Kuna mahali tutakuwa tunakosea sana. Kama kuna kuna hoja na iwekwe wazi ijadiliwe, lakini hili suala la eti 'wageni', na nini sijui, halitawajenga zaidi ya kuzidi kuwagaweni.
Naona ni mwanzo wa kufungua milango ya kubaguana, kuna watu watadai wanaostahili zaidi chamani ni wanachama waishio nchini kuliko waishio nje ya nchi. Itafika mahali kabla ya kugombea uongezi mtadai ili kukidhi vigezo lazima uonyesho ngeu au jeraha mwilini mwako ulilolipata katika harakati za 'kukipigania' chama au ulete ushahidi wa mtu wako wa karibu aliyeuawa katika harakati hizi. Kufikia hapo tayari mnakuwa mmeshasahau objective yenu ya kimsingi kwa sababu ya madaraka.
Misimamo mingine ni upofu tu kuendelea kuing'ang'ania, the true meaning of victory has hidden in the truth that, 'sometimes the better way to win is to loose'.
Nisiwachoshe bwana maana waingereza wana kamsemo kao kanasema "behavior is comfort zone". Hivyo basi maamuzi ni yenu, 'mfe mkiwa maadui au mshinde mkiwa mmeungana'.
Msitusumbue sisi na hiyo misimamo isiyoeleweka unless kuna ukweli mnatuficha.