AG, Mshauri Mh.Rais Atoe Maagizo kwa Presidential Decrees Kuyapa Nguvu ya Kisheria

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,494
113,590
Wanabodi,

Nchi zote zinazoheshimu katiba, zinaendeshwa kwa mujibu Katiba, sheria, taratibu na kanuni na sio kwa kauli za viongozi tuu ambazo kauli nyingine zinakwenda kinyume cha katiba, sheria, taratibu na kanuni!.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndie mkuu wa nchi, head of state, ndie mkuu wa serikali, Head of the Government, Mkuu wa Mhimili wa the Executive na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama , ambaye pía ni sehemu ya Bunge kwa kulizindua, kulivunja, na kuidhinisha miswada kuwa sheria na kuteua mtendaji mkuu wa Bunge, (Katibu wa Bunge), na pia rais ni sehemu ya mahakama kwa kumteua Jaji Mkuu, Mkuu wa Mhimili wa Mahakama, Mtendaji Mkuu wa Mahakama, kuteua Majaji, kuidhinisha adhabu ya kifo na kutoa msamaha kwa wafungwa. Rais kama Mwenyekiti wa Chama Tawala, ndie hupitisha jina la Spika na majina ya wabunge wote watakaokuwa mawaziri.

Hivyo kwa muundo huu, rais wa JMT ndio kila kitu. Hii inamfanya rais kila agizo analolitoa lihesabiwe kama amri ni sheria, atakayekiuka anatumbuliwa!.

Serikali inaendeshwa kwa mujibu wa kitu kinachoitwa "Government Standing Orders" lakini sasa tunashuhudia baadhi ya standing orders zikiwekwa pending na badala yake sasa serikali yetu inaendeshwa kwa kauli za viongozi!.

Kikatiba, kisheria, kitaratibu na kikanuni, sio kila maagizo ya rais ni sheria kiasi cha kupelekea kila anayekwenda kinyume cha maagizo ya rais anahesabiwa amefanya kosa la insubordination ambayo adhabu yake ni summary dismissal kwa kuwa condemned unheard.

Ili kauli ya rais iwe ni sheria, kauli hiyo ikiishatolewa lazima ifuatiwe na maandishi, au a Presidential Decree ambayo ndio amri rasmi ya kiRaisi kuhusu jambo lolote ambalo rais ameliagiza, hiyo predidential decree inapata nguvu ya kisheria baada ya kuchapishwa kwenye gazeti la serikali, Government Gazzette, hivyo atakayekiuka agizo hilo itampasa hukumu.

Hata lile tangazo la kufuta maandimisho sherehe za uhuru, kiukweli kabisa, mwanzo lilotolewa kienyeji enyeji!, baada ya sisi kulipigia kelele humu, Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria, ongoza kwa 'presidential decrees'! ndipo ikulu wakatoa a decree na kui back date!, hivyo agizo hilo lilifuatiwa na maandishi huku yakieleza ni kwa mujibu wa mamlaka gani, sheria gani, kifungu gani, taratibu gani na kanuni gani au a presidential decree.

Tangazo la taasisi za umma kuhifadhi fedha zake BOT pekee pia lilitakiwa kufuatiwa na decree ili liwe ndio sheria mpya ya hifadhi ya fedha za umma. Sikumbuki kuona deceee yoyote ya rais kwenye hili!

Kwa mujibu wa Gavana wa BOT, Prof.Benno Ndulu sio makosa kwa taasisi za umma kuweka fedha kwenye Fixed Deposit
https://www.jamiiforums.com/threads/gavana-bot-kufungua-akaunti-maalum-si-kosa hivyo kama rais ameitumbua bodi ya TRA kwa kosa la kukiuka maagizo yake, ametumia his appointment powers to hire and fire as he pleases lakini bodi hiyo haina kosa lolote kisheria kufungua hiyo FDA.

Kwa vile all banking transactions zinafanywa transparently na all the records ziko in black and white, kama kuna wakuu wowote waliozipiga fedha za FDA then wachukuliwe kama majizi mengine yoyote na wizi ni kosa la jinai halina limitation of time, hivyo wahusika watafutwe na kushitakiwa regardless walifanya wizi huo lini, lakini kama bodi ya TRA ilifanya kwa nía njema, tangazo la rais la sababu za kuivunja bodi ya TRA ni udhalilishaji kwa waliokuwa wajumbe wa bodi hiyo kuonekana kuwa kumbe walitaka kutuibia akiwemo Gavana Ndulu. Ningekuwa mimi kesho yake tuu angeikuta barua yangu mezani kwake.

Presidential powers to appoint hazimtaki rais kutoa sababu zozote kwanini amemteua fulani na akiamua kumtengua uteuzi halazimishwi kutoa sababu zozote kwa nini amemtengua fulani kwa sababu teuzi na tengua, zinafanyika at his pleasures, sasa kama raus aliamua kutosema sababu siku alipoamua kutengua, alipaswa asiseme kabisa hizo sababu forever na sio leo anatengua hasemi sababu halafu kesho anasema sababu, huku ni kuwadhalilisha watenguliwa kwa kila anayetenguliwa kuonekana ni jipu!, hii inconsistency is not good for presidential institutions kwa vile rais ni taasisi anaoaswa afanye mambo ki taasisi na sio kiutashi, na akifanya maamuzi ya kiutashi yafuatiwe na kutaasishwa ili yawe ya kitaasisi.

Hata rais aliposema atafuta mishahara ya peponi, watu tulisema humu, Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote

Hili swali nililo muuliza rais Magufuli pale ikulu, ile November 4, Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli ni swali very valid!. Japo rais alipiga chenga kulijibu, ilipaswa wasaidizi wake waje wamjibie siku za usoni, baadhi ya hizi amri za rais zinazokwenda kinyume cha katiba, rais Magufuli anazitoa kwa mamlaka gani kwenye kifungu gani na sheria gani?. Akitoa amri yoyote ambayo haipo kikatiba, kisheria, kitaratibu na kikanuni, atoe a presidential decree to support it!.

Najua rais wetu Mhe. Dr John Pombe Joseph Magufuli anayafanya haya yote kwa nía njema, in good faith ila katika kuyafanya haya lazima azingatie katiba, sheria, taratibu na kanuni na pia sio tuu kwa kufanya the right thing at the right time, but he got to do it right.

Paskali
 
Kwanza anajua kabisa kwamba he is wrong na utakaa ukisikia akimjibu professor Ndulu........

Hivi Mtu tajiri kama Mengi au Bakhiresa ana utajiri unaokaribia 1 trions na bank unakuta wana angalau pesa tasilimu billion 100 wanatunziwa na mabenki lakini wakiitaji pesa wanaenda kwenye bank hizo hizo kukopa.......

Ina maana bodi ya Bakhiresa inayopitisha kwamba wakakope yenye watu waliobobea kwenye mambo ya utawala na financial wanakuwa ni wajinga?....


Wanakopa na pesa zao bado zipo bank kwenye fixed deposits na wanaendelea kulipa riba ya mikopo yao........ .

Serikali inayoogopa kukopa na kuweka pesa kwenye bank za ndani alafu inajidai ipo kwenye mixed economy ni kudanganya umma,......

Nchi zote zilizoendelea hata marekani pesa za serikali zinawekwa kwenye bank za biashara ili Ku boost investment in private sector..........
 
Mkuu Pascal Mayala Jf Member Uliyewahi Kumuuliza Rais Wa JMT Swali Bora Kuwahi Kuulizwa Awamu Hii Ya Tano Kwa Huu Mwaka Mmoja Wa Uongozi Wa Rais.

Leo Tena Umekuja Na Swali/Hoja Nzito Ambayo Kwa Wale Wanaelekeza Hisia Zao Kwenye Mahaba Ya Vyama Halijibiki Hata Yule Uliyemuuliza Wakati Ule Hili Pia Hawezi Kulijibu Zaidi Ya Porojo.

Kwasasa Nchi Hii Viongozi Wengi Ni Waoga Sana Tena Wanafki Mno YaaNi Kila Jambo Tunasifia Tu Kulinda Vyeo Na Hata Anapokosea Jamaa Wanamtazama.

Utawakuta Wako Mitaani Wanalalamika Tu Na Baadhi Yao Wanaona Mambo Yanaharika Hofu Zimewatanda
Huwezi Kuamini Yanayoendelea Hayawapendezi Wengi
 
Uongozi wa nchi sio Uongozi wa NZENGO. Unapoongoza nchi kama nzengo, madhara yake ni kuteua mtu baada ya muda unamtumbua kisha unamteua tena. TAFSIRI yake wewe si mtu SAHIHI kufanya maamuzi sahihi. (Rejea Kuteuliwa-Kutumbuliwa-Kuteuliwa kwa Diwani At human)
 
Moja ya mabandiko mujarabu kwa mwaka huu 2016 ni hili
lakini nikiangalia degree of confidence ya AG wetu sioni uthubutu wa kufanya hili ombi muhimu kwa kweli. WELEDI pia ni kigezo kingine kinachomfanya pengine akose ujasiri na kujiamini AG wetu kutoa ushauri huu.
 
Paskali, kuna wakati kulikuwa na taarifa kuwa rais wa Uganda alikuwa na washauri 70 , ila kila alipokuwa anakutana nao alikuwa akiwashauri yeye badala ya yeye kushauriwa......ya AG nakuachia wewe ...
 
Rais ana uhuru wa kuteua na kutengua atakavyo bila kuhojiwa. Tumuacheni atumie nguvu na mamlaka yake.
1473759015_fotolia_111548243_subscription_xxl.jpg
 
Wanabodi,

Nchi zote zinazoheshimu katiba, zinaendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni na sio kwa kauli za viongozi ambazo zinakwenda kinyume cha sheria, taratibu na kanuni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndie mkuu was nchi, head of state, ndie mkuu wa serikali, Head of Executive na Amiri Jeshi Mkuu, ambaye pía ni sehemu ya bunge kwa kulizindua, kulivunja, kuidhinisha sheria na kuteua mtendaji mkuu (Katibu wa Bunge), na sehemu ya mahakama kwa kumteua Mtendaji Mkuu na kuidhinisha adhabu ya kifo.

Hivyo kwa muundo huu, rais ndio kila kitu. Hii inamfanya rais kila agizo analolitoa lihesabiwe kama ni sheria, atakayekiuka anatumbuliwa.

Serikali inaendeshwa kwa mujibu wa kitu kinachoitwa "Government Standing Orders" lakini sasa tunashuhudia baadhi ya standing orders zikiwekwa pending na badala yake serikali kuendeshwa kwa kauli za viongozi.

Kisheria kitaratibu na kikanuni, sio kila Maagizo ya rais ni sheria kiasi cha kupelekea kila anayekwenda kinyume cha maagizo ya rais anahesabiwa amefanya kosa la insubordination ambayo adhabu yake ni summary dismissal kwa kuwa condemned unheard.

Ili kauli ya rais iwe ni sheria, kauli hiyo ikiishatolewa lazima ifuatiwe na a Presidential Decree ambayo ndio amri rasmi ya kiraisi kuhusu
jambo lolote ambalo rais ameliagiza, hivyo atakayekiuka agizo hilo itampasa hukumu.

Hata lile tangazo la kufuta maandimisho sherehe za uhuru lilifuatiwa na a presidential decree.

Tangazo la taasisi za umma kuhifadhi fedha zake BOT pekee pia lilitakiwa kufuatiwa na decree ili liwe ndio sheria mpya ya hifadhi ya fedha za umma.

Kwa mujibu wa Gavana wa BOT, Prof.Benno Ndulu sio makosa kwa taasisi za umma kuweka fedha kwenye Fixed Deposit
https://www.jamiiforums.com/threads/gavana-bot-kufungua-akaunti-maalum-si-kosa hivyo kama rais ameitumbua bodi ya TRA kwa kosa la kukiuka maagizo yake, ametumia his appointment powers to hire and fire as he pleases lakini bodi hiyo haina kosa lolote kisheria kufungua hiyo FD.

Kwa vile all banking transactions nzinafanywa transparently na all the records ziko in black and white, kama kuna wakuu wowote waliozipiga fedha za FDA then wachukuliwe kama majizi mengine yoyote na wizi ni kosa la jinai halina limitation of time, hivyo wahusika watafutwe na kushitakiwa regardless walifanya wizi huo lini, lakini kama bodi ya TRA ilifanya kwa nía njema, tangazo la rais la sábado za kuivunja bodi ya TRA ni udhalilishaji kwa waliokuwa wajumbe wa bodi hiyo kuwa kumbe walitaka kutuibia akiwemo Ndulu. Ningekuwa mimi kesho yake tuu angeikuta barua yangu mezani kwake.

Presidential powers to appoint hazimtaki rais kutoa sababu zozote kwanini amemteua fulani na akiamua kutengua uteuzi halazimishwi kutoa sababu zozote kwa sababu hayo yanafanyika at his pleasures, sasa kama aliamua kutosema sababu siku alipoamua, alipaswa asiseme kabisa hizo sababu forever na sio leo hesemi kisha kesho anasema, hii inconsistency is not good for presidential institutions.

Najua rais wetu Mhe. Dr John Pombe Joseph Magufuli anayafanya haya yote kwa nía njema, in good faith ila katika kuyafanya haya lazima azingatie sheria, taratibu na kanuni na pia sio tuu kwa kufanya the right thing at the right time, but he got to do it right.

Paskali[/
Wanabodi,

Nchi zote zinazoheshimu katiba, zinaendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni na sio kwa kauli za viongozi ambazo zinakwenda kinyume cha sheria, taratibu na kanuni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndie mkuu was nchi, head of state, ndie mkuu wa serikali, Head of Executive na Amiri Jeshi Mkuu, ambaye pía ni sehemu ya bunge kwa kulizindua, kulivunja, kuidhinisha sheria na kuteua mtendaji mkuu (Katibu wa Bunge), na sehemu ya mahakama kwa kumteua Mtendaji Mkuu na kuidhinisha adhabu ya kifo.

Hivyo kwa muundo huu, rais ndio kila kitu. Hii inamfanya rais kila agizo analolitoa lihesabiwe kama ni sheria, atakayekiuka anatumbuliwa.

Serikali inaendeshwa kwa mujibu wa kitu kinachoitwa "Government Standing Orders" lakini sasa tunashuhudia baadhi ya standing orders zikiwekwa pending na badala yake serikali kuendeshwa kwa kauli za viongozi.

Kisheria kitaratibu na kikanuni, sio kila Maagizo ya rais ni sheria kiasi cha kupelekea kila anayekwenda kinyume cha maagizo ya rais anahesabiwa amefanya kosa la insubordination ambayo adhabu yake ni summary dismissal kwa kuwa condemned unheard.

Ili kauli ya rais iwe ni sheria, kauli hiyo ikiishatolewa lazima ifuatiwe na a Presidential Decree ambayo ndio amri rasmi ya kiraisi kuhusu
jambo lolote ambalo rais ameliagiza, hivyo atakayekiuka agizo hilo itampasa hukumu.

Hata lile tangazo la kufuta maandimisho sherehe za uhuru lilifuatiwa na a presidential decree.

Tangazo la taasisi za umma kuhifadhi fedha zake BOT pekee pia lilitakiwa kufuatiwa na decree ili liwe ndio sheria mpya ya hifadhi ya fedha za umma.

Kwa mujibu wa Gavana wa BOT, Prof.Benno Ndulu sio makosa kwa taasisi za umma kuweka fedha kwenye Fixed Deposit
https://www.jamiiforums.com/threads/gavana-bot-kufungua-akaunti-maalum-si-kosa hivyo kama rais ameitumbua bodi ya TRA kwa kosa la kukiuka maagizo yake, ametumia his appointment powers to hire and fire as he pleases lakini bodi hiyo haina kosa lolote kisheria kufungua hiyo FD.

Kwa vile all banking transactions nzinafanywa transparently na all the records ziko in black and white, kama kuna wakuu wowote waliozipiga fedha za FDA then wachukuliwe kama majizi mengine yoyote na wizi ni kosa la jinai halina limitation of time, hivyo wahusika watafutwe na kushitakiwa regardless walifanya wizi huo lini, lakini kama bodi ya TRA ilifanya kwa nía njema, tangazo la rais la sábado za kuivunja bodi ya TRA ni udhalilishaji kwa waliokuwa wajumbe wa bodi hiyo kuwa kumbe walitaka kutuibia akiwemo Ndulu. Ningekuwa mimi kesho yake tuu angeikuta barua yangu mezani kwake.

Presidential powers to appoint hazimtaki rais kutoa sababu zozote kwanini amemteua fulani na akiamua kutengua uteuzi halazimishwi kutoa sababu zozote kwa sababu hayo yanafanyika at his pleasures, sasa kama aliamua kutosema sababu siku alipoamua, alipaswa asiseme kabisa hizo sababu forever na sio leo hesemi kisha kesho anasema, hii inconsistency is not good for presidential institutions.

Najua rais wetu Mhe. Dr John Pombe Joseph Magufuli anayafanya haya yote kwa nía njema, in good faith ila katika kuyafanya haya lazima azingatie sheria, taratibu na kanuni na pia sio tuu kwa kufanya the right thing at the right time, but he got to do it right.

Paskali
Sio siri kuwa viongozi na watalamu walioko kwenye serilikali ni woga kiasi cha kushindwa kufanya kazi zao kwa weledi. Hii inanikumbusha utawala mzee Karume, Zanzibar. Ukweli kabisa hatutakiwi kuwaamini wanasiasa, lakini litakuwa kosa kubwa kabisa kuogopa kuhoji na hata kuwa challenge
 
Wanabodi,

Nchi zote zinazoheshimu katiba, zinaendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni na sio kwa kauli za viongozi ambazo zinakwenda kinyume cha sheria, taratibu na kanuni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndie mkuu was nchi, head of state, ndie mkuu wa serikali, Head of Executive na Amiri Jeshi Mkuu, ambaye pía ni sehemu ya bunge kwa kulizindua, kulivunja, kuidhinisha sheria na kuteua mtendaji mkuu (Katibu wa Bunge), na sehemu ya mahakama kwa kumteua Mtendaji Mkuu na kuidhinisha adhabu ya kifo.

Hivyo kwa muundo huu, rais ndio kila kitu. Hii inamfanya rais kila agizo analolitoa lihesabiwe kama ni sheria, atakayekiuka anatumbuliwa.

Serikali inaendeshwa kwa mujibu wa kitu kinachoitwa "Government Standing Orders" lakini sasa tunashuhudia baadhi ya standing orders zikiwekwa pending na badala yake serikali kuendeshwa kwa kauli za viongozi.

Kisheria kitaratibu na kikanuni, sio kila Maagizo ya rais ni sheria kiasi cha kupelekea kila anayekwenda kinyume cha maagizo ya rais anahesabiwa amefanya kosa la insubordination ambayo adhabu yake ni summary dismissal kwa kuwa condemned unheard.

Ili kauli ya rais iwe ni sheria, kauli hiyo ikiishatolewa lazima ifuatiwe na a Presidential Decree ambayo ndio amri rasmi ya kiraisi kuhusu
jambo lolote ambalo rais ameliagiza, hivyo atakayekiuka agizo hilo itampasa hukumu.

Hata lile tangazo la kufuta maandimisho sherehe za uhuru lilifuatiwa na a presidential decree.

Tangazo la taasisi za umma kuhifadhi fedha zake BOT pekee pia lilitakiwa kufuatiwa na decree ili liwe ndio sheria mpya ya hifadhi ya fedha za umma.

Kwa mujibu wa Gavana wa BOT, Prof.Benno Ndulu sio makosa kwa taasisi za umma kuweka fedha kwenye Fixed Deposit
https://www.jamiiforums.com/threads/gavana-bot-kufungua-akaunti-maalum-si-kosa hivyo kama rais ameitumbua bodi ya TRA kwa kosa la kukiuka maagizo yake, ametumia his appointment powers to hire and fire as he pleases lakini bodi hiyo haina kosa lolote kisheria kufungua hiyo FD.

Kwa vile all banking transactions nzinafanywa transparently na all the records ziko in black and white, kama kuna wakuu wowote waliozipiga fedha za FDA then wachukuliwe kama majizi mengine yoyote na wizi ni kosa la jinai halina limitation of time, hivyo wahusika watafutwe na kushitakiwa regardless walifanya wizi huo lini, lakini kama bodi ya TRA ilifanya kwa nía njema, tangazo la rais la sábado za kuivunja bodi ya TRA ni udhalilishaji kwa waliokuwa wajumbe wa bodi hiyo kuwa kumbe walitaka kutuibia akiwemo Ndulu. Ningekuwa mimi kesho yake tuu angeikuta barua yangu mezani kwake.

Presidential powers to appoint hazimtaki rais kutoa sababu zozote kwanini amemteua fulani na akiamua kutengua uteuzi halazimishwi kutoa sababu zozote kwa sababu hayo yanafanyika at his pleasures, sasa kama aliamua kutosema sababu siku alipoamua, alipaswa asiseme kabisa hizo sababu forever na sio leo hesemi kisha kesho anasema, hii inconsistency is not good for presidential institutions.

Najua rais wetu Mhe. Dr John Pombe Joseph Magufuli anayafanya haya yote kwa nía njema, in good faith ila katika kuyafanya haya lazima azingatie sheria, taratibu na kanuni na pia sio tuu kwa kufanya the right thing at the right time, but he got to do it right.

Paskali
Paskali, usihangaike sana...yale ni maagizo ya kikao cha baraza la mawaziri kuhusu fedha za serikali,usisumbuke sana...wateule wa raisi hata bila decree lazima wafuate maagizo. utakapokuja utawala mpya nao watafanya yao ili kutekeleza wanayoyaamini kwani Nyerere,Mwinyi,Mkapa,Kikwete na sasa Magufuli hawafanani, ni lazima tuone tofauti zao,ili dhana ya kila 'zama na vitabu vyake itimie'.
 
Pasco nakubaliana na hoja zako,unachosema leo alishasema Mwl Nyerere miaka 21 iliyopita pale Kilimanjaro Hotel sijui siku hizi inaitwaje.Naomba nimnukuu ingawa si neno kwa neno.

Mosi.Tunamtaka Rais atakaye linda muungano
Pili. Tunamtaka Rais atakayelinda na kuheshimu katiba.

Kipindi hicho bado hata sijaanza kunyoa ndevu,nilimwona Mwl Nyerere kama kiongozi anayetupotezea muda kwakuwa tayari tuliamini Agustine Lyatonga Mrema anatosha.Hayo ya kuheshimu katiba hayana maana hata kidogo,tulikuwa tumeichoka CCM iliyojaa rushwa,iliyopalilia utengeno baina ya Zanzabar na Tanganyika.Isitoshe Mzee Ruksa wakati huo Rais wa JMT alikuwa kama Rais wa Zanzibar zaidi kuliko JMT.

Ujio wa Dr Magufuli na aina ya uongozi anaotuonyesha nimejikuta namkubuka Mwl Nyerere na suala la kuheshimu katiba.
 
Back
Top Bottom