mr.dominick
JF-Expert Member
- Jun 21, 2012
- 244
- 28
Na bado watafuataia na wengine hakuna mtu atakaye ishinda serikali mkono wake ni mrefuuu wewe hapo hata ukikimbilia chooni kwenye nnya(headhunt movie) tunakupata tuu!
that's why some people become martyrs and others snipers, yet others freedom fighters and more other guerrillas. (and the state in turn labels them as terrorists!!!!)
Wakati huu wa crisis Jumuiya ya madaktari ilitoa full mandate kwa kamati kuu kuendelea kunegotiate na serikali hivyo Ulimboka alikuwa anatekeleza majukumu aliyopewa na Madaktari. Wakat mwingine it is better to remain silent and let people doubt you instead of talking and letting people clearing their doubt @ Maundumla and Pinda!!!Sasa rais ajiuzulu kwa kipi hasa?
Mimi nadhani ingekuwa busara mheshimiwa kiongozi wa madaktari Dr Ulimboka ajiuzulu mara moja kwa sababu wakati anafanya mazungumzo na hao jamaa kama alizungumza nao kama mwakilishi wa madaktari bila kupata idhini ya chama cha madaktari ni makosa makubwa!!
Mhola ahene.Nimesema hivyo kwa sababu kuna post humu inaonyesha kuwa alipigiwa simu na mtu asiyemfahamu akaenda peke yake.Sasa inashangaza aliendaje peke yakeNg'wanambula one saa,ubhange ngika si,aliekuambia dr Ulimboka alikuwa peke yake ni nani,na aliekuambia alikwenda kukutana na watu asiemjua ni nani?fuatilia vizuri upate kuhabarika,
Yan haya ni mauaji kbisa na tunahitaji tamko la serikali kwa hili.
Kumbe ndio maana ya msemo wa liwalo na liwe.
Ndio hilo lishakua sasa!!kauli tata ya "liwalo na liwe" imeanza kufanya kazi kabla
"Ndugu zangu,
Najaribu kutuliza mawazo ili angalau niweze kuwapa kidogo tulipofikia na tunakoelekea juu ya suala hili. Kwa kweli haivumiliki ukimwona ulimboka kwa jinsi alivyotendewa na hali aliyonayo; kwa wale wanaojua hali za kitabibu, "this is a very unstable condition that demands permanent watch 24/7".
Kwa taarifa tulizokusanya, ulimboka na mwenzake waliitwa na Afisa mmoja (Jina linahifadhiwa) ili kuzungumza mambo (fulani) na wakiwa wanaendelea na mazungumzo bila kuwa na mwelekeo wa muafaka, jamaa akawasiliana na watu (fulani) kwa simu. Ghafla wakajitokeza "ASKARI" wakawataka yule (Afisa) na Dr (aliyeongozana na Ulimboka) waendelee na shughuli zao na kuwambia "Tunamtaka huyu". Wakatumia nguvu, wakamburuta na kumtia kwenye gari jeusi na kuondoka naye wakidai wanampeleka Polisi.
Huku wakiwa wanamtesa, walimlazimisha mambo kadhaa (kwa sasa tusiyataje) wakaenda naye asikokujua, wakampiga sana kwa ngumi, mateke na magongo na wakati mwengine wakitumia Bunduki zao. Wakiwa wanampiga pia walikuwa wakisema kuwa amewatesa/wasumbua sana na kuwa anajifanya mjanja mbele ya (Srk) na hivyo wanamalizana naye; akapoteza fahamu...
Wakamtupa eneo la mapori huko Tegeta hadi alipookotwa na wananchi asubuhi na kukabidhiwa mikononi mwa Wanaharakati waliompeleka Hospitali Muhimbili.
Wakati akipokelewa MOI tayari baadhi ya wanaharakati walishafika eneo lile, kumbe kati ya walimpokea alikuwamo kijana anayesadikiwa kuwa ni "Askari". Huyu aligundulika baada ya mda mfupi akiwa amejificha chooni akiwasiliana kwa simu na watu aliokuwa akiwaambia " Hajafa. Bado anahema.... na maneno mengine yaliyoashiria kuwa waliofanya 'kazi' ile hawakukamilisha 'maagizo'. Vijana wakamfundisha adabu kwa hasira na kumkuta akiwa na Redio Call, ambayo baada ya muda mfupi Polisi FFU walifika na gari na vifaa vya vurugu wakiisaka ile Radio.
Nashindwa kuendelea....."
NB: Haya ni maelezo ya mwanaharakati Albanie Marcossy aliyehusika kumsaka kama nilivyoyanukuu Mabadiliko Group.
This is old communist style(tactics) hivi kweli dunia ya sasa unaweza kufanya vitu kwa staili hii ya kizamani ?huwezi kufunga mtu mdomo kwa kutumia mbinu hii ya kizamani dunia iko macho na mambo hayo ya kibabe ya kizamani hayakubalikiHii hatari sana maana nchi yetu ni ya amani lakini kuna matukio huwa yanatokea ukiyaangalia yanatia kichefuchefu, hii yote ni kutokana na nchi yetu bado watu wake wengi si waumini wa kutofautiana hoja ndio maana hata katika maisha yetu ya kwaida huwa mtu akiwa mbishi sana kwenye jamii huwa anachukuliwa kama adui badala ya kumkusanyia vielelezo ili aache kubisha vivyo hivyo kwenye serikali yetu nako ni yaleyale mtu anafanya kosa ambalo linaleta madhara kwa taifa akiambiwa wakati na yeye anajua amefanya kosa anawaona wale waliogundua uovu kama ni maadui. Kiukweli tumeshuhudia mashaidi wa kesi mbalimbali wanakufa katika mazingira ya utata wakati kesi zipo katika hatua ngumu na huwezi sema wameuliwa kwa kuwa hakuna ushahidi. Hii ni sawa na Kubenea alivyomwagiwa tindikali kutokana na kusema ukweli