A Mexican is twice richer than Tanzania

Sijarudia upotoshaji.

Nimesema



Elewa tofauti ya Net worth na GDP.Hii ni point muhimu sana.

Huyu Slim hela zake zote ndiyo hizo bilioni hamsini na kitu, hizo ni hela / mali zake zote.

Tanzania GDP yetu (uzalishaji wa nchi kwa mwaka mmoja tu) ndiyo takribani nusu yake.

Sasa kusema Slim ni tajiri mara mbili ya Tanzania ni sawasawa tuchukue mali zako zote, tuseme dola milioni moja, halafu tuzilinganishe na mshahara wangu wa mwaka mmoja, dola laki tano, halafu tukasema wewe ni tajiri mara mbili yangu. Wakati wewe umetumia miaka 60 kupata dola milioni moja na mimi nimepata dola laki tano katika mwaka mmoja tu.

Lakini kwa kuelewa kwamba Slim ni mtu mmoja, nikaona kurekebisha facts huku kusichukuliwe kama niko complacent na umasikini wetu.

Kwa sababu hata kama habari ingekuwa kwamba kuna Mmexico huko ana mihela na mali alizo accumulate maisha yake yote ambazo zina net worth iliyo twice our GDP, bado ni habari mbaya.

Kwa hiyo hamna contradiction wala upotoshaji hapo.

Si kweli kwamba Slim ni twice as rich as Tanzania kama nilivyofafanua katika hiyo posti ndefu hapo juu.

Lakini ukweli huu usitufumbe macho tukaona sawa mtu mmoja kuwa na net worth iliyo twice our GDP. Ukitaka kuudharau ukweli huu just because perspective inayoongelewa haijacompare GDP kwa GDP au net worth kwa net worth, wewe ndiye utakuwa unapotosha.

Umenena kweli kabisa kaka, ila naomba kuuliza swali ingawa naandika kwenye giza UMEME hamna hapa natumia simu ya mkononi.

Je ARDHI ya Tanzania ina thamani gani?
Maziwa ya maji (lakes) Mlima Kilimanjaro na fukwe za bahari zina thamani gani?

Kitu kinakua na thamani kama kinaweza kuzalisha au kuleta faida, kama hakiwezi basi hakina THAMANI.

Yap, Networthy na GDP ni sawa na kulinganisha pilipili na machungwa, hapo tupo pamoja.
 
Umenena kweli kabisa kaka, ila naomba kuuliza swali ingawa naandika kwenye giza UMEME hamna hapa natumia simu ya mkononi.

Je ARDHI ya Tanzania ina thamani gani?
Maziwa ya maji (lakes) Mlima Kilimanjaro na fukwe za bahari zina thamani gani?

Kitu kinakua na thamani kama kinaweza kuzalisha au kuleta faida, kama hakiwezi basi hakina THAMANI.

Yap, Networthy na GDP ni sawa na kulinganisha pilipili na machungwa, hapo tupo pamoja.

Ardhi na maliasili ya Tanzania ina utajiri ambao to put it simply, ni incalculable, kwa sababu ili ujue utajiri huu itabidi uchimbe ardhi yote na upige mahesabu ya vito vyote, mafuta yote, maji yote, mchanga wote, dhahabu yote etc etc.

Nakubali kwamba kitu kinakuwa na thamani kama kinaweza kuzalisha, na ardhi hii inaweza kuzalisha, kwa sababu ni arable na ina madini, so there is no question kwamba hii ardhi na maliasili nyingine haiwezi kuzalisha. Now if you are talking about kuzalisha kwa sasa, au mazao kuwafikia walengwa, those are different issues.You see nimependa ukweli kwamba umetumia maneno

"Kitu kinakua na thamani kama kinaweza kuzalisha au kuleta faida, kama hakiwezi basi hakina THAMANI."

Kwa kusema "kinaweza kuzalisha" inherently umeweka swala la potentiality, kwa kujua ukweli huu ndiyo maana hata Nyerere hakuwa na papara ya kuchimba madini/ mafuta, kwa sababu alijua as long as yapo ardhini, na bei ziko juu, potential ya kutumika ipo, na hivyo thamani ipo.

Kwa hiyo kama ulikusudia kuonyesha kwamba madini haya na maliasili nyingine hazina thamani kwa sababu "hayawezi kuzalisha" utakuwa unakosea, yanaweza kuzalisha, we only have to act on them, kwa hiyo kama hatuchimbi madini haya hayaishi kuwa na thamani, ila sisi wenyewe ndio tunaoshindwa kuitumia thamani hii na a more appropriate concept inakuwa kwamba hatufaidiki na thamani ya madini haya, which is close to "yanakosa thamani" in the strict utilitarian sense, lakini haimaanishi kwamba madini na maliasili hizi hazina thamani na kama zinahitajika ku account katika utajiri wa nchi.

Ni kama mtu kuwa na debit card ya Visa yenye hela nyingi kijijini ambako hamna ATM wala maduka yanayotumia Visa card. Huyu mtu anaweza kushindwa kuitumia card yake, na hii katika the strict utilitarian sense inaifanya hii Visa card kuwa kama worthless, lakini si kweli kwamba hii card haina value, kwa sababu akifika kwenye mji wenye ATM na maduka yanayotumia Visa card anatesa.

Au mtu kuwa na jiwe la almasi sehemu ambayo watu hawajui thamani ya almasi.In one sense almasi inakuwa worthless kwa sababu haiwezi hata kumnunulia gunia la mahindi, lakini ukiangalia tena akienda sehemu watu wanapojua thamani ya almasi, almasi hii tunaona kwamba bado ina thamani, na ukweli kwamba kuna situation fulani zinazoifanya almasi hii kukosa value, hakuiondolei value kabisa, kwani inaweza kurudi katika chart.

Value ni kama kile ki crystal/ kirusi kilicho katika jani la tumbaku, ambacho kinaweza kufa kwa muda mrefu, lakini conditions za kurudia maisha zikiwa nzuri kinarudia maisha baada ya kifo/ hybernation.

Kwa hiyo, on the one hand, ni kweli maliasili inaweza isiwe na immediate value, lakini on the other hand potential value iko pale pale.

All this "one the one hand..., on the other hand..." business reminds me of the uttrance of Harry S. Truman "Give me a one-handed economist! All my economists say, On the one hand... on the other..."

He must have been a one track minded president.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Back
Top Bottom