Alinda
Platinum Member
- Jun 26, 2008
- 1,695
- 2,151
Mnachokosea nyie katika mjadala huu ni dhana au kufikiri kwamba pengine mimi ni mwanachama wa ACT ama naunga mkono kila wanalolifanya kina Zitto. Dada Alinda Unakosea sana, kwa sababu mimi nachoandika ni REALITY kama ninavyoiona mimi. Ndio maana nikasema ACT ni zao la CDM wenyewe, ACT yaweza kuwa mpini wa CCM lakini alouchonga mpini ni CDM, ndio maana nikamtetea Mwigamba, Kitila na Zitto walipofukuzwa CDM. Toka najiunga Jamii forums katika mijadala yetu miye hutazama Uhalisia zaidi ya Matumaini kwa sababu siwezi kuweka matumaini mahala ambapo Wadanganyika wenyewe ni wanafiki na vigeugeu..Nawatazama kwanza Wadanganyika wenyewe kisha naunganisha na wazo ama idea ilojitokeza..
Kitu pekee kinachoniweka mimi sawa na ACT ni Mrengo wao kaitka siasa za UJAMAA na kurudisha misingi tuliyoanza nayo katika ujenzi wa Taifa letu. Hawa matajiri iwe ni watu aa mataifa matajiri siku zote ni WANAFIKI na walaghai wakubwa wapo tayari kutumia fedha zao kutununua na kama fedha ikishindikana kuwanunua basi watatumia nguvu. Ndipo ujue hawakuwa na nia njema toka mwanzo.
Kwa hiyo nawatetea kina Zitto katika yale nayoyaona nia njema zile siasa za majitaka kwa sababu Zitto alifukuzwa CDM inakuwaje watu wanamfuata hadi alikokimbilia? Mkisha mfukuza mtu atoke nje ya nchi na akapanda pipa halafu bado unamfuata hadi huko aliko, inatupa shaka zaidi sisi tunaofuatilia siasa za Bongo..
Hoja iliyopo ni mapato na matumizi ya ACT (chama unachotetea katika mrengo wao) Wao walituahidi kuleta kila baada ya robo mwaka report ya mapato na matumizi ya chama chao.. Hivyo mimi mimi Alinda ambaye ni mtanzania ninayohaki ya kuhoji walichotuahidi. Na ndicho nilichofanya.
Nimekumention Wewe kwa ungwana tu kaka yangu kwani ulishawahi uliza lini na wapi ACT wazalendo walisema kuleta report ya mapato na matumizi..
Pia ni muhimu pale vyama vya siasa wanaposema jambo basi walitekeleza sasa kama wasipotekeleza jambo dogo kama ili tuawaaminije katika mambo makubwa?