ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 643
- 1,603
Ndugu watanzania wote kwa ujumla, kokote mlipo tunawasalimu kwa salamu inayo ashiria mabadiliko na uwazi.
Ndugu watanzania, miongoni mwa maswali ambayo watanzania walikuwa wameuliza kuhusiana na chama cha ACT-Tanzania, ni pamoja na kutaka kujua kwamba chama kilitumia kiasi gani cha fedha katika zoezi la usajili na uhakiki wa wanachama waanzilishi zaidi ya 2000, na mpaka sasa chama kimetumia kiasi gani cha fedha, kimebaki na kiasi gani cha fedha na kimepata wapi fedha hizo.
Swali hili kimsingi ni muhimu sana kwa kuwa linagusa moja kwa moja moja ya msingi mmojawapo mkubwa wa chama, yaani "msingi wa uwazi"; ambapo chama kinaamini kwamba ni lazima kifanye shughuli zake kwa uwazi wa hali ya juu.Vile vile chama kinatambua kuwa miongoni mwa maeneo yanayofaa kupimia uadilifu wa watu ni katika eneo hili la mapato na matumizi.
Kwa kuwa ACT-Tanzania inajipambanua katika misingi ya uwazi √
Kwa kuwa ACT-Tanzania ni chama cha siasa cha mfano nchini √
Kwa kuwa taasisi yoyote ya umma ina wajibu wa kuweka wazi mapato na matumizi yake kwa kuwa yanatokana na umma wenyewe √
Kwa kuwa wanachama wanajitahidi kuchangia chama kwa moyo safi pamoja na kuwa na kipato duni √
Na kwa kuwa ACT- Tanzania imekuja kumaliza mazingaombwe ya kisiasa nchini √
ACT- Tanzania inapenda kuwafahamisha watanzania wote kwamba, kwa kuanzia itakuwa ikitoa taarifa zake za mapato na matumizi kwa umma, kila baada ya kipindi cha robo mwaka (miezi mnne) kwa kuanzia.Chama kinatamani ikiwezekana kiwe kinatoa taarifa zake kila mwezi lakini kwa kipindi hiki cha kuanzia, hakitaweza kufanya hivyo kwa kuwa zoezi hilo linahitaji gharama kubwa na chama bado hakijawa na chanzo cha mapato cha kuaminika.Kama ambavyo watanzania wengi wamekishauri chama kuwa kila kinapotoa taarifa muhimu, kisitegemee mitandao ya kijamii pekee bali kutumia mbinu zote za mawasiliano ili kuwafikia watanzania wote, ni dhahiri kwamba zoezi hilo linahitaji gharama kidogo.
Chama kinawaomba watanzania wahesabu miezi minne toka chama kilipopata usajili wa kudumu na hapo wasipopata taarifa ya fedha, basi watakuwa na haki ya kuhoji.Ni jambo lisolokuwa na wasi wasi kwamba taarifa itakapotoka kila mtu atajua ACT-Tanzania inapata wapi mapato yake, imepata kiasi gani, imetumia kiasi gani, imetumia kwenye nini, na imebaki na nini.
Ni matumaini yetu kwamba kila mtanzania mzalendo atakuwa ametuelewa vyema.
Ikumbukwe kuwa ACT-Tanzania ni kwa ajili ya taifa letu leo na kesho!
Tuwasiliane kwa acttanzania@yahoo.com au acttanzania@gmail.com
Ndugu watanzania, miongoni mwa maswali ambayo watanzania walikuwa wameuliza kuhusiana na chama cha ACT-Tanzania, ni pamoja na kutaka kujua kwamba chama kilitumia kiasi gani cha fedha katika zoezi la usajili na uhakiki wa wanachama waanzilishi zaidi ya 2000, na mpaka sasa chama kimetumia kiasi gani cha fedha, kimebaki na kiasi gani cha fedha na kimepata wapi fedha hizo.
Swali hili kimsingi ni muhimu sana kwa kuwa linagusa moja kwa moja moja ya msingi mmojawapo mkubwa wa chama, yaani "msingi wa uwazi"; ambapo chama kinaamini kwamba ni lazima kifanye shughuli zake kwa uwazi wa hali ya juu.Vile vile chama kinatambua kuwa miongoni mwa maeneo yanayofaa kupimia uadilifu wa watu ni katika eneo hili la mapato na matumizi.
Kwa kuwa ACT-Tanzania inajipambanua katika misingi ya uwazi √
Kwa kuwa ACT-Tanzania ni chama cha siasa cha mfano nchini √
Kwa kuwa taasisi yoyote ya umma ina wajibu wa kuweka wazi mapato na matumizi yake kwa kuwa yanatokana na umma wenyewe √
Kwa kuwa wanachama wanajitahidi kuchangia chama kwa moyo safi pamoja na kuwa na kipato duni √
Na kwa kuwa ACT- Tanzania imekuja kumaliza mazingaombwe ya kisiasa nchini √
ACT- Tanzania inapenda kuwafahamisha watanzania wote kwamba, kwa kuanzia itakuwa ikitoa taarifa zake za mapato na matumizi kwa umma, kila baada ya kipindi cha robo mwaka (miezi mnne) kwa kuanzia.Chama kinatamani ikiwezekana kiwe kinatoa taarifa zake kila mwezi lakini kwa kipindi hiki cha kuanzia, hakitaweza kufanya hivyo kwa kuwa zoezi hilo linahitaji gharama kubwa na chama bado hakijawa na chanzo cha mapato cha kuaminika.Kama ambavyo watanzania wengi wamekishauri chama kuwa kila kinapotoa taarifa muhimu, kisitegemee mitandao ya kijamii pekee bali kutumia mbinu zote za mawasiliano ili kuwafikia watanzania wote, ni dhahiri kwamba zoezi hilo linahitaji gharama kidogo.
Chama kinawaomba watanzania wahesabu miezi minne toka chama kilipopata usajili wa kudumu na hapo wasipopata taarifa ya fedha, basi watakuwa na haki ya kuhoji.Ni jambo lisolokuwa na wasi wasi kwamba taarifa itakapotoka kila mtu atajua ACT-Tanzania inapata wapi mapato yake, imepata kiasi gani, imetumia kiasi gani, imetumia kwenye nini, na imebaki na nini.
Ni matumaini yetu kwamba kila mtanzania mzalendo atakuwa ametuelewa vyema.
Ikumbukwe kuwa ACT-Tanzania ni kwa ajili ya taifa letu leo na kesho!
Tuwasiliane kwa acttanzania@yahoo.com au acttanzania@gmail.com