ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 643
- 1,603
Ndugu watanzania wote kwa Ujumla, tunawasalimu kwa salamu inayoashiria mabadiliko na uwazi!
Ndugu watanzania wenzetu, pamoja na kuwa na vitu vingi sana duniani vyenye thamani kubwa sana; ni ukweli usiopingika kwamba hakuna kitu chenye thamani inayolingana wala inayokaribia kulingana na thamani ya 'Utu' wa Mtu.Mtu anapozaliwa mtu, anakuwa na thamani ya asili ambayo kwa namna yeyote ile ni lazima ifahamike, iheshimiwe, ilindwe kwa namna yeyote na kufanywa ionekane wakati wote katika jamii yetu.
Katika Misingi ya chama cha ACT-Tanzania, miongoni mwa misingi yake mikubwa ambayo chama kinaisimamia na kitaisimamia, kuilinda na kuitetea, ni pamoja na msingi wa Utu.
"ACT-Tanzania inaamini kuwa sera, mipango na shughuli zozote za kichama au za kiserikali zitakuwa hazina mafanikio ya kudumu kama hazitatambua, kuheshimu na kulinda utu wa kila Mtanzania. Ni kwa sababu hiyo tunu kuu itakayotuongoza katika utumishi wa umma ni kuheshimu, kutambua na kulinda utu wa kila mtu bila kujali tofauti zozote ambazo zinawatofautisha watu"
ACT-Tanzania tunatambua kuwa kuna tofauti nyingi zinazowatofautisha wanadamu.Kwa mfano kuna watu wengine masikini wengine matajiri, wengine wazima wengine walemavu.Vile vile tunafahamu vyema kwamba katika jamii yeyote ni lazima watu wawe na tofauti za kimtizamo; hivyo basi hata katika jamii yetu, tofauti za kimtizamo ni lazima.Hata hivyo ACT-Tanzania inaamini kwamba hakuna tofauti yeyote inayoweza kuhalalisha au kuwa ndio sababu ya kutotambua na kuheshimu utu wa mtu kama vile inavyopaswa.
ACT-Tanzania inaamini kwamba pamoja na tofauti za kisiasa miongoni mwa watu na vyama, ni lazima siasa hizo ziweke mbele msingi wa utu kama nguzo mama ya siasa za msingi, hivyo kuzifanya shughuli zote za kisiasa ziende katika misingi ya ustaarabu na ubinadamu na tofauti zibaki katika sera na itikadi.
Hata hivyo ACT-Tanzania inatambua juu ya uwepo wa idadi kubwa ya watu katika jamii zetu ambao kwa sababu za kisiasa wanaweza ama kupoteza utu wao au kuchezea na kutolinda wala kujali utu wa watu wengine , ili kupata maslahi fulani ya kisiasa.ACT-Tanzania inaamini kwamba jamii hujengwa, na hali hiyo inaweza kubadilishwa taratibu taratibu kwa chama, wanachama, wadau na watanzania wote waliostaarabika kutoa elimu kwa jamii zilizowazunguka kwa nadharia na vitendo na hilo ndilo ambalo chama cha ACT-Tanzania kinalifanya.
Mwisho, Kimsingi jamii inapaswa kufahamu kwamba thamani ya kitu chochote duniani hupatikana kutokana na uwepo wa watu,na watu huwa watu kwa sababu ya hadhi ya utu wao.Hivyo ni jukumu letu sote kuulinda na kuuhifadhi utu wetu na utu wa wawatanzania wenzetu kwa ujumla kwa maslahi ja jamii ya mwanadamu kwa ujumla.Tukiweza kufanya hivyo, itakuwa ni rahisi sasa kupata maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kujenga jamii ya watanzania wenye furaha kama kinavyodhamiria chama chetu.
Ikumbukwe kuwa ACT-Tanzania ni kwa ajili ya Taifa la leo na kesho!
ACT-Tanzania tumedhamiria na bila shaka Mungu atatusaidia!
Ndugu watanzania wenzetu, pamoja na kuwa na vitu vingi sana duniani vyenye thamani kubwa sana; ni ukweli usiopingika kwamba hakuna kitu chenye thamani inayolingana wala inayokaribia kulingana na thamani ya 'Utu' wa Mtu.Mtu anapozaliwa mtu, anakuwa na thamani ya asili ambayo kwa namna yeyote ile ni lazima ifahamike, iheshimiwe, ilindwe kwa namna yeyote na kufanywa ionekane wakati wote katika jamii yetu.
Katika Misingi ya chama cha ACT-Tanzania, miongoni mwa misingi yake mikubwa ambayo chama kinaisimamia na kitaisimamia, kuilinda na kuitetea, ni pamoja na msingi wa Utu.
"ACT-Tanzania inaamini kuwa sera, mipango na shughuli zozote za kichama au za kiserikali zitakuwa hazina mafanikio ya kudumu kama hazitatambua, kuheshimu na kulinda utu wa kila Mtanzania. Ni kwa sababu hiyo tunu kuu itakayotuongoza katika utumishi wa umma ni kuheshimu, kutambua na kulinda utu wa kila mtu bila kujali tofauti zozote ambazo zinawatofautisha watu"
ACT-Tanzania tunatambua kuwa kuna tofauti nyingi zinazowatofautisha wanadamu.Kwa mfano kuna watu wengine masikini wengine matajiri, wengine wazima wengine walemavu.Vile vile tunafahamu vyema kwamba katika jamii yeyote ni lazima watu wawe na tofauti za kimtizamo; hivyo basi hata katika jamii yetu, tofauti za kimtizamo ni lazima.Hata hivyo ACT-Tanzania inaamini kwamba hakuna tofauti yeyote inayoweza kuhalalisha au kuwa ndio sababu ya kutotambua na kuheshimu utu wa mtu kama vile inavyopaswa.
ACT-Tanzania inaamini kwamba pamoja na tofauti za kisiasa miongoni mwa watu na vyama, ni lazima siasa hizo ziweke mbele msingi wa utu kama nguzo mama ya siasa za msingi, hivyo kuzifanya shughuli zote za kisiasa ziende katika misingi ya ustaarabu na ubinadamu na tofauti zibaki katika sera na itikadi.
Hata hivyo ACT-Tanzania inatambua juu ya uwepo wa idadi kubwa ya watu katika jamii zetu ambao kwa sababu za kisiasa wanaweza ama kupoteza utu wao au kuchezea na kutolinda wala kujali utu wa watu wengine , ili kupata maslahi fulani ya kisiasa.ACT-Tanzania inaamini kwamba jamii hujengwa, na hali hiyo inaweza kubadilishwa taratibu taratibu kwa chama, wanachama, wadau na watanzania wote waliostaarabika kutoa elimu kwa jamii zilizowazunguka kwa nadharia na vitendo na hilo ndilo ambalo chama cha ACT-Tanzania kinalifanya.
Mwisho, Kimsingi jamii inapaswa kufahamu kwamba thamani ya kitu chochote duniani hupatikana kutokana na uwepo wa watu,na watu huwa watu kwa sababu ya hadhi ya utu wao.Hivyo ni jukumu letu sote kuulinda na kuuhifadhi utu wetu na utu wa wawatanzania wenzetu kwa ujumla kwa maslahi ja jamii ya mwanadamu kwa ujumla.Tukiweza kufanya hivyo, itakuwa ni rahisi sasa kupata maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kujenga jamii ya watanzania wenye furaha kama kinavyodhamiria chama chetu.
Ikumbukwe kuwa ACT-Tanzania ni kwa ajili ya Taifa la leo na kesho!
ACT-Tanzania tumedhamiria na bila shaka Mungu atatusaidia!
**********************************************
Tutakuwa tukiitolea ufafanuzi Misingi ya Chama cha ACT-Tanzania, mmoja baada ya mwingine kwa kadiri ya uwezo wetu na kwa kutumia mbinu zozote tutakazoweza hadi itakapoeleweka kwa watu wazima wote na wenye akili timamu kwani chama chochote kile bora hujengwa na misingi kwanza.Kwa kuwa kila mtu ana wajibu katika nchi yake; nawe utakuwa umefanya jambo la maana kwa kutuunga mkono kwa kuifundisha misingi hii katika jamii yako.