Kilimo ni biashara, kilimo ni kazi, kilimo ni ajira. Huu utaritibu wa uwepo wa vitu vinavyoitwa vyama vya ushirika na vyama vya msingi havimsaidii mkulima bali vina muangamiza. Huu utaratibu wa uwepo wa vyama vya ushirika ulibuniwa na Serikali ya awamu ya kwanza kama njia ya kuimarisha sera ya ujamaa. Ni sera iliyoshindwa na toka enzi hizo hadi leo havijawahi kuwa na manufaa kwa mkulima zaidi ya wizi na ufisadi.
Angalia mazao yote ambayo hayapitii kwenye hivi vyama yanaendelea vizuri. Lakini yale mazao ambao yanasimamiwa na vyama hivi yanadorora siku hadi siku.
Kimsingi hata uwekezaji mkubwa kwenye haya mazao haupo kwa sababu watu hawawe zikuwekeza kwenye mazao haya sababu ya kuogopa urasimu na dana dana.
Wafanya biashara waachwe wanunue mazao moja kwa moja kutoka kwa wakulima, halafu utaona jinsi mazao haya yatakavyo shamiri.
Mh. Magufuli wewe ni mtu wa reforms..tafadhali vunjilia mbali vitu vinaitwa vyama vya ushirika na vyama vya msingi. Acha kilimo iwe kazi huru, biashara huru na ajira huru. Hapo utakuwa umewasidia wakulima
Angalia mazao yote ambayo hayapitii kwenye hivi vyama yanaendelea vizuri. Lakini yale mazao ambao yanasimamiwa na vyama hivi yanadorora siku hadi siku.
Kimsingi hata uwekezaji mkubwa kwenye haya mazao haupo kwa sababu watu hawawe zikuwekeza kwenye mazao haya sababu ya kuogopa urasimu na dana dana.
Wafanya biashara waachwe wanunue mazao moja kwa moja kutoka kwa wakulima, halafu utaona jinsi mazao haya yatakavyo shamiri.
Mh. Magufuli wewe ni mtu wa reforms..tafadhali vunjilia mbali vitu vinaitwa vyama vya ushirika na vyama vya msingi. Acha kilimo iwe kazi huru, biashara huru na ajira huru. Hapo utakuwa umewasidia wakulima