Twilumba
JF-Expert Member
- Dec 5, 2010
- 11,540
- 12,398
MZIMU wa ajali unaendelea kuisumbua kampuni ya mabasi ya Abood! Mchana wa leo basi lake lingine limepata ajali eneo la Mtego wa Simba, nje kidogo ya mji wa morogoro. Basi hilo, lenye namba za usajili T453 AES, lilikuwa likitoka Morogoro kuelekea jijini Dar es salaam. Limegonga kwa nyuma Trekta aina ya Masey Ferguson (pichaji juu) lenye namba za usajili T 583 ALK, na baade kumgonga mzee mmoja laiyekuwa akiendesha baiskeli akitoka kuchota maji kisimani. Katika ajli hiyo hakuna mtu aliyekufa lakini hali ya dereva wa trekta na yule wa baiskeli, zimeelezwa kuwa ni mbaya sana na wako hospitalini.
Source: Dastan Shekidele, Morogoro
Source: Dastan Shekidele, Morogoro