ACT inavyoenda kupenya kati ya UKAWA na CCM

ACT inavyoenda kupenya kati ya UKAWA na CCM

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
Usiposumbua bongo waweza kudhani ACT kama chama chenye nia ya kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya mtanzania kimezaliwa katika wakati mbaya sana, naam katika wakati ambao vyama vikubwa na venye nguvu vya upinzani vikidhamiria kusimamisha mgombea mmoja katika ngazi zote na dhamira yao hiyo kuhitimishwa kwa makubaliano yaliyotiwa muhuri mbele ya wanaoitwa wafuasi na wanachama wa vyama hivyo katika viwanja vya jangwani.

Kwa wenye kusumbua bongo, wasiongozwa na ushabiki isipokuwa kweli, yaani werevu katu hawafikiri kama hichi chama kimezaliwa katika wakati mbaya, badala yake wataona kuwa chama hiki kimekuja katika wakati muafaka, wakati ambao kiukweli tunahitaji mbadala wa CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani na CCM kama chama tawala. Niko na sababu zifuatazo zilizonipelekea kuamini kuwa huu si wakati mbaya kwa ACT na ya kwamba kinakwenda kupenya kati ya CCM na UKAWA.

ofic ya cdm,,,.jpg

MOSI: FALSAFA NA ITIKADI YA ACT.
Falsafa na itikadi ya ACT vyote kwa pamoja vinajenga mahusiano ya moja kwa moja kati ya chama na wananchi wote bila kujali tafauti zao za umri, jinsia, kabila, dini, nk. Chama kimeundwa kwa kufuata misingi ya demokrasia jamii. Uzalendo, usawa, uadilifu, uwazi, uwajibikaji, demokrasia rasilimali, hifadhi ya jamii, utu, umoja wa Afrika na kujitegemea, weledi na bidii katika kazi ni misingi kumi ya ACT itakayo iwezesha chama hiki kupenya kati ya CCM na UKAWA.

Misingi hii ambayo inagusa maisha ya mtanzania wa mjini na kijijini haionekani au hautumiki katika vyama vinavyounda UKAWA na CCM. Kama ikienezwa vizuri na ikieleweka vijijini na mjini watanzania wataenda kuichagua ACT badala ya UKAWA au CCM kama inavyotegemewa. Huku ndio kupenya kwenyewe kwa ACT kati ya UKAWA na CCM.

arusha.jpg

PILI: HIVI WATANZANIA WANAHITAJI MUUNGANO TU WA UPINZANI?
Huku nikizingatia mashirikiano yaliokwisha kufanyika huko nyuma kwa vyama vyetu hivi vya upinzani, tangu mwaka 1995 kila chama kimekuwa kikipigana kivyake katika vita ya kuitoa CCM ikulu. Viongozi wa vyama vya CUF, CHADEMA na NCCR huenda wamejua kuwa watanzania wanataka kuona upinzani ulioungana, lakini wameshindwa kujua ni muungano upi wa upinzani ambao watanzania wanauhitaji.

Watanzania hawahitaji muungano wa vyama vya upinzani ambavyo tafauti yao na CCM ni majina tu. Wanahitaji muungano ambao ukipewa dhamana ya kusimamia rasilimali za nchi hii pamoja na katiba yetu ya nchi basi kutakuwa hakuna majuto kama ilivyo sasa chini ya CCM.

Hivi CUF itaishauri nini CHADEMA juu ya ung'ang'anizi wa kiti cha urais ikiwa Lipumba kila uchaguzi yeye ndiye huwa mwenyekiti wa CUF? Hivi Mbowe atamshauri nini Mbatia juu matumizi mabaya ya fedha za umma ukiwa CHADEMA mahesabu yake ni pasua kichwa? Hivi Mbatia atamshauri nini Slaa juu ubabe ikiwa yeye mwenyewe anaiongoza NCCR kama kampuni yake?

Vyama hivi ndio vinaunda huo UKAWA, na ndio vinajinasibisha na ukombozi ikiwa vitendo vyao havina tafauti na chama cha majambazi(CCM). Watanzania hawatakuwa tayari kuitoa CCM madarakani na kuingiza UKAWA, badala yake watakuwa radhi kuipa dola ACT na huko ndio kupenya kwenyewe.

Akihojiwa katika kipindi cha BARAGUMU chanell Ten katibu mkuu wetu alisema chama chetu kiko tayari kushirikiana na chama chochote ili mradi chama hicho kwa kiasi fulani kifanane na ACT katika itikadi na namna wa uendeshaji wa chama wenye kuzingatia uwajibikaji na uwazi. Kwa kauli hii na nikizingatia na uendeshwaji wa vyama vinavyounda UKAWA sitarajii hata kidogo kwa ACT kujiunga na UKAWA labda tu vyama hivyo vibadilike na kufanana na ACT. Kama havitabadilika ACT haina budi kupenya kati yao na CCM.
View attachment 197696

TATU: KUNING'INIA KWA CHADEMA.
Siasa za huku bara ziko tafauti kabisa na siasa za Zanzibar, tangu mfumo wa vyama vingi urudishwe CUF imeandelea kuwa chama kikuu cha upinzani upande wa Zanzibar wakati huku bara kofia hiyo imekuwa ikihama toka chama kimoja na kwenda kingine. Kwanini hivyo bara na kwanini hivyo Zanzibar? Si mada yangu kwa leo ila historia kwa upande wa Zanzibar ndio kila kitu.

NCCR ndio kilikuwa chama cha upinzani chenye nguvu huku bara tangu kilipoanzishwa na hata baada ya uchaguzi mkuu mwaka 1995(ingawa hakijawahi kuongoza bungeni), mwaka 2000 hadi tukielekea uchaguzi mwaka 2010 kofia hiyo ilikuwa inashikiliwa na CUF na kuanzia 2010 hadi sasa kofia hiyo inashikiliwa na CHADEMA.

wanachama.jpg

Kuna jambo hakuna mwenye kulibishia hapa kuwa kila kofia hii ilipohama ilikiacha chama iliyoishikilia kikiwa dhaifu katika mambo inayoyapigania, misimamo na kupungukiwa na idadi kubwa ya wanachama na wafuasi. NCCR ilipoishiwa nguvu huku bara pia ilipokonywa mashabiki na wanachama wake wengi, kimsingi ilianza kupokonywa mashabiki na wanachama na chama cha CUF kabla hata kupokonywa rasmi kofia ya chama kikubwa cha upinzani upande wa bara katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2000. Pia CUF ilianza kupokonywa mashabiki na wanachama wake na CHADEMA kabla ya chama hicho kupokonywa rasmi kofia ya chama kikuu cha upinzani mwaka 2010. Si wanachama na mashabiki wa kawaida vyama hivi vilikuwa vinapoteza lakini pia hata baadhi ya viongozi wake na wanachama waandamizi. Bahati mbaya watanzania wanaojishughulisha na ushabiki wa vyama ni walewale sababu ongezeko lao ni dogo sana. Hii ina maanisha nini?

Hii ina maanisha kuwa wanachama na mashabiki wa NCCR waliokipa nguvu chama hicho mwaka 1995, ndio hao hao walioipa nguvu CUF mwaka 2000, ndio hao hao walioipa nguvu CHADEMA mwaka 2010 na ndio hao hao baadhi yao waliomua kuanzisha na kujiunga ACT.

Mbishi pekee atakayekataa kuwa uanzishwaji wa ACT na kupata usajili wa kudumu wa chama hicho mara baada ya kudhaminiwa na wanachama zaidi ya 200 katika mikoa 18 ya bara na visiwani unatokana na nguvu ya asili ya NCCR. Wanachama wengi wa ACT hawakutoka kwa wananchi ambao hawakuwa na chama au hawakuwa mashabiki wa chama, wanachama wengi wa ACT wengi wao walikuwa wanachama wa CHADEMA, CUF na ADC. Waliokuwa viongozi wa CHADEMA katika mikoa mbalimbali wamejiunga na ACT na kundi kubwa la wanachama na mashabiki wa chama hicho, vivyo hivyo kwa CUF na ADC.

CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kilikuwa kinaituhumu CUF kuwa kibaraka wa CCM, lakini mara baada ya kuona chama hicho kinapoteza mvuto na wanachama wake na kinaendea kupoteza kofia yake, kikaona njia pekee ya kuendelea kubaki katika chati ni kuiangukia CUF na NCCR, kwa hivyo ajenda ya katiba ilikuwa njia tu kufikia lengo hilo la CHADEMA. Pamoja na hayo, nikiangalia nguvu ya CUF na NCCR, kwa vyovyote vile kuning'inia kwa CHADEMA ndio kuning'inia kwa UKAWA, na huko ndio kupenya kwa ACT kati ya UKAWA na CCM.

Hatuwezi kuukwepa ukweli kuwa NCCR na CUF vimejitahidi kurudisha hadhi yao vimeshindwa, CHADEMA imestuka kuwa inaenda kupoteza hadhi yake kwa ACT mara baada ya wanachama na waliokuwa viongozi wake kujiunga na ACT, hivi yenyewe CHADEMA inategemea muujiza wa UKAWA kuwa itapona ugonjwa unaowasumbua hata sasa CUF na NCCR? Thubutu labda viongozi walioipaisha na sasa kuishusha CHADEMA watoke katika ofisi za Ufipa, na si hivyo tu hata ile tabia iliyoifikisha CHADEMA katika anguko hili ikomeshwe, kinyume chake ACT inakwenda kukalia kiti cha CHADEMA na huko ndio kupenya kwa ACT kati ya UKAWA na CCM.

View attachment 197697

NNE: MASHABIKI SI WANACHAMA WA CHADEMA.
Vyama vyote vya upinzani isipokuwa ACT havina wanachama zaidi ya mashabiki, na hii ndio sababu iliyopelekea NCCR, CUF na sasa CHADEMA kupoteza nguvu. Vyama hivi vina mashabiki wa wanasiasa au mashabiki wa matukio ya kisiasa. NCCR ilikuwa na mashabiki wa Mrema na ajenda ya kuitoa CCM madarakani, CUF imepata nguvu kutokana na msimamo dhidi ya muundo wa muungano, CHADEMA imepata nguvu kutokana na matukio ya Buzwagi, EPA na Richmond, na UKAWA inapata nguvu hizi kutokana na ajenda ya KATIBA. Mashabiki wa ajenda ya KATIBA wataachana na UKAWA endapo likitokea ajenda nyingine kubwa au itakayowavutia kuliko hata ya KATIBA au suala la KATIBA likifikia mwisho huku mashabiki wa ajenda hiyo wakiwa wameridhika. Ikiwa CUF, NCCR na CHADEMA zimepoteza mvuto sababu ya kuhama kwa washabikiwa au kupoteza mvuto kwa ajenda zilizokuwa zinashabikiwa, UKAWA itawezaje kukwepa mtego huo?

Ndio maana ACT tunajikita katika kuzitangaza na kutoa elimu juu ya uzuri na manufaa ya itikadi yetu ya mrengo wa kati kushoto na falsafa yetu ya unyerere na ile misingi yetu kumi. Tunataka watanzania waikaribishe ACT katika nyumba zao kwasababu ya uzuri na manufaa ya itikadi, falasafa na misingi kumi ya ACT. Chama kitashughulikia matukio ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa kuongozwa na itikadi, falasafa na misingi kumi ya ACT.

Kwa kufanya hivyo tutakuwa na wanachama wa ACT na si mashabiki wa watu na matukio, na chama hakitayumba hata kidogo sababu ya kiongozi kutishia kujitoa au kujitoa kama ilivyo sasa kwa CHADEMA kinavyoyumbishwa kutokana na sakata la Mwigamba, Prof Kitila na Zitto. UKAWA wana mashabiki wa matukio na watu lakini ACT ina wanachama na mashabiki wa chama, na huku ndio kupenya kwa ACT kati ya UKAWA na CCM.

View attachment 197698

TANO: UBEPARI, UJAMAA NA ULIBERALI.
Tupozungumzia UKAWA katu huwezi kuepuka kuona mchanganyiko huo wa kiitikadi; ubapari wa CHADEMA, ujamaa wa NCCR na uliberali wa CUF. Vyama hivi kila kimoja kimeshindwa kujenga itikadi zao hizi kwa wanachama na mashabiki wao, hivi huo mseto wanakwenda kufafanua vipi hata waeleke kwa watazania kama si kujichanganya na kupoteza dira?

Wakati UKAWA wakivurugana juu ya misingi ya itikadi gani waisimamie na kutoka nayo mbele ya umma yenyewe ACT itakuwa inaendelea kutangaza misingi yake kumi inayozingatia misingi ya demokrasia jamii. Hivyo ACT inaenda kueleweka kwa haraka zaidi kuliko UKAWA, na huku ndio kupenya kwa ACT kati ya UKAWA na CCM.

kiongoz.jpg

SITA: WATANZANIA WAMECHOKA NA CCM, LAKINI HAWANA HILA.
Kuendelea kwa CCM kupewa ridhaa ya kuongoza dola na ushindi wa chama hicho katika chaguzi ndogo hakumaanishi kuwa watanzania bado wanaipenda CCM, ufisadi na kulewa madaraka kwa CCM kuna julikana vizuri kwa watanzania. Pamoja na kujulikana huko lakini bado wanaendelea kuichagua, hivi waache kuichagua CCM waichague CHADEMA ambayo kabla haijakabidhiwa dola imeshaanza kupata hati chafu? Hivi waichague CUF ambayo mwenyekiti wake ni mfalme? Kuchaguliwa kwa CCM ni kuthibiti kwa msemo wa ZIMWI likujualo halikuli likakwisha.

Vyama vinavyounda UKAWA na vyama vyote vya upinzani tulivyovikuta vimeshindwa kuonesha kwa vitendo ni kwa namna gani vitakuwa tafauti na CCM pindi vikipewa dola, badala yake vinaonekana vitakuja kufanya maovu makubwa kuizidi hata CCM. Watanzania walikuwa wanatafuta chama cha kuitoa CCM madarakani na sasa wameshakipata, na hivi ndivyo ACT inavyokwenda kupenya kati ya UKAWA na CCM.

ACT-TANZANIA ==========> TAIFA KWANZA.
UWAZI NA MABADILIKO ===> CHUKUA HATUA


Njano5.
0784845394.
 
Nyie mmefulia, hata mlete ma thread marefu kiasi gani hatuna mpango wa kuyasoma. Juzi maazimio yenu yamedoda mkakosa wachangiaji, rudini Facebook na twitter huko ndio mtapata mburulaz kibao.

Kujenga Chama kikakubalika nchi nzima sio kazi rahisi kama kuvua migebuka. Msione Halima Mdee ameiteka Kanda ya ziwa mkadhani bahati mbaya, watu wamejenga chama.
 
Pole sana ndugu naona unataka kuwarudisha watanzania nyuma tena kwa hatua 200,000. Wenzio wanasonga mbele. Umepoteza muda wako mwingi kukifagilia hicho chama chako mfu ACT lakini kwa sasa UKAWA ndio habari ya mjini.
 
Matokeo ya kupenya katikati ni mimba "Chotara." Hamjijui mnasimamia upande gani.
 
Waacheni tu watanzania wasonge mbele na harakati za ukombozi, hiyo ACT yenu ipo nyuma sana ya wakati. Watanzania hawataki kurudi nyuma tena!
 
watanzania wataenda kuichagua ACT badala ya UKAWA au CCM kama inavyotegemewa. Huku ndio kupenya kwenyewe kwa ACT kati ya UKAWA na CCM.
Njano5.
0784845394.
Mtandao wa ushindi utakuwa kama ifuatavyo. Kwenye ngazi ya kitaifa tutakuwa na kamati yenye members watatu tu. M1 ndiye atakayekuwa anawasiliana na tunayemtaka ambaye ataitwa MM (Mhusika Mkuu). Tumepanga kwamba kusiwe na mawasiliano mengi kati ya kamati na mhusika mkuu kuepuka tracking ya wapinzani wetu. M1 ni mtu wa karibu na MM kwa hiyo mawasiliano yao hayataweza kutiliwa shaka na mtu yeyote hata wangewasiliana mara nyingi kiasi gani. Hata hivyo, linapokuja suala la mkakati huu tunasihi mawasiliano yawe kwa kuonana uso kwa uso ama kwa simu na si sms. M1 ndiye atakayewasilisha mambo yote yanayotoka kwenye kamati ya kitaifa na endapo kuna haja ya MM kukutana na kamati ya kitaifa, mipango yote ya kikao itafanywa na M1 kwa usiri mkubwa. M2 ni mtu ambaye yuko kwenye ofisi kuu za taasisi yetu wakati M3 ndiye mchapaji wa mkakati huu.

Kamati hii imefanywa kuwa na members wachache sana wenye uelewa mpana wa mambo na wenye elimu nzuri ili kuhakikisha kazi inafanyika kitaalam na kwa uhakika sana. Kamati ya kitaifa itapeleka mapendekezo yake kwaMM na yeye pia ataleta ushauri wake kwa kamati kama mishale inavyoonyesha. Chini ya kamati ya kitaifa kutakuwepo waratibu wa kanda zote kumi watakaojulikana kama MK1 – MK10. Hawa watatafutwa na kusimikwa na kamati ya kitaifa kwa kushauriana na MM kwa utaratibu utakaokubalika na pande zote yaani MM na kamati ya kitaifa. Chini ya waratibu wa kanda kutakuwapo waratibu wa mikoa yote 30 (MMK1 – MMK30) ambao watapatikana kwa utaratibu ule ule wa kuwapata waratibu wa kanda. Isipokuwa pale ambapo inakuwa ngumu, itabidi kamati ya taifa isaidiane na waratibu wa kanda kuwapata waratibu wa mikoa lakini kamati itashauriana na MM kabla ya kuwasimika rasmi hao waratibu wa mikoa.Mtandao utakuwa kama inavyoonyeshwa kwenye mchoro ufuatao:

 

hichi chama kimezaliwa katika wakati mbaya, chama hiki kimekuja katika wakati muafaka, wakati ambao kiukweli tunahitaji mbadala wa CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani na CCM kama chama tawala. huu si wakati mbaya kwa ACT na ya kwamba kinakwenda kupenya kati ya CCM na UKAWA.
Njano5.
0784845394.

ACT a.k.a SACCOSS ya Zitto kiwe chama kikuu cha upinzani na kikwazo cha CHADEMA au UKAWA kuingia IKULU!
 
Umenena Jambazi Rangimoto. Rudisha pesa zetu za CHADEMA mitandaoni ulizokula kabla ya kuhamia Alliance for Cowards and Traitors-Tanzania.
 
Dotto C. Rangimoto

Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100 kwamba watanzania hawahitaji muungano wa upinzani tu na NDIO MAANA ACT IMEAMUA KUUNGANA NA CCM ili kuvunja nguvu za upinzani. ACT chama cha mapesa ya MAFISADI
 
Last edited by a moderator:
Mwanzo sikuwaelewa vizuri ACT lkn kiukweli kwa mwenendo Wa chadema katika uadilifu wametuangusha vyakutosha,yaani chadema ikiwa haijapata dola wanaambulia hati chafu kwenye mahesabu haliyakuwa walifahamu fika kuwa watakaguliwa?

Nikirejea kwenye huu uzi,umejitahidi saana kuonyesha jinsi ACT itakavyopenya kimkakati,name kqa siasa za Tanzania sitashangaa kuona ACT kinakuwa chama Kikuyu cha upinzani muhimu tu nikujiepusha name madudu yaliyofanywa na watangulizi Wei(CUF name CHADEMA)

Act ifanye siasa za Agenda,siasa za kujenga hoja,siasa za kutoa elimu ya Urania name siasa zilizojikita vijijini ambako wengi wamepigika.

Karibuni ACT mtukomboe wanyonge.
 
mheshimiwa sana Dotto C. Rangimoto, hata shetani naye huwaga ana maneno matamu hivi hivi, pengine kuliko hata malaika!

wakati ndani ya CCM tayari vimezaliwa vyama vidogo vidogo kadhaa(chama Lowasa, chama Membe, chama Pinda, chama Sitta, chama January, nk,nk), wapinzani wanajipanga kwenye "chama" kubwa UKAWA. haihitajiki shahada hapo kujua kitakachotokea.

come again...ACT who??
 
Ushauri wabure kwa wote msiopenda kusoma kabla ya ku comment ,uzi huu ni muhimu saaana kwa mustakabali wa siasa zetu hasa tunapokwenda 2015,

Upinzani wametukatisha tamaa hasa baada ya kufanya vitendo visivyomithilika.

Mfano mzuri ni tabia ya kujifanya mawinyi na wasiokosoleka.

Mbaya zaidi ni ile tabia ya Chadema kuchakachua katiba yake wenyewe ili kuwabakisha watwana madarakani.

Hii inawatia shaka wananchi kuqa hata wakiingia madarakani qatafanya hivyohivyo kwa katiba ya nchi kama ilivyo kwa Rais wa Bukinafaso ambae leo tumeshuhudia Bunge likichomwa moto.

ACT mnapaswa kuwa makini kwa kila hatua moja mtakayipiga,mnaadui wengi ,na wote ni kuhakikiaha chama hakikui na kinarudia makosa kama yaliyokwisha fanywa na watangulizi wenu.
 
Pole sana ndugu naona unataka kuwarudisha watanzania nyuma tena kwa hatua 200,000. Wenzio wanasonga mbele. Umepoteza muda wako mwingi kukifagilia hicho chama chako mfu ACT lakini kwa sasa UKAWA ndio habari ya mjini.

hakuna kurudi nyuma mkuu, bali hapa tunachukua hatua stahiki dhidi ya CCM na mawakala wao.
 
Chama cha mtandaoni. Rudini kwenye drawing board. Hamuwezi kufanikiwa kwa kuunda chama cha upinzani chenye sera za kupinga vyama vingine vya upinzani.
 
Back
Top Bottom