Kwanza napenda kumpongeza sana waziri wa mambo ya nje bw. Bernad Membe. Hajawahi kuwa na kashfa nzito kama hizi zinazopelekea mheshimiwa rais kupangua tena baraza la mawaziri. Kwa upande wake kiukweli amejitahidi sana na ahsante kwa hilo.
Membe anapoanza kupotea ni pale anapoutafuta urais 2015 kwa nguvu zote hata kwa kutumia pesa za wizara yake kwa usiri mkubwa. Hivi sasa ameanzisha kampeni kubwa ya kuwateka vijana hasa wale wenye UWEZO WA USHAWISHI KWA WENZAO ambao wanapatikana vyuo vikuu. Anataka kutumia nafasi ya kutengeneza makongamano katika vyuo ili kuanza mapema kujitengenezea jina zuri ifikapo 2015.
Habari nyeti zinasema kuwa bwana Membe akishirikiana na viongozi wa CCM katika vyuo vikuu, anafanya ajenda ya siri kuwarubuni viongozi wa serikali za wanafunzi ( marais wa vyuo) kwa kuwapa pesa ili waandae makongamano yatakayowaunganisha wanafunzi ili apate mwanya wa kutoa hotuba zake za kujiweka safi zaidi.
Hivi karibuni anaandaa kongamano kubwa kwa kuwatumia wanaCCM vijana wa vyuo vikuu Morogoro (Mzumbe, SUA,St. Jordan, Muslim na Ardhi). Anatumia mwanya huo akijifanya anazungumzia mambo ya ajira na uchumi, maana ameshajinadi sana kuwa yeye ni bingwa sana wa uchumi. Pia amejipanga kuwatumia watu wengine mashuhuri nchini km wafanyabiashara wakubwa, wanamichezo, wanaharakati nk ili kuambatana nao katika hayo makongamano yasiyo na tija kwa vijana. Amepanga bajeti kubwa mno kuweza kuwagharimia usafiri wa bure kutoka vyuoni mwao mpaka pale atakapotaka kuwakusanya hao maelfu ya wasomi wasio na hatia ambao wataingizwa katika wimbi la siasa bila wao wenyewe kujijua. Kwa sasa kongamano kubwa la kuwakutanisha wanavyuo wa Morogoro amepanga kulifanya chuo kikuu Mzumbe katika ukumbi wa NAH (New Assembly Hall), huku akiambatana na mfanyabiashara mkubwa ili kusingizia kuwa ndiye aliyetoa wazo na mapesa kwa ajili ya makongamano hayo.
Hatukatai mawaziri au wanasiasa kuhutubia katika vyuo vikuu kwani nao kimsingi ni wananchi tena wenye taaluma zao. Lakini kwa nini kuharibu upeo wa kufikiri wa vijana kwa kuwaingiza kwenye siasa?.kwa nini kuwatumia viongozi wa serikali za wanafunzi kueneza itikadi za mtu binafsi ama chama? je, vyuo vikuu vikiongozwa kwa kuangalia itikadi za chama fulani cha siasa, nchi hii itazaa wasomi wa namna gani? tatizo la RUSHWA je, litakwisha kweli ikiwa hawa vijana waddogo viongozi wa vyuo wanafundishwa kuwa MAFISADI? tatizo la elimu Tanzania litakwisha kweli ikiwa siasa ndiyo inayotawala katika taasisi za elimu? kwa hapo Membe amekosea na wanaharakati pamoja na wanahabari wanatakiwa kulipigania kwa nguvu zote swala hilo nyeti sana.
Vijana ni "thinking tank of the nation". Sasa ikiwa akili zao zitakua "corrupted" na porojo za kisiasa tokea awali katika hatua za mwanzo kabisa za ukombozi wa fikra, je hii si balaa kwa taifa? MBAYA ZAIDI ni pale wanafunzi wa vyuo wanapopoteza muda wao wa kujisomea na kuanza kujadli mambo ya siasa. Ndiyo maana wanavyuo wetu watazidi kuwa maMBUMBUMBU miaka yote kwa sababu ya mitizamo waliyojengewa kuwa SIASA ndio mlango pekee wa kutokea na kufanikiwa kimaisha, hivyo kwa nini tushangae sasa kuona vijana wetu wakikimbilia siasa? MEMBE AMEKOSEA NA AFIKIRIE MARA MBILI KABLA YA KUAMUA
Enzi zangu nilipokua nasoma chuo kikuu pale Mlimani miaka ya 90 mwanzoni, elimu yetu haikuchanganywa na siasa hata kidogo, na mpaka nimekwenda nchi za magharibi hawana "longolongo" kama hawa wanasiasa wa bongo. Kule ni vitendo zaidi na wanafunzi wanajielewa na hawataki kurubuniwa. kwani kama Membe anawapenda sana wanafunzi basi si angejikita katika utatuzi wa TATIZO LA MIKOPO ELIMU YA JUU kwa kutumia uzoefu wake wa Mambo ya nje? si angechukua mifano hiyo?, nawaomba sana wanahabari msipuuze ujumbe huu ili jamii iweze kuelewa ukiritimba anaotaka kuufanya. Kwa nini tuwe wazalishaji wa MAJANGA kila siku badala ya NEEMA? Mara utasikia DOWANS, RICHMOND, NISHATI NA MADINI nk sasa ni kuzaa BALAA LA SIASA VYUONI? Tusikubali hata chembe. Pia wadogo zangu vyuoni acheni kuwa wafuasi wa wanasiasa ,igeni mifano ya wasomi wenzenu katika nchi zilizoendelea wanavyofanya. Vinginevyo yatatokea yale ya SOMALIA, SYRIA, LIBYA, JORDAN nk.
Chuo kikuu Dodoma (UDOM) kila siku migogoro, ni nani asiyejua kuwa chanzo chake ni siasa? Taratibu turuhusu ujinga huu kupenyeza kwa vyuo vingine vinavyotegemewa sana nchini kama Mzumbe na SUA (Sokoine University of Agriculture)?? Membe awaache hawa vijana wajisomee, wamechakachua UDOM sasa yatosha . Vinginevyo vijana wakigundua hizi hila za wanasiasa kuwa ndiyo chanzo cha wao kutofanikiwa naamini kabisa kuwa WORLD WAR III itaanzia Tanzania. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu wabariki wanafunzi wa vyuo vikuu.
NB....wanahabari mnaweza mkaichapa hii habari kwenye magazeti ama mkaihariri kwa kutumia upeo na taaluma zenu..
Membe anapoanza kupotea ni pale anapoutafuta urais 2015 kwa nguvu zote hata kwa kutumia pesa za wizara yake kwa usiri mkubwa. Hivi sasa ameanzisha kampeni kubwa ya kuwateka vijana hasa wale wenye UWEZO WA USHAWISHI KWA WENZAO ambao wanapatikana vyuo vikuu. Anataka kutumia nafasi ya kutengeneza makongamano katika vyuo ili kuanza mapema kujitengenezea jina zuri ifikapo 2015.
Habari nyeti zinasema kuwa bwana Membe akishirikiana na viongozi wa CCM katika vyuo vikuu, anafanya ajenda ya siri kuwarubuni viongozi wa serikali za wanafunzi ( marais wa vyuo) kwa kuwapa pesa ili waandae makongamano yatakayowaunganisha wanafunzi ili apate mwanya wa kutoa hotuba zake za kujiweka safi zaidi.
Hivi karibuni anaandaa kongamano kubwa kwa kuwatumia wanaCCM vijana wa vyuo vikuu Morogoro (Mzumbe, SUA,St. Jordan, Muslim na Ardhi). Anatumia mwanya huo akijifanya anazungumzia mambo ya ajira na uchumi, maana ameshajinadi sana kuwa yeye ni bingwa sana wa uchumi. Pia amejipanga kuwatumia watu wengine mashuhuri nchini km wafanyabiashara wakubwa, wanamichezo, wanaharakati nk ili kuambatana nao katika hayo makongamano yasiyo na tija kwa vijana. Amepanga bajeti kubwa mno kuweza kuwagharimia usafiri wa bure kutoka vyuoni mwao mpaka pale atakapotaka kuwakusanya hao maelfu ya wasomi wasio na hatia ambao wataingizwa katika wimbi la siasa bila wao wenyewe kujijua. Kwa sasa kongamano kubwa la kuwakutanisha wanavyuo wa Morogoro amepanga kulifanya chuo kikuu Mzumbe katika ukumbi wa NAH (New Assembly Hall), huku akiambatana na mfanyabiashara mkubwa ili kusingizia kuwa ndiye aliyetoa wazo na mapesa kwa ajili ya makongamano hayo.
Hatukatai mawaziri au wanasiasa kuhutubia katika vyuo vikuu kwani nao kimsingi ni wananchi tena wenye taaluma zao. Lakini kwa nini kuharibu upeo wa kufikiri wa vijana kwa kuwaingiza kwenye siasa?.kwa nini kuwatumia viongozi wa serikali za wanafunzi kueneza itikadi za mtu binafsi ama chama? je, vyuo vikuu vikiongozwa kwa kuangalia itikadi za chama fulani cha siasa, nchi hii itazaa wasomi wa namna gani? tatizo la RUSHWA je, litakwisha kweli ikiwa hawa vijana waddogo viongozi wa vyuo wanafundishwa kuwa MAFISADI? tatizo la elimu Tanzania litakwisha kweli ikiwa siasa ndiyo inayotawala katika taasisi za elimu? kwa hapo Membe amekosea na wanaharakati pamoja na wanahabari wanatakiwa kulipigania kwa nguvu zote swala hilo nyeti sana.
Vijana ni "thinking tank of the nation". Sasa ikiwa akili zao zitakua "corrupted" na porojo za kisiasa tokea awali katika hatua za mwanzo kabisa za ukombozi wa fikra, je hii si balaa kwa taifa? MBAYA ZAIDI ni pale wanafunzi wa vyuo wanapopoteza muda wao wa kujisomea na kuanza kujadli mambo ya siasa. Ndiyo maana wanavyuo wetu watazidi kuwa maMBUMBUMBU miaka yote kwa sababu ya mitizamo waliyojengewa kuwa SIASA ndio mlango pekee wa kutokea na kufanikiwa kimaisha, hivyo kwa nini tushangae sasa kuona vijana wetu wakikimbilia siasa? MEMBE AMEKOSEA NA AFIKIRIE MARA MBILI KABLA YA KUAMUA
Enzi zangu nilipokua nasoma chuo kikuu pale Mlimani miaka ya 90 mwanzoni, elimu yetu haikuchanganywa na siasa hata kidogo, na mpaka nimekwenda nchi za magharibi hawana "longolongo" kama hawa wanasiasa wa bongo. Kule ni vitendo zaidi na wanafunzi wanajielewa na hawataki kurubuniwa. kwani kama Membe anawapenda sana wanafunzi basi si angejikita katika utatuzi wa TATIZO LA MIKOPO ELIMU YA JUU kwa kutumia uzoefu wake wa Mambo ya nje? si angechukua mifano hiyo?, nawaomba sana wanahabari msipuuze ujumbe huu ili jamii iweze kuelewa ukiritimba anaotaka kuufanya. Kwa nini tuwe wazalishaji wa MAJANGA kila siku badala ya NEEMA? Mara utasikia DOWANS, RICHMOND, NISHATI NA MADINI nk sasa ni kuzaa BALAA LA SIASA VYUONI? Tusikubali hata chembe. Pia wadogo zangu vyuoni acheni kuwa wafuasi wa wanasiasa ,igeni mifano ya wasomi wenzenu katika nchi zilizoendelea wanavyofanya. Vinginevyo yatatokea yale ya SOMALIA, SYRIA, LIBYA, JORDAN nk.
Chuo kikuu Dodoma (UDOM) kila siku migogoro, ni nani asiyejua kuwa chanzo chake ni siasa? Taratibu turuhusu ujinga huu kupenyeza kwa vyuo vingine vinavyotegemewa sana nchini kama Mzumbe na SUA (Sokoine University of Agriculture)?? Membe awaache hawa vijana wajisomee, wamechakachua UDOM sasa yatosha . Vinginevyo vijana wakigundua hizi hila za wanasiasa kuwa ndiyo chanzo cha wao kutofanikiwa naamini kabisa kuwa WORLD WAR III itaanzia Tanzania. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu wabariki wanafunzi wa vyuo vikuu.
NB....wanahabari mnaweza mkaichapa hii habari kwenye magazeti ama mkaihariri kwa kutumia upeo na taaluma zenu..