JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Katibu Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Ado Shaibu, amesema kuwa Chama hicho kinao wagombea Udiwani kwenye Kata zote Tanzania Bara na Zanzibar.
Lakini pia amessema kwamba tayari kwa Zanzibar wameshapata wagombea kwenye majimbo yote ya Zanzibar na Tanzania Bara.
Aidha amesema kwamba kuna Wanachama kutoka Vyama mbalimbali ikiwemo CCM, ambao wameonesha nia kujiunga na ACT Wazalendo, ambapo ameweka wazi kwamba milango ipo wazi katika kuunganisha nguvu.
Shaibu amesema kwamba Chama hicho kinakusudia kuwa na vuguvugu kubwa ambalo litawezesha kukitoa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.
Ameyasema hayo kwenye Mkutano Mkuu wa Chama hicho unaoendelea Jijini Dar es salaam leo Agost 6, 2025.
Lakini pia amessema kwamba tayari kwa Zanzibar wameshapata wagombea kwenye majimbo yote ya Zanzibar na Tanzania Bara.
Aidha amesema kwamba kuna Wanachama kutoka Vyama mbalimbali ikiwemo CCM, ambao wameonesha nia kujiunga na ACT Wazalendo, ambapo ameweka wazi kwamba milango ipo wazi katika kuunganisha nguvu.
Shaibu amesema kwamba Chama hicho kinakusudia kuwa na vuguvugu kubwa ambalo litawezesha kukitoa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.
Ameyasema hayo kwenye Mkutano Mkuu wa Chama hicho unaoendelea Jijini Dar es salaam leo Agost 6, 2025.