Hakuna ubishi CV ya Mh. Migiro siyo ya kitoto. Ukiachilia mbali kuwa ni msomi wa PhD, pia first class ya UDSM nayo sio kitu kirahisi. Nakumbuka Prof. Lipumba kuna wakati alikuwa akijisifu kuwa alipata first class ya uchumi pale UDSM.
Kwahiyo ni wazi kuwa CCM wana katibu mkuu bora kulinganisha na CHADEMA, angalau kwa hivi vigezo vya elimu na uzoefu wa uongozi kitaifa na kimataifa.
..unaamini Dr.Migiro anaweza kuwa Katibu Mkuu wa Chadema na akaimudu hiyo nafasi kama alivyoweza John Mnyika?
..Dr.Migiro ni mhadhiri na mkufunzi mahiri wa sheria, lakini sio mwanasiasa mzuri. Kwenye siasa ameteuliwa kutokana na vyeti, lakini ni nafasi ambazo zinahitaji mtu mwenye wito, na kipaji.