Africa Cup of Nations (AFCON) 2015 updates

Africa Cup of Nations (AFCON) 2015 updates

Hawa nao wanatuchelewesha kulala tu, maana sahivi dakika 90 zingekuwa zishakamilika.
 
Mi naona kosa pekee la refa ni kuzima kadi nyekundu alostahili mchezaji wa ghana just baada ya 1st goal
 
Hivi FFU hawapo wawatulize

EQG ina jumla ya raia 600000 tu na huenda police hawazidi elfu 1 na hawawezi kutuliza ghasia hzo.
Labda wadeploy toka nchi zingine za jirani.
 
Wange wakodi wale askari walio mshughulikia Lipumba!
 
Mashabiki wa Ghana ndo wamekimbilia uwanjani baada ya kuchezea kichapo jukwaani.
 
yaani ingekuwa bongo basi saa hizi uwanja ungekuwa umejaa moshi tu vijana wa ERNEST MANGU wangekuwa wamekichafua zamani!

bonge ushenzi tu!
Hawa mashabiki wanadiriki pia kuirushia makopo helicopter ya police inayopita juu ya uwanja.
 
Hawa mashabiki wa Guinee equtorial wangekuwa wanakinukisha hivi na kwa dictator rais wao anayeinyonya nchi yenye utajiri wa mafuta,basi wangekuwa mbali kweli kiuchumi
 
Kuna kila dalili ya mambo kunuka hapo.
Hebu tuone yatakayojiri ila naona wachezaji wa ghana wako katika hali ya utulivu sana ila mashabiki wa EQG wanaendelea kurusha chupa, wanang'oa viti na kurusha uwanjani kama mashabiki wa simba vile!

Hata hizi rangi za jezi zao zinaashilia usimba usimba.
 
Mi naona kosa pekee la refa ni kuzima kadi nyekundu alostahili mchezaji wa ghana just baada ya 1st goal

Nadhan red card alistahili golikipa wa E. Guinea na si kinyume chake
 
Safari yao imeishia hapo,nalazima watakuwa wanacheza bila mashabiki next round,alafu mbona game ya mwisho EqG walibebwa sana,
 
Sijapata kuona watu wapu....vu kama hawa jamaa
 
Hata hizi rangi za jezi zao zinaashilia usimba usimba.

kumbe!
Sijui kwa nini rangi nyekundu wanapenda sana kung'oa vitu uwanjani?
Cc Simba, @EQG
 
Last edited by a moderator:
Hawa mashabiki wa Guinee equtorial wangekuwa wanakinukisha hivi na kwa dictator rais wao anayeinyonya nchi yenye utajiri wa mafuta,basi wangekuwa mbali kweli kiuchumi

Si umeshasema kuwa rais dictator!! Anaweza ua raia wake wote tena kwa hao 600000 tu mbona dakika tu anaweza kumaliza wote?
 
Bila kusahau jamani mpira huu umesimama tangu dakika ya 82 mpaka sasa!
 
Kisheria ni kwamba mpira ukisimama kwa dakika 15 refa ana uamuzi wa kusitisha mechi na mechi ikarudiwa au ukafanyika utaratibu mwingine ufanyike. Ila hawa mashabiki ni wajinga na wasidhani kama refa/fifa ataamua hii mechi irudiwe.
 
Back
Top Bottom