Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Chama cha ACT Wazalendo kimeahidi kufuta leseni za wavuvi endapo wananchi watawachagua wagombea ubunge na udiwani kutoka katika chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Chama hicho kimekosoa utaratibu wa wavuvi kulipia leseni wakati huohuo wakikatwa tozo ya mafuta tofauti na ilivyo katika sekta ya kilimo ambapo wakulima hulipia tozo ya mafuta pekee wanapotumia matrekta.
Kiongozi mstaafu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe alisema hayo wakati wa mkutano wa kampeni wa chama hicho jimbo la Kigamboni uliofanyika Oktoba 02, 2025 jijini Dar es Salaam.
“Mkulima chombo chake cha kazi ni trekta lakini trekta halina leseni wakati mvuvi chombo chake ni boti na kina leseni, tunaposema taifa la wote maslahi ya wote maana yake haki iwe kwa wote mvuvi na mkulima”, alisema Zitto
Akimnadi Mwanaisha Mdeme ambaye ni mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya chama chake, Zitto alisema mgombea huyo na wagombea wengine wa chama wanaotoka katika maeneo yenye uvuvi wataungana kuwatetea wavuvi nchini.
Aidha alikosoa utaratibu wa mvuvi kulipa leseni za wasaidizi wake wanapokuwa kwenye shughuli za uzalishaji wakati katika sekta nyingine za usafirishaji na kilimo mwenye leseni ni dereva pekee
“Watu wa malori tingo hana leseni lakini kwenye sekta ya uvuvi kila aliyepo ndani ya boti ya uvuvi anakatiwa leseni kwa sababu hamna mtu wa kuwasemea”, aliongeza Zitto
Naye mgombea ubunge katika jimbo hilo, Mwanaisha Mdeme aliwaomba wananchi kumtuma bungeni ili akatatue changamoto za miundombinu na huduma duni za kijamii zilizopo katika jimbo hilo.
“Asubuhi tunapokwenda kwenye shughuli zetu tunashuhudia wanafunzi wakitembea muda mrefu kwenda shule kwa sababu hakuna mabasi ya abiria kutokana na ubovu wa barabara”, alisema Mwanaisha
Chama hicho kimekosoa utaratibu wa wavuvi kulipia leseni wakati huohuo wakikatwa tozo ya mafuta tofauti na ilivyo katika sekta ya kilimo ambapo wakulima hulipia tozo ya mafuta pekee wanapotumia matrekta.
Kiongozi mstaafu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe alisema hayo wakati wa mkutano wa kampeni wa chama hicho jimbo la Kigamboni uliofanyika Oktoba 02, 2025 jijini Dar es Salaam.
“Mkulima chombo chake cha kazi ni trekta lakini trekta halina leseni wakati mvuvi chombo chake ni boti na kina leseni, tunaposema taifa la wote maslahi ya wote maana yake haki iwe kwa wote mvuvi na mkulima”, alisema Zitto
Akimnadi Mwanaisha Mdeme ambaye ni mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya chama chake, Zitto alisema mgombea huyo na wagombea wengine wa chama wanaotoka katika maeneo yenye uvuvi wataungana kuwatetea wavuvi nchini.
Aidha alikosoa utaratibu wa mvuvi kulipa leseni za wasaidizi wake wanapokuwa kwenye shughuli za uzalishaji wakati katika sekta nyingine za usafirishaji na kilimo mwenye leseni ni dereva pekee
“Watu wa malori tingo hana leseni lakini kwenye sekta ya uvuvi kila aliyepo ndani ya boti ya uvuvi anakatiwa leseni kwa sababu hamna mtu wa kuwasemea”, aliongeza Zitto
Naye mgombea ubunge katika jimbo hilo, Mwanaisha Mdeme aliwaomba wananchi kumtuma bungeni ili akatatue changamoto za miundombinu na huduma duni za kijamii zilizopo katika jimbo hilo.
“Asubuhi tunapokwenda kwenye shughuli zetu tunashuhudia wanafunzi wakitembea muda mrefu kwenda shule kwa sababu hakuna mabasi ya abiria kutokana na ubovu wa barabara”, alisema Mwanaisha