Ada elimu msingi: Hatua moja mbele itakayoturudisha hatua mbili nyuma

kulyunga

JF-Expert Member
Oct 19, 2011
230
421
Salaam na fanaka za msimu huu wa sikukuu ziwe pamoja nanyi nyoote..

straight kwenye mada, nikiwa kama mtanzania wa kawaida, mzazi na mdau wa elimu nadhani tamko la kusitishwa ada na michango yote katika kile kilichopachikwa jina la "elimu msingi" pamoja na kuonekana kina faida lukuki usoni lakini naamini kabisa kilifanyika bila utafiti wa madhara yake hususani katika shule maarufu za KATA ambazo ndizo zinazotengeneza sehemu kubwa ya shule za umma au za kina "sie" tunaofurahishwa na tamko hili la Mzee wa "hapa kazi tu"

kuondolewa kwa michango hii no dhahiri kutapunguza mzigo kwa wazazi na walezi na hivyo kufanya idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa katika sekondari kuwa kubwa.
lakini kwa upande mwingine madhara ystakayotokana na agizo hili ni mengi sana has a kwa mazingira halisi ya nyingi ya shule hizi kimazingira.

kwa mfano shule nyingi za KATA zilijengwa ili kuhudumia KATA nzima na KATA nyingi zina vijiji zaidi ya vinne na hivyo ujengwaji wa nyingi kati ya shule hizi ulifanyika katikati ya KATA hizo na kufanya umbali kwenda na kurudi shule kuwa mkubwa kiasi ambacho kinaweza kumuathiri mwanafunzi kama atalazimika kwenda shule ba kurudi nyumbani kila Siku.

kwa mantiki hiyo wazazi wengi waliridhia na kukubaliana wanafunzi wawe wanakaa shuleni katika hosteli "bubu" ambazo madarasa yalitumika kama mabweni na wazazi walitoa michango ya mahitaji muhimu ikiwemo chakula na vifaa vya nalazi kwa mujibu wa makubaliano yao. hii ilisaidia kupunguza idadi ya watoto hasa wa kike wanaoacha shule kutokana na ujauzito na mazingira yasiyo rafiki hasa umbali wa nyumbani na shuleni.

sasa rasmi serikali imekataza michango yote ya namna hii na tayari wakuu wa shule waliokuwa na hosteli bubu za aina hii wameamriwa kutoziendesha tena.
naona tunarudi kule kule kwa kupoteza watoto wa kike kutokana na mimba, utoro utarudi kule kule kutokana na umbali na hatari ya watoto kufanyiwa ukatili njiani itakuwa ni kubwa zaidi.

kama kweli serikali imedhamiria hili basi hatukuwa tayari tulihitaji utafiti wa kina ambao ungeenda sambamba na ujenzi wa mabweni ili kuepuka kutengeneza matatizo mengine ambayo yataturudisha nyuma hatua nyingi zaidi na kufanya elimu yetu izidi kudorora badala ya kwenda mbele kama tunavyotarajia..
 
serikali ya kukurupakaaaa na vingozi wanakurupuka na wananchi wanakurupuka kushangiliaaa viongozi kukurupukaaa,subiri mje muone
 
serikali iko majini ktk hilo..mi naomba tusubili hiyo sera itakovyoanza kutekelezwa tutaona majibu yake then tuweze ku_judge
 
No Research No Right to Speak, Mleta mada uko sahihi, wangefanya utafiti kwanza KABLA ya kutoa tamko. Kuna msemo unasema vya bure vina UA. Magufuli angeanzisha hili 2017, mwaka huu angefanya utafiti NA kujipanga kwanza.

Naomba niishie hapa nisije itwa mchochezi cyber crime ikanizoa.
 
Wabongo bhana hivi ingekuwaje km mamvi ndo angekuwa rais na ahadi ya elimu bure hadi chuo kikuu???
 
Hivi mwanzisha uzi, mzee wa ng'ombe aliyeahidi elimu bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu uliwahi muuliza hayo? Au uliwahi kufanya huo utafiti unaoutaja hapa?

BTW, suala la chakula na malazi ni jukumu la mzazi, hilo limeelezwa vyema kwenye hii Sera ya elimu bure. Jukumu la wapi mtoto analala na kula haliihusu serikali, isipokuwa kwa shule za serikali za bweni!!
 
No Research No Right to Speak, Mleta mada uko sahihi, wangefanya utafiti kwanza KABLA ya kutoa tamko. Kuna msemo unasema vya bure vina UA. Magufuli angeanzisha hili 2017, mwaka huu angefanya utafiti NA kujipanga kwanza.

Naomba niishie hapa nisije itwa mchochezi cyber crime ikanizoa.

Lowassa alikuwa ameahidi nini kwenye elimu?! Acheni mambo hayo!! Mnatafuta sababu ya kuja kusema anko Magu hakutekeleza ahadi yake ya elimu bure, ili ije iwe kete yenu ya 2020!

Na mtataga maana kila alichoahidi atatimiza!!
 
Walidandia hoja.Hqwakujipanga..nahisi magufuli ana wasiwasi wa kutosha.Ataisoma namba kwa kweli
 
Huu upuuzi nimesema saana hapa watu wanang'ang'ania vyama. Jambo hili ni mwanzo wa kuvurunda elimu na kutoa kafara ajira za wengi. Bora la kuwapa vifaa vya kujifungulia bure kina mama wajawazito halihitaji tafiti kuliko hili.
 
Of coarse... umezungumza fact.. bt kikubwa tunaangalia... kipi kinafaida sana kuilo madhara.... altrrnatvl way way itatumika....
 
Tunao uzoefu in early 60's & 70's tulipofanya nationalisation na kudeclare elimu bure tunasoma yalishindikana iliyopelekea baadae siri kali kurudisha kwa wadau na wamissionary. Wazo ni zuri tatitizo hapa ni "technical know how" Nadhani hapa tutatumia sijui supplimentary model au VP? Jamaa hana nia mbaya ametoa highlight tu kwenye hii program. Kata bila michango sijui serikali italipa mpaka bili za umeme, wapishi, walinzi na test hadi remidial sijui? Daaah God be with us. Tunaliendea Bomu lililotegwa tu linasubiri kulipuka
 
Back
Top Bottom