Mimi ni shabiki halisi wa mpira japokua namkubali sana Messi, kwanza sikutarajia kwamba watafika fainal mana kikosi ndio kilekile cha 2022 kilichobeba kombe wameshachoka.
Ufaransa na Argentina tuzipe heshima yake tuache ushabiki
Ufaransa kabeba 2018 halafu karudi tena fainali 2022
Argentina kabeba 2022 karudi tena fainali 2026
Sio rahisi Mzee, Kuna timu hazijawahi kucheza hata fainali
Hata Infantino hakutarajia ndio maana aliwaandalia njia nyepesi.
Wewe unafikiri ni kwa bahati mbaya Argentina iwe timu pekee kwenye miaka 96 ya World Cup kufika semi final bila kukutana na top 10 ranked?
Hivi unadhani yale ambayo tumekuwa tukiyalalamikia humu kuhusu favouritism ambayo Argentina na Messi wamekuwa wakiipata, ilikuwa ni maneno matupu yasiyokuwa na hoja?
Unadhani ni kwanini Laporta ambaye ni raisi wa Club ya Barcelona kabla ya mechi alisema Spain wana timu nzuri ya kushinda kuliko Argentina ila ikiwa tu mwamuzi atachezesha fair?
Hivi unafikiri ni bahati mbaya kwenye miaka 96 ya World Cup (kasoro minne iwe karne ) Messi kuwa na Penalty nyingi kuliko mchezaji yeyote na huku penati 4 akizipata kwenye single tournament??
Uliyemuona jana, yule ndio Messi ambaye sisi tumekuwa tukimjua siku zote na tukiwaambia mnakaza fuvu.
Stats za Messi jana ni sawa tu na zangu ambaye nilikuwa naangalia hiyo game maana sina on target, sina off target, sina dribbles, sina goli.
Kitu pekee kinacho nitofautisha nayeye ni kwamba, mwenzangu alikuwa hana hivyo vyote akiwa yupo uwanjani wakati mimi nikiwa kwenye kitanda.