Nimesikitishwa sana na kitendo nilichofanyiwa na hawa jamaa wa Access Bank.
Mnanamo mwezi wa kumi na moja mwaka jana nilienda Access Bank kwaajili ya kufungua Account ya Kampuni, nilipofika niliwaona wahusika na wakanipatia taratibu zao za kufuata kwaajili ya kukamilisha zoezi la kufungua Account.
Nami niliwaletea nyaraka zote walizozihitaji ktk mchakato mzima.Baada ya kukabidhi nyaraka hizo niliambiwa nisubiri baada ya siku tatu nitajulishwa.Baada ya siku tatu nilienda nikaambiwa kuwa nisubiri kidogo kwani nyaraka zangu zimepelekwa BRELA kwaajili ya uhakiki km kweli kampuni imesajiriwa.Jamaa akaniambia kuwa nitapigiwa simu wakati wowote pindi mambo yakiwa tayari.
Jambo la ajabu nimesubiri kwa muda mrefu bila majibu duh nikaamua kwenda Internataional Commercial Bank kuanza zoezi jipya la kufungua Account, nimetumia km wiki mbili hivi Account ikawa imefunguliwa.Sasa nikabaki na maswali lukuki iweje hawa watumie wiki mbili tu kufungua Account ili hali Access Bank sasa ni miezi mitano bila jibu lolote!?.
Ndipo nikaamua kurudi tena Access Bank, mhusika nikamuliza kwanini zoezi hili limechukua mda mrefu namna hii?, ili hali ICB wametumia wiki mbili tu?.jamaa akaniambia kuwa tatizo ni BRELA kwani mafairi yote yamekwisha pelekwa huko, lakini kila wakifuatiliwa wanaambiwa mafairi hayaonekani, wakati mwingine wanaabiwa njoo kesho bado tunatafuta mafairi.Pia akanitanabahisha kuwa ktk kila Bank kunatofauti wa kushughurika mambo eti kuna baadhi ya Bank wanatoa kitu kidogo kwa jamaa wa BRELA ili kurahisisha mambo.duh TZ kila kitu ni rushwa hata kufungua Account mnaomba rushwa.Duh kumbe ndo maana watu wa ICB waniliambia nitoe Tsh 15000/= ya kurahisisha mambo kule BRELA. duh watu wa BRELA acheni mambo hayo jamani munaturudisha nyuma kimaendeleo.
Mnanamo mwezi wa kumi na moja mwaka jana nilienda Access Bank kwaajili ya kufungua Account ya Kampuni, nilipofika niliwaona wahusika na wakanipatia taratibu zao za kufuata kwaajili ya kukamilisha zoezi la kufungua Account.
Nami niliwaletea nyaraka zote walizozihitaji ktk mchakato mzima.Baada ya kukabidhi nyaraka hizo niliambiwa nisubiri baada ya siku tatu nitajulishwa.Baada ya siku tatu nilienda nikaambiwa kuwa nisubiri kidogo kwani nyaraka zangu zimepelekwa BRELA kwaajili ya uhakiki km kweli kampuni imesajiriwa.Jamaa akaniambia kuwa nitapigiwa simu wakati wowote pindi mambo yakiwa tayari.
Jambo la ajabu nimesubiri kwa muda mrefu bila majibu duh nikaamua kwenda Internataional Commercial Bank kuanza zoezi jipya la kufungua Account, nimetumia km wiki mbili hivi Account ikawa imefunguliwa.Sasa nikabaki na maswali lukuki iweje hawa watumie wiki mbili tu kufungua Account ili hali Access Bank sasa ni miezi mitano bila jibu lolote!?.
Ndipo nikaamua kurudi tena Access Bank, mhusika nikamuliza kwanini zoezi hili limechukua mda mrefu namna hii?, ili hali ICB wametumia wiki mbili tu?.jamaa akaniambia kuwa tatizo ni BRELA kwani mafairi yote yamekwisha pelekwa huko, lakini kila wakifuatiliwa wanaambiwa mafairi hayaonekani, wakati mwingine wanaabiwa njoo kesho bado tunatafuta mafairi.Pia akanitanabahisha kuwa ktk kila Bank kunatofauti wa kushughurika mambo eti kuna baadhi ya Bank wanatoa kitu kidogo kwa jamaa wa BRELA ili kurahisisha mambo.duh TZ kila kitu ni rushwa hata kufungua Account mnaomba rushwa.Duh kumbe ndo maana watu wa ICB waniliambia nitoe Tsh 15000/= ya kurahisisha mambo kule BRELA. duh watu wa BRELA acheni mambo hayo jamani munaturudisha nyuma kimaendeleo.