Afrika kuongoza kwa kilimo cha bangi ya matibabu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Kundi la wanasayansi, watafiti na wajasiriamali limesema bara la Afrika linaweza kufikia kuwa mzalishaji mkubwa wa bangi inayotumika kwa ajili ya matibabu.

Jordan Curl; mtaalamu kutoka Kituo cha Uwekezaji na Utafiti wa Bangi cha nchini Israel amewaambia wajumbe wanaohudhuria mkutano wa teknolojia ya mihadarati mjini Cape Town, Afrika ya Kusini, kuwa "Afrika itakuwa kitovu cha uzalishaji bangi duniani."
Kulingana na taasisi moja ya mjini London, soko la bangi na bidhaa za zao hilo kutoka Afrika linatarajiwa kufikia thamani ya dola bilioni 7.1 ifikapo mwaka 2023.

Wawekezaji wengi wanavutiwa kuwekeza kwenye kilimo cha mihadarati hiyo kusini mwa Afrika kutokana na uwepo wa ardhi kubwa, idadi ya kutosha ya wafanyakazi wanaoweza kuajiriwa kwa fedha chache na hali nzuri ya hewa inayowezesha kustawi kwa bangi.

Afrika Kusini ndiyo taifa linaloongoza barani Afrika kwa uzalishaji wa bangi likifuatiwa na Zimbabwe na Lesotho, ambazo hivi karibuni zimetoa leseni ya kilimo cha bangi kwa matumizi ya kitabibu.
1575014634125.png


Chanzo: DW Swahili.
 
Hii nchi ina laana! Biashara hii ni biashara isiyohitaji sayansi ya roketi kuifanya ila utaambiwa ni haramu
 
Back
Top Bottom