70% ya Watanzania wanafata Upepo - JK

Kikwete si alipata about 80% Basi ianwezekana kabisa anachosema ni kweli.

70% waliompigia kura wanafuata upepo, 10% ni mostly mafisadi na watu waliojua watafaidik akiwa rais, wachache wanaamini ni rais anayefaa.
 
Juzi Bwana mkubwa aliporudi ziarani, aliongea uwanjani na waandishi akasema kuwa,haiwezekani kwake kupendwa na watu wote, kwa sababu watu wanatofaotiana kimtazamo, asilimia 15 ya watu wanaweza kumpenda, asilimia 15 watamchukia hata afanye mema, na asilimia 70 wanafata upepo!! Wadau kuhusu hii asilimia 70 ya wa tz kufata upepo haijanikalia sawa, kwa kweli inatoa picha mbaya, inaonyesha kuwa asilimia 70 ya Wa tz ni mambumbumbu??? Great thinkers nakuombeni mtoe mchango wenu kuhusu hii asilimia 70 !!

Inataka kufanana na ile ya "Watanzania ni wavivu wa kufikiri"
 
kushagua ccm 2010 ni sawa na kufukuwa mashimo pasipo na kuweka mbegu...... utavuna nini???????????????????
 
Mwalimu wetu mmoja miaka ya mwanzo ya Tisini (alipenda kuitwa 'Mh Kipanga') aliwahi kusema hivi "....any fool can be president of this country". JK na CCM wanajua Watanzania wengi can be fooled anytime of the day.

Kuna Watanzania wengi tu ambao hawajui hata maana ya Urais wenyewe. Nina jirani yangu mtu mzima, watoto wake hawaendi shule - hana uwezo wa kuwalipia - lakini anamsifu JK kuwa ni kiongozi bora na ametekeleza ahadi zake nyingi tu alizotoa wakati wa kampeni za uchaguzi 2005. Huyu anaishi mjini na mtu ungetarajia awe muelewa, hao walio vijijini wakoje? No wonder CCM (sic!) inashinda maeneo yenye maskini wengi.
 
Politicians wajanja sana, jamaa amekwepa issue ya msingi pale ambayo ilikuwa anatakiwa aeleze kwa nini anasitasita kuchukua maamuzi mazito yanayojumuisha issues za richmod,meremeta,tangogold, kagoda to mention few of them. Badala yake akaingiza issue nyingine watu wa i discuss

Labda atakapojibu atuambie hatua zitakazochukuliwa kuhusu mambo mazito yanayosemwa badala ya kujibu vijembe vya kisiasa
 
politicians wajanja sana, jamaa amekwepa issue ya msingi pale ambayo ilikuwa anatakiwa aeleze kwa nini anasitasita kuchukua maamuzi mazito yanayojumuisha issues za richmod,meremeta,tangogold, kagoda to mention few of them. Badala yake akaingiza issue nyingine watu wa i discuss

labda atakapojibu atuambie hatua zitakazochukuliwa kuhusu mambo mazito yanayosemwa badala ya kujibu vijembe vya kisiasa

hapo hata mimi nakuunga mkono mpuguso
 
Hapa sasa naamini kuwa na yeye alichaguliwa na hao 70% wanao fuata upepo hawakujua kwa nn wanamchagua.
 
Hapa sasa naamini kuwa na yeye alichaguliwa na hao 70% wanao fuata upepo hawakujua kwa nn wanamchagua.

Fide,

Mimi naamini katika 80% alizopata kuna 20% za wizi na 60% ndio zetu mafuata upepo na mafisadi.

...wewe hukumbuki wengi [yaani fuata upepo] wa wapiga kura wetu walipelekwa na zile kwaya za komba, ngoma za kienyeji na kanga?

Nani alikwambia watu walifanya rational decisions?
 
hapa rais kakosea kidogo, mitanzania tunaofuata mkumbo ni asilimia zaidi ya 90. subiri uchaguzi wa mwakani ndo utajua naongelea nini. mijitu tunakufa na ziki lakini bado tunawapa jamaa hao hao kura watumalize, kufuata mkumbo at its besti.aaaargh najiskia hasira sana. acha nilog off kwa sekunde 3 kupunguza munkari.
 
Back
Top Bottom