SIFA ZA DALALI WA UPATANISHO ALIYE MKWELI
Rais Martti Ahtisaari - Ili Ufanikiwe Katika Upatanishi wa Amani unapaswa kuwa Dalali Mwaminifu
19 November 2025
Deus Kibamba - Uchunguzi wa Kisanyasi Unatakiwa Badala Uchungizi uliogubikwa na Siasa
View: https://m.youtube.com/watch?v=wegx-qz6k7o
Uchunguzi wa Kisayansi ndiyo uponyaji utapatikana kwa taifa na mioyo ya raia
Walioteuliwa katika Tume kama wajumbe, wajipime kama wanatosha na kukubalika na umma mpana.
Kama baadhi ya wajumbe hao wanajiona hawatoshi, wajiuzulu ili TUME hii ibaki na heshima ya kukubalika
Watu wengi hawajulikani wapo wapi, haijulikani kama wapo mahabusu, kizuizini au nini kimewakumba hadi hatuwaoni
Nina vijana nilifundisha lakini kwa sasa sijawaona na sijui wapo wapi
Umuhimu wa Jopo Huru lilisolipwa na mkuu wa nchi au serikali yake ni mkubwa sana, na utaipa serikali ya Tanzania heshima kuondokana na doa alilolitaja mkuu wa nchi kule Bungeni Dodoma
Tusizuie majopo ya Huru, tukiwazuia wanaotaka kutuma Jopo Huru itaipa serikali na nchi wakati mgumu
Hakuna ubaya wa kuwa na majopo ya ndani na nje ya nchi pia tusijaribu kuyazuia
Dr. Lazarus Chakwera na Jopo lake litakuwa rapport building yaani wadau mbalimbali kufahamiana na kuaminiana. Hivyo Dr. Chakwera na Jopo lake linakuja kwa ajili ya rapport ila wataalamu wa uchunguzi wa kisayansi watakuja baada ya wadau wote ikiwemo serikali kukubaliana na yale yanayopigiwa kelele ikiwemo ruhusa ya kuongea kwa uhuru ..
Jeuri, ngebe, uhafidhina havitakiwi ikiwa kweli tunataka kutoka sababu zilizosababisha Oktoba 29, 2025 maandamano kutokea baada ya nafasi zote za kudai haki iwe mahakamani, mchakato wa uchaguzi, kutekwa, kukamatwa bila kufikikishwa kituo cha polisi, taratibu za ukamataji, sheria kandamizi kama hii ya uundwaji Jopo la Uchunguzi ya 2023 n.k
Rais anatakiwa kushinda kiti ch urais kwa asilimia 50 + kura 1 badala sheria ya sasa ambapo rais anaweza kuchaguliwa kwa asilimia 10 ya watu milioni 70.