Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,186
- 10,922
Bi Naledi Pandor, Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini ameshangazwa na matumizi ya maneno pekee kutaka misaada ifikishwe Gaza bila vitendo huku watu wakidondoka mitaani kwa njaa.
Amesema wale wale wanaipa Israel silaha iendeleze maangamizi ya Wapalestina kama hawana undumilakuwili kuhusiana na maafa ya Gaza basi wana wajibu wa kufikisha misaada hata kwa kutumia majeshi yao ili vyakula viingie Gaza kuokoa maisha ya watu.
Pamoja na pendekezo hilo, Bi. Naledi ametaka Umoja wa Mataifa ufanyiwe marekebisho makubwa na kiwe chombo cha kidemokrasia zaidi. Kwanza ametaka utaratibu wa veto wa mataifa matano tu uondoshwe na kuwepo na uwakilishi wa kimabara kwenye baraza la Usalama la taasisi hiyo.
Amesema wale wale wanaipa Israel silaha iendeleze maangamizi ya Wapalestina kama hawana undumilakuwili kuhusiana na maafa ya Gaza basi wana wajibu wa kufikisha misaada hata kwa kutumia majeshi yao ili vyakula viingie Gaza kuokoa maisha ya watu.
Pamoja na pendekezo hilo, Bi. Naledi ametaka Umoja wa Mataifa ufanyiwe marekebisho makubwa na kiwe chombo cha kidemokrasia zaidi. Kwanza ametaka utaratibu wa veto wa mataifa matano tu uondoshwe na kuwepo na uwakilishi wa kimabara kwenye baraza la Usalama la taasisi hiyo.