Godlisten Masawe
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 738
- 283
Jamii Forum ni kiboko sana.
Kuna wadau walisema wiki tatu zilizopita kuwa huyu Kibanda anakwenda kuajiriwa Habari Cooperation, hivyo zile makala zake za kumsifia Kinana na kuwaponda Chadema zilikuwa ni chokochoko za kuanzisha bifu na mwajiri wake(Mbowe) ili aondoke kwa visa, lakini watu walimwangilia tu na sasa kaamua kuvaa magamba wazi.
Nchi yetu hii tamu kweli kweli! Nataka nione zile makala motomoto za kuichachafya serikali na CCM zikitoka kwenye magazeti ya New Habari!
Ndugu Mwita Maranya yametia yaliyonenwa na manabii
Aliyekuwa mhariri mtendaji wa gazeti la Tanzania Daima Absalom Kibanda, leo ameaga rasmi na kuachia nafasi yake mhariri mtendaji, kwa maelezo kuwa anaenda kujiunga na kampuni ya New Habari Corporation 2006, inayochapisha zaidi ya magazeti manne hapa nchini.
Akiongea na wafanyakazi wa gazeti la Tanzania Daima leo asubuhi, kibanda alisema sababu kubwa ya kuondoka hapo ni kwa ajili ya kutafuta changamoto mpya katika majukumu yake ya uandishi.
Amewataka waandishi wa gazeti wanaobakia waendelee kufanya kazi kwa bidii, kwa ajili ya kulikomboa taifa kwa kuuanika ukweli pasipo kuogopa,
Hawawezi mkuu labda iwe ni mkakati wa kambi yao.Pengine mkakati wa kumshughulikia Mbunge wa mtama na kiongozi ajaye wa upinzani (baada ya uchaguzi mkuu 2015)Sasa huko alikoenda kuna changamoto gani?
Mkuu Yericko,
huu ndiyo unafiki wa hawa watu.Lakini katika safari ya mabadiliko ni lazima tupate moyo hasa tunapoona kasi ya usaliti inaongezeka.Kama mimi kadiri ninaposalitiwa ndivyo kasi yangu na ari ya kupambana inapokua juu.Let us move on comrade!
Atakuwa kama Tambwe akiwa NCCR then KAFU leo bado anasema tu Ubaya wa wapinzani so Kibanda kaanzaKweli kazi ya uandishi wa habari Tanzania haina tofauti na uuza baa. Jamani Kibanda kama aliyokuwa akiandika yalikuwa yanatoka moyoni, huko ataandika nini au ni wale wale akina Salva Rweyemamu. Kweli namna hii hatuwezi kuendeleza nchi yetu. Yaani kila mtu anapigwa bei kienyeji hivi hivi.
Kibanda ni mchumia tumbo siku nyingi hivo sishangai kama anaweza kuacha jukumu zito alilokuwa amejitwika kwa manufaa ya wengi na kwenda kuliko na maslahi zaidi!
Aje tena hapa akane kutumika kuichafua CDM.By the way tunamtakia kila la kheri.
Kamata jahazi Ansbert Ngurumo