3 Bedroom House, toa changamoto!

Kabla haijawekwa kwa AutoCad, toa changamoto yako hapa, nini kimekosewa, nini kipo sawa...wapi parekebishwe..[emoji116]

View attachment 2240747
Master bedroom imejificha sana. Uzoefu wangu binafsi unanielekeza master bedroom lazima ikae sehemu ambapo unaweza kuona eneo kubwa la nyum a/uwanja wako hata kama kuna dalili ya kibaka baba ndio uchunfulie dirishani uone kwa usahihi. No bora eneo la jiko lingerudi nyuma huko Master bedroom ikae hapo.
 
Kabla haijawekwa kwa AutoCad, toa changamoto yako hapa, nini kimekosewa, nini kipo sawa...wapi parekebishwe..[emoji116]

View attachment 2240747
Master Bedroom ipo karibu na room za kawaida. Naona mwenye nyumba atakosa uhuru wa kujinafasi na mke wake akihofia watoto watasikia au mgeni anaweza wachungulia kwa kitasa
 
Kwa mimi huwa napenda master bedroom iwe upande upepo unatokea upate hewa ya kutosha chumbani kwako baba mwenye nyumba
 
Kabla haijawekwa kwa AutoCad, toa changamoto yako hapa, nini kimekosewa, nini kipo sawa...wapi parekebishwe..[emoji116]

View attachment 2240747
Binafsi nimeona haya;
1. Choo na bafu vipo pamoja kwenye vyoo viwili.. Ikitokea mmoja anaoga na mwingine anataka kuharisha ni ishu
2. Hapo penye maandishi walkway, sioni sababu ya kuwa pakubwa hivyo. Patashawishi kugeuzwa stoo ya ndoo za maji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…