Afisa kilimo wa kata ameng'oa mahindi kwenye shamba la Mama yangu akamlazimisha ampe na kuku wawili

maliuogo

Member
Jul 30, 2017
62
30
Kama nilivoeleza hapo juu, mimi ni kijana mtafutaji kwa sasa niko hapa mjini Dar, sasa kule kijijini kwetu wanyonge wanaonewa kweli wapendwa. Mama yangu mzazi anashamba lake kalima pamba kachanganya na mahindi kwenye ile pamba na amefanya hivo kwa lengo lakutaka kujiongezea kipato. Maana ana eneo dogo la kulima ndio akaamua alime mazao mawili kwenye eneo moja, lakini sasa kipindi anaanza kulima mpaka mazao yamekua hakupewa hata ushauri wowote kutoka kwa Afisa kilimo.

Sasa kinachoumiza leo hii pamba na mahindi yameanza kubeba watoto anakuja afisa kilimo wa kata na mtendaji wa kijiji kaambiwa ayatoe mahindi kwenye pamba . Mama akayatoa alipomaliza kuyatoa kaambiwa alipe kuku lasivyo wamkamate waende naye polisi. Mama kwakuwa ndio na uzee umemsogelea alipoambiwa kupelekwa polisi ikabidi awape kuku wawili ndio wakamuacha.

Sasa mimi nimeambiwa leo hii na Mama yangu alipoenda kutafuta simu kwa jirani ili anipigie .Wapendwa kwa hali hii kweli ndio tunatetea wanyonge nimeumia sana naombeni ushauri wenu.

Afisa kilimo huyu anapatikana mkoa wa Mwanza wilaya ya Misungwi, kata ya Mamaye ndio anapofanyia kazi.
Naombeni tu ushauri jamani ukiona labda nimekukwaza nishauri tu usinitukane. Ahsanteni
 
Unawanunulia simu wanawake wa Dar mama yako hata tecno ya 15,000 hana ? Maliza hiyo aibu ya kifamilia ndio uje mbele ya wanaume. Kijijini hata vi bibi vinazo itel wewe huku unahonga iphone. Unachopewa baada ya kuhonga hakijai kwenye kisosi
 
Kama nilivoeleza hapo juu, mimi ni kijana mtafutaji kwa sasa niko hapa mjini dar, sasa kule kijijini kwetu wanyonge wanaonewa kweli wapendwa. Mama yangu mzazi anashamba lake kalima pamba kachanganya na mahindi kwenye ile pamba na amefanya hivo kwa lengo lakutaka kujiongezea kipato.Maana anaeneo dogo la kulima ndio akaamua alime mazao mawili kwenye eneo moja, lakini sasa kipindi anaanza kulima mpaka mazao yamekua hakupewa hata ushauri wowote kutoka kwa Afisa kilimo.

Sasa kimachoumiza leo hii pamba na mahindi yameanza kubeba watoto anakuja afisa kilimo wa kata na mtendaji wa kijiji kaambiwa ayatoe mahindi kwenye pamba . Mama akayatoa alipomaliza kuyatoa kaambiwa alipe kuku lasivyo wamukamate waende nae polisi. Mama kwakuwa ndio na uzee umemusogelea alipoambiwa kupelekwa polisi ikabidi awape kuku wawili ndio wakamuacha.

Sasa mimi nimeambiwa leo hii na Mama yangu alipoenda kutafuta simu kwa jirani ili anipigie .Wapendwa kwa khali hii kweli ndio tunatetea wanyonge nimeumia sana naombeni ushauri wenu.
Afisa kilimo huyu anapatikana mkoa wa Mwanza wilaya ya Misungwi, kata ya Mamaye ndio anapofanyia kazi.
Naombeni tu ishauri jamani ukiona labda nimekukwaza nishauri tu usinitukane. Ahsanteni
Kwanza kama wadau walivyoshauri, mnunulie mama simu pamoja na kasolar kazuri ka kuicharge.

Pili, huna ndugu pale mama anapoishi?
Tatu, mwambie mama aende mbele zaidi na asiogope kutetea haki yake. Inatakiwa alipwe pamoja na hayo mahindi yaliyokatwa.
 
Hivi TAKUKURU si ipo kwa kazi hiyo? Kutuletea hiyo hadithi humu ili upate huruma ya wadau haina maana. Peleka tatizo lako panapohusika.
 
Hua mnawasiliana vp? Mtafutie kwanza simu mama yako. Inawezekena angekua na simu yote hayo yasingetokea, angewajulisha mapema.
 
Hivi TAKUKURU si ipo kwa kazi hiyo? Kutuletea hiyo hadithi humu ili upate huruma ya wadau haina maana. Peleka tatizo lako panapohusika.



TAKUKURU!!!? ni aina ya muwindaji anayesubiri kufuatwa na mnyama na siyo yeye kumfuata mnyama hata kama ameambiwa alipo.
 
Nilishawahi kusimamia mitihani shule ya Msingi Mamaye (kpnd hicho ikiwa ni kata ya Kolomije),nitakusaidia kuzungumza na mtendaji wa kijiji cha Magaka pamoja na WEO wa Mamaye ili wanidhibitishie hilo na kama itakuwa kweli walifanya hivyo basi nitakupa namba za Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Misungwi pamoja na Afisa wa Takukuru Wilaya,vilevile nitakupatia namba ya Mkuu wa kituo cha police Wilaya

Lakn,kumbuka kuwa ni makosa kuchanganya pamba na zao lingine so,kosa la huyu Afisa Kilimo ni kuchukua kuku!
 
Jamani tuweni makini sana
Afisa Kilimo hawezi kufanya hivyo
Nakama amefanya hivyo kunasababu
Je Amelima kwenye chanzo cha maji
Au ili kupata pamba zuri je inaruhusiwa kuchanganya namazao mengine ?
Kama walishakatanzwa kufanya hivyo
 
Nilishawahi kusimamia mitihani shule ya Msingi Mamaye (kpnd hicho ikiwa ni kata ya Kolomije),nitakusaidia kuzungumza na mtendaji wa kijiji cha Magaka pamoja na WEO wa Mamaye ili wanidhibitishie hilo na kama itakuwa kweli walifanya hivyo basi nitakupa namba za Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Misungwi pamoja na Afisa wa Takukuru Wilaya,vilevile nitakupatia namba ya Mkuu wa kituo cha police Wilaya
Lakn,kumbuka kuwa ni makosa kuchanganya pamba na zao lingine so,kosa la huyu Afisa Kilimo ni kuchukua kuku!

Mpe hizo namba aamue yeye
Jinsi unazishikilia utafikiri ni wewe peke yako ndio unazifahamu au kuweza kuzijua.
Na huyo Afisa pia inaelekea anajua watu wanakosea ila anaacha hadi aje kuwaumiza mioyo na kujipatia kitu kama kwa huyu kuku.
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Nilishawahi kusimamia mitihani shule ya Msingi Mamaye (kpnd hicho ikiwa ni kata ya Kolomije),nitakusaidia kuzungumza na mtendaji wa kijiji cha Magaka pamoja na WEO wa Mamaye ili wanidhibitishie hilo na kama itakuwa kweli walifanya hivyo basi nitakupa namba za Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Misungwi pamoja na Afisa wa Takukuru Wilaya,vilevile nitakupatia namba ya Mkuu wa kituo cha police Wilaya
Lakn,kumbuka kuwa ni makosa kuchanganya pamba na zao lingine so,kosa la huyu Afisa Kilimo ni kuchukua kuku!
Monde arabe

Fafanua kidogo, kwanini ni kosa kuchanganya pamba na zao lingine.
 
Nilishawahi kusimamia mitihani shule ya Msingi Mamaye (kpnd hicho ikiwa ni kata ya Kolomije),nitakusaidia kuzungumza na mtendaji wa kijiji cha Magaka pamoja na WEO wa Mamaye ili wanidhibitishie hilo na kama itakuwa kweli walifanya hivyo basi nitakupa namba za Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Misungwi pamoja na Afisa wa Takukuru Wilaya,vilevile nitakupatia namba ya Mkuu wa kituo cha police Wilaya
Lakn,kumbuka kuwa ni makosa kuchanganya pamba na zao lingine so,kosa la huyu Afisa Kilimo ni kuchukua kuku!
Wewe ndio umetoa msaada safi mkuu
 
Kama nilivoeleza hapo juu, mimi ni kijana mtafutaji kwa sasa niko hapa mjini dar, sasa kule kijijini kwetu wanyonge wanaonewa kweli wapendwa. Mama yangu mzazi anashamba lake kalima pamba kachanganya na mahindi kwenye ile pamba na amefanya hivo kwa lengo lakutaka kujiongezea kipato.Maana anaeneo dogo la kulima ndio akaamua alime mazao mawili kwenye eneo moja, lakini sasa kipindi anaanza kulima mpaka mazao yamekua hakupewa hata ushauri wowote kutoka kwa Afisa kilimo.

Sasa kimachoumiza leo hii pamba na mahindi yameanza kubeba watoto anakuja afisa kilimo wa kata na mtendaji wa kijiji kaambiwa ayatoe mahindi kwenye pamba . Mama akayatoa alipomaliza kuyatoa kaambiwa alipe kuku lasivyo wamukamate waende nae polisi. Mama kwakuwa ndio na uzee umemusogelea alipoambiwa kupelekwa polisi ikabidi awape kuku wawili ndio wakamuacha.

Sasa mimi nimeambiwa leo hii na Mama yangu alipoenda kutafuta simu kwa jirani ili anipigie .Wapendwa kwa khali hii kweli ndio tunatetea wanyonge nimeumia sana naombeni ushauri wenu.
Afisa kilimo huyu anapatikana mkoa wa Mwanza wilaya ya Misungwi, kata ya Mamaye ndio anapofanyia kazi.
Naombeni tu ishauri jamani ukiona labda nimekukwaza nishauri tu usinitukane. Ahsanteni
Pole sana mkuu huyo afisa kilimo anaitwa nani?
 
Back
Top Bottom