PreGE2025 Ado Shaibu: Mdee na wenzake wakija ACT WAZALENDO tutawapokea kwa kishindo

PreGE2025 Ado Shaibu: Mdee na wenzake wakija ACT WAZALENDO tutawapokea kwa kishindo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Katibu Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Ado Shaibu amesema chama hicho kipo tayari kuwapokea wanasiasa kutoka vyama vingine na kitawapokea kwa heshima ya hali ya juu pindi watapokuwa tayari.

Akizungumza katika mahojiano maalum aliyofanya na Jambo TV Ado, amesema kuwatengeneza baadhi ya hao wanasiasa hasa wanawake sio kazi rahisi hivyo kwa chama chao kuwapata inakuwa ni thamani imeongezeka kwao.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Katika mahojiano hayo amemtaja wanasiasa mashuhuri kama Halima Mdee, Esther Bulaya, Esther Matiko na Catherine Ruge ambao wamejitengenezea majina katika kipindi walichohudumu katika siasa za upinzani.

"watu wa aina hii wakitaka kuja ACT Wazalendo sio kwamba tu tuwapokea, tutawapokea kwa kishindo kinachoendana na heshima yao kwa hiyo tunawakaribisha sana" amesema Ado.

Hata hivyo amesema ni vyema wanasiasa hao wakawachukua kuliko wakaichezea nafasi halafu wakachukuliwa na Chama cha Mapinduzi CCM.
 
Katibu Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Ado Shaibu amesema chama hicho kipo tayari kuwapokea wanasiasa kutoka vyama vingine na kitawapokea kwa heshima ya hali ya juu pindi watapokuwa tayari.

Akizungumza katika mahojiano maalum aliyofanya na Jambo TV Ado, amesema kuwatengeneza baadhi ya hao wanasiasa hasa wanawake sio kazi rahisi hivyo kwa chama chao kuwapata inakuwa ni thamani imeongezeka kwao.

Katika mahojiano hayo amemtaja wanasiasa mashuhuri kama Halima Mdee, Esther Bulaya, Esther Matiko na Catherine Ruge ambao wamejitengenezea majina katika kipindi walichohudumu katika siasa za upinzani.

"watu wa aina hii wakitaka kuja ACT Wazalendo sio kwamba tu tuwapokea, tutawapokea kwa kishindo kinachoendana na heshima yao kwa hiyo tunawakaribisha sana" amesema Ado.

Hata hivyo amesema ni vyema wanasiasa hao wakawachukua kuliko wakaichezea nafasi halafu wakachukuliwa na Chama cha Mapinduzi CCM.
View attachment 3309640

IMG_20250416_173934.jpg
 
Ila hiki chama wanachama wake wa ZNZ wajarbu kukiokoa maana hawa wa Tanganyika wamekaaa kifisifisi sana kula mizoga
 
Back
Top Bottom