Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,053
Hii Makala ya ACT ina tofauti gani na yaliyoandikwa humu? CHADEMA, Zitto anakamilisha "siku zake 40" kisha ushindi unafuata! Mbona haijafungwa?
Mkuu Ally Kanah , hivi kuna nini cha kumfanya mtu atukane kwenye uzi huu? kwa kweli inasikitisha ila mimi siku hizi sina mengi ya kusema, ninachosisitiza kila siku ni kwamba "na tufanye tufanyalo, ila tujue tu kwamba mwisho wa ubaya aibu!"Machadema bana ha ha ha mbona povu linawatoka hivyo kwa chama kichanga kama ACT je CCM mtaiweza kweli hali yakuwa ACT inawameza taratibu?? Ha ha ha Kweli Chagadema cha babu majanga na DJ Marienge
Ndugu Mwisho wa ubaya aibu! haya!leo ACT wanakuja na propaganda ileile chini ya kuvuli cha UTU!!!!
Ndugu Mwisho wa ubaya aibu! haya!
Mkuu, vyama vyao vinafananafanana majina: CCK, CCJ, ACT, ADC. Watu wale wale.Nyie mtakuwa kama kile chama cha sijui CCK au sijui CCJ.
Mtakufa karibuni tu.
Naona betlehem anatumia id's zake zote mbili. Moja inaposti ingine inalike interchangeably.
Fun huh!
Ndugu, Mi sielewi hapa hii Tz inaelekea wapi!? Watu wanakuja na maneno wasiyojua hata maana yake!!
Kama sikosei hili ni bandiko lao la kwanza kuhusu MISINGI ya chama, iweje waanze na msingi wa UTU ambao tangu mateso ya Mama yetu pale MOI hadi umauti ccm walikuwa wamevalia njuga, na Misingi ipo mingi lakini eti wamechagua UTU!!?
Wanatuhubiria UTU wakati huo huo wanakiuka UTU kwa Mama yetu!!? Au wanatufanya hamnazo!?
Mkuu, vyama vyao vinafananafanana majina: CCK, CCJ, ACT, ADC. Watu wale wale.
Kama ACT ingalikuwa na watu makini,ingeshakataa support ya ccm.
Vinginevyo,tunashindwa kuwatofautisha!
mkuu kama hueleweki vizuri! unasema ACT-Tanzania ina misingi mingi, hebu tuambie iko mingapi!, itaje!, na utuambie wewe umeiona wapi?
😛uke:😛uke:😛uke:
ACT = CCM's Left hand
Ndugu watanzania wote kwa Ujumla, tunawasalimu kwa salamu inayoashiria mabadiliko na uwazi!
Ndugu watanzania wenzetu, pamoja na kuwa na vitu vingi sana duniani vyenye thamani kubwa sana; ni ukweli usiopingika kwamba hakuna kitu chenye thamani inayolingana wala inayokaribia kulingana na thamani ya 'Utu' wa Mtu.Mtu anapozaliwa mtu, anakuwa na thamani ya asili ambayo kwa namna yeyote ile ni lazima ifahamike, iheshimiwe, ilindwe kwa namna yeyote na kufanywa ionekane wakati wote katika jamii yetu.
Katika Misingi ya chama cha ACT-Tanzania, miongoni mwa misingi yake mikubwa ambayo chama kinaisimamia na kitaisimamia, kuilinda na kuitetea, ni pamoja na msingi wa Utu.
"ACT-Tanzania inaamini kuwa sera, mipango na shughuli zozote za kichama au za kiserikali zitakuwa hazina mafanikio ya kudumu kama hazitatambua, kuheshimu na kulinda utu wa kila Mtanzania. Ni kwa sababu hiyo tunu kuu itakayotuongoza katika utumishi wa umma ni kuheshimu, kutambua na kulinda utu wa kila mtu bila kujali tofauti zozote ambazo zinawatofautisha watu"
ACT-Tanzania tunatambua kuwa kuna tofauti nyingi zinazowatofautisha wanadamu.Kwa mfano kuna watu wengine masikini wengine matajiri, wengine wazima wengine walemavu.Vile vile tunafahamu vyema kwamba katika jamii yeyote ni lazima watu wawe na tofauti za kimtizamo; hivyo basi hata katika jamii yetu, tofauti za kimtizamo ni lazima.Hata hivyo ACT-Tanzania inaamini kwamba hakuna tofauti yeyote inayoweza kuhalalisha au kuwa ndio sababu ya kutotambua na kuheshimu utu wa mtu kama vile inavyopaswa.
ACT-Tanzania inaamini kwamba pamoja na tofauti za kisiasa miongoni mwa watu na vyama, ni lazima siasa hizo ziweke mbele msingi wa utu kama nguzo mama ya siasa za msingi, hivyo kuzifanya shughuli zote za kisiasa ziende katika misingi ya ustaarabu na ubinadamu na tofauti zibaki katika sera na itikadi.
Hata hivyo ACT-Tanzania inatambua juu ya uwepo wa idadi kubwa ya watu katika jamii zetu ambao kwa sababu za kisiasa wanaweza ama kupoteza utu wao au kuchezea na kutolinda wala kujali utu wa watu wengine , ili kupata maslahi fulani ya kisiasa.ACT-Tanzania inaamini kwamba jamii hujengwa, na hali hiyo inaweza kubadilishwa taratibu taratibu kwa chama, wanachama, wadau na watanzania wote waliostaarabika kutoa elimu kwa jamii zilizowazunguka kwa nadharia na vitendo na hilo ndilo ambalo chama cha ACT-Tanzania kinalifanya.
Mwisho, Kimsingi jamii inapaswa kufahamu kwamba thamani ya kitu chochote duniani hupatikana kutokana na uwepo wa watu,na watu huwa watu kwa sababu ya hadhi ya utu wao.Hivyo ni jukumu letu sote kuulinda na kuuhifadhi utu wetu na utu wa wawatanzania wenzetu kwa ujumla kwa maslahi ja jamii ya mwanadamu kwa ujumla.Tukiweza kufanya hivyo, itakuwa ni rahisi sasa kupata maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kujenga jamii ya watanzania wenye furaha kama kinavyodhamiria chama chetu.
Ikumbukwe kuwa ACT-Tanzania ni kwa ajili ya Taifa la leo na kesho!
ACT-Tanzania tumedhamiria na bila shaka Mungu atatusaidia!
**********************************************Tutakuwa tukiitolea ufafanuzi Misingi ya Chama cha ACT-Tanzania, mmoja baada ya mwingine kwa kadiri ya uwezo wetu na kwa kutumia mbinu zozote tutakazoweza hadi itakapoeleweka kwa watu wazima wote na wenye akili timamu kwani chama chochote kile bora hujengwa na misingi kwanza.Kwa kuwa kila mtu ana wajibu katika nchi yake; nawe utakuwa umefanya jambo la maana kwa kutuunga mkono kwa kuifundisha misingi hii katika jamii yako.