Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,845
Hiki kilikuwa ni chuo kugumu na chenye sheria kali kuliko jeshi, tulikuwa wanachuo 21 toka Tanzania lakini tulifanikiwa kumaliza chuo tulikuwa kumi tu na mwishoni watano.
Tulipewa kila kitu bure lakini vinavyofanana kuanzia nguo mpaka dawa ya mswaki. Tuliishi maisha ya useja (total celibacy) huku tukiziadhibu hisia kwa kiwango cha juu mno!
Tulikuwa kwenye self cultivation (bringing back the scattered mind) Na hii ndio ilikuwa ratiba ya siku moja inayojirudia mara sita kwa wiki.
05:40 kuamka kutandika vitanda na kupiga mswaki/ kuiga
05:50 parade/ rollcall
06:00-0650 chanting/ meditation
06:50-07:00 parade/ rollcall na kwenda dining hall kimya na kwa mistari bila kuangalia kulia wala kushoto
07:20 chanting and giving offerings kwa milefo, na hungry ghost kisha breakfast
07:20-07:50 usafi
07:50-8:00 parade/ roll call na kuingia darasani
Vipindi vilikuwa ni dk 50 mapumziko dk 10 kuanzia saa mbili mpaka saa tano na dk 50
11:50-12:00 parade/ roll call na kumatch kwa mistari iliyonyooka kwenda dining
-Kuchant kutoa offerings kwa Milefo(future buddha?), hungry ghosts na kisha kula
12:00-13:50-lunch, walking meditation na kupumzika
13:50-14:00 parade roll call na darasani mpaka saa 15:50
15:50-16:00 parade roll call na kubadili nguo
16:00-16:50 martial arts, kung fu karate tai chi nk
16:50-17:50 free time hapa ndio sasa mnaweza kupiga soga na kuendelea na martia arts gym library etc
17:50-18:00 parade rollcall na kumatch kwenda dining
18:00-18:50 chanting offerings kwa Buddha na hungry ghost na kupata dinner
18:50-19:00 parade roll call
19:00-20:50 darasani
20:50-21:50 meditation/chanting
21:50-22:00 kurudi vyumbani kwa kumatch kwenye mistari tena kimya, kuingia vyumbani kuzima taa na kulala
Ukionekana nje baada ya hapo ni majanga
Chuo kiliongozwa na sheria kwenye kila kitu, sheria ya kutumia Maji, kutembea, kuongea kukaa kula kugeuka kulala, kutandika kuvaa etc kila kitu kilikuwa ni sheria na ndio maana wengi sana walishindwa maisha yale
Hii picha ni jinsi tulivyokuwa tunakaa mstarini kila mtu na nafasi yake kwahiyo hata kama haupo nafasi yako inabaki wazi.