Acheni Mchezo na UKIMWI

GOOGLE X

New Member
Dec 1, 2019
1
42
Kuna jamaa alikuwa rafiki yangu wakati nipo chuo miaka kadhaa iliyopita. Sasa kuna siku alilala na msichana bila kupima. Baada ya kumaliza ngono akawa amemsisitiza akapime baada ya mwezi halafu amtumie majibu, msichana akamwambia sawa.

Kama mwezi mmoja hivi kupita jamaa alimkumbusha msichana kwenda kupima. Siku moja tumekaa chini ya mdigrii kwenye Vimbweta pale UDSM, kuna ujumbe wa simu ukaingia kwenye simu yake kutoka kwa yule msichana, ambao baadaye niliusoma, ulisomeka hivi:

"Hello, nimeenda angaza kupima nikapewa majibu ya kutatanisha, nimeambiwa nirudi baada ya miezi 3, hapa nilipo nimechanganyikiwa".

Baada ya jamaa kusoma ujumbe alianza kama vile kuweweseka, anajinyosha, anasimama, anakaa, anazungukazunguka huku na kule na kurudi huku akiwa ameinamisha kichwa.

Muda kiasi wa ukimya ulipita, halafu akaniuliza, hivi kama mtu ameambukizwa ukimwi mwezi mmoja uliopita, akipima leo inaweza kuonekana kama ameambukizwa au lah?

Nikamjibu, UKIMWI hauna maana kabisa, mtu aliyeambukizwa juzi usiku anaweza kukuambukiza wewe leo, lakini akipima hata baada ya miezi 3 inaweza kusoma negative, pia anaweza kupima akaonekana hana hata baada ya mwaka. Wewe uliyeambukizwa inategemea sababu mbalimbali, unaweza kupima hata baada ya miezi sita ikaonekana huna, na baada ya mwaka au miaka hata 2 na zaidi ukajitokeza.

Alichukua makabrasha yake akaondoka kimyakimya bila kuniaga huku akiwa anatembea kwa kupepesuka kama mlevi.

Niliporudi Hostel pale Mabibo nikamkuta room amelala na viatu kitandani, ndipo nikachukua simu yake kimyakimya na kusoma sms zilizonipa tukio zima kati yake na yule msichana.

Kusema ukweli, jamaa alianza kuishi kama mwehu kadri siku zilivyoenda. Baada ya siku tatu nilihama maana nilihisi angeweza kunidhuru au hata kunichanja na wembe aliojikata ili kama ana UKIMWI aniambukize na mimi.

 
Nshapiga saaana madem wa chuo na kazini ila jf sithubutu na sina ngoma hadi wa fields au HR
 
Sasa mkuu, hata kama wewe umepata kinachotakiwa si kwenda angaza wanakotoa ushauri nasaha? Sasa unataka nivamie fani za watu?
EPUKA NAYE KABISA
MIJITU INAJITAKIA kutokuvaa Condom na haitaki kusubiri Ndoa au kupimwa eti ukae nae kumshauri
nakushauri hata usijihusishe naye kuna mwenzetu kajinyonga leo huko Magomeni kwa member Mwanaidi wa JF, p/se NDEGE MJANJA HUKIMBIZA BAWA LAKE
 
Angaza wapo wanasubiri wateja, halafu unataka nibebe jukumu lao?


Wewe hujaambiwa ufanye kazi ya Angaza, ulitakiwa uumpe ushauri huyo rafiki yako juu ya nini cha kufanya, mfano ungemshauri aende huko Angaza (baada ya kuthibitika kwamba yeye ni muathirika), cha ajabu ulimtosa kana kwamba wewe ni "immune" kwa huo ugonjwa au huna jamaa au ndugu ambaye aliwahi kuathirika au wewe huwezi kuupata katika njia zingine mbali na ngono kiasi kwamba huyo rafiki yako awe ni mlaumiwa na mbezwaji (contempted) katika hiyo hali. Ukimwi upo kwa ajili ya wanadamu, tofauti ni njia ipi mtu anaweza kuambukizwa, unaweza kuambukizwa kupitia blood transfusion nk,

"A friend in needy is a friend indeed"
 
Mlikutana betri na tochi. Elimu ya Ukimwi zero kabisa yet you're waiting to graduate
 
Mkuu, usitoe ushauri kama hujaulizwa. Angaza tayari alikuwa anaijua, sasa ningeshauri nini? Soma uone alivyoniuliza maswali kuhusu kupima. Bora mimi ambaye sikumshauri kama unavyotaka, kuna jamaa alimwambia, kama umeukwaa ukivuka miaka 2 shukuru!


Bila shaka huyo hakuwa rafiki yako. Full stop.
 
Ivi Virusi vinaishi kwenye Damu Pekeake au any kind of Maji maji yatokayo mwilini? (e.g Semen,Vaginal fluid etc)... maana sielew wapo wanao sema ni damuni wengine wanasema kote kote
 
Malizia hiyo stoty, walienda kupima wote? Na nn matokeo kwa wote kwa pamoja!!
 
Huyo naye hana akili ukimwi sio wa kuuwazia kabisa ndio maana wenyewe wanakuambia ukitimiza masharti utaishi long bila shida.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom