
Tena ndo Wana ongoza Kwa kua na mahusiano yanayoelweka kuliko hao wenye matako.
Wanaume tunawajua ,wengine wenu hamuoi hao wenye matako wala kuwekeza,mnajifurahisha nao Kwa muda tu ila mnakuja kuwekeza kwenye wadada wa kawaida kabisaa 🤣
 
Lakini kwanini mambo haya yamekuja ghafla hivi?

Taarifa kamili hii hapa.

=====

Hospitali ya Aga Khan kwa kushirikiana na Shirika la Reconstructing Women International (RWI) na Hospitali ya Taifa Muhimbili, inatarajia kufanya upasuaji kurekebisha maumbile kwa wanawake na wasichana 25 kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Upasuaji huo utakuwa bure na unatarajia kuanza kesho Jumanne Novemba 28 hadi Desemba 2, 2023 ukiwa na lengo la kurejesha uwezo wa kutembea kwa watu ambao wanamatatizo yaliyotokana na majeraha makubwa ya moto, ajali za barabarani kasoro za kimwili na wahanga wa ukatili wa kijinsia.

Upasuaji utasimamiwa na timu ya madaktari wa kimataifa wa upasuaji wa kurekebisha maumbile kutoka Marekani, Canada, na Ulaya wakishirikiana na madaktari wa Hospitali za Aga Khan Dar es Salaam, Muhimbili, Bugando, na Mnazi Mmoja ya Zanzibar.

Daktari Mwandamizi wa Upasuaji wa Aga Khan, Dk Athar Ali amesema programu hiyo ambayo kwa mwaka huu ni ya nane tangu kuanza kwake inalenga kurejesha utendaji wa kimwili ili kuwezesha na kuboresha maisha ya wanawake na wasichana wa Tanzania.

Mleta mada kuna namna umepotosha katika hili.

Usahihi.
Hizo sio operesheni za urembo au matamanio (cosmetic surgeries) bali ni operesheni tiba. Lengo ni kurejesha kile cha kawaida katika maumbile kilichoharibika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuungua kwa moto na ajali. Lengo ni kurudisha utu wa muonekano wa mwanamke na uwezo wa viungo vyake kufanya kazi.

Kwanini ni bure?
1. Wahanga wakubwa wa hayo matatizo ni watu wa kawaida wenye vipato vidogo na maskini.

2. Ni operesheni za mafunzo ili kujenga uwezo (kwa wengi wa madaktari wa kitanzania) na uzoefu (kwa madaktari kutoka nje).

3. Kuna taasisi imedhamini matibabu yao.
 
Mleta mada kuna namna umepotosha katika hili.

Usahihi.
Hizo sio operesheni za urembo au matamanio (cosmetic surgeries) bali ni operesheni tiba. Lengo ni kurejesha kile cha kawaida katika maumbile kilichoharibika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuungua kwa moto na ajali. Lengo ni kurudisha utu wa muonekano wa mwanamke na uwezo wa viungo vyake kufanya kazi.

Kwanini ni bure?
1. Wahanga wakubwa wa hayo matatizo ni watu wa kawaida wenye vipato vidogo na maskini.

2. Ni operesheni za mafunzo ili kujenga uwezo (kwa wengi wa madaktari wa kitanzania) na uzoefu (kwa madaktari kutoka nje).

3. Kuna taasisi imedhamini matibabu yao.
Asante kwa masahihisho , swali dogo la nyongeza , hivi hakuna wanaume walioungua moto na wao warejeshwe kwenye hali ya kawaida ?
 
Back
Top Bottom