Afrika yaadhimisha mwaka mmoja bila Polio

Afrika yaadhimisha mwaka mmoja bila Polio

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,571
Reaction score
62,162
150724101653_polio_vaccine_512x288_epa_nocredit.jpg

Afrika imepiga hatua kubwa katika kuangamiza ugonjwa wa kupooza Polio.



Bara hili linaadhimisha mwaka mmoja tangu kisa cha mwisho kiripotiwe katika mtoto mdogo nchini Somalia.

Huku wataalam wa afya wakifurahishwa na hatua zilizopigwa Shirika la afya duniani limeonya dhidi ya kulegeza msimamo .

Linasema kuwa chanjo dhidi ya watoto inapaswa kuendelea kutolewa ,lakini swala la usalama nchini Somalia na Nigeria linatoa changamoto chungunzima.

Bara la Afrika linatarajiwa kutoripoti visa vyovyote vya ugonjwa huo kwa miaka miwili zaidi kabla ya ugonjwa huo kuripotiwa kuangamizwa barani humo.

Chanzo: BBC
 
Wamemaliza polio kwa chanjo ambazo hatujui zimetuacha na magonjwa mangapi...
 
Back
Top Bottom