PreGE2025 2025 ni Samia vs Dovutwa na kina Rungwe

PreGE2025 2025 ni Samia vs Dovutwa na kina Rungwe

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Watanzania jiandae Kwa kampeni za kufa mtu, kampeini za kiushindani.

Mchuano utakuwa mkubwa haijapata kutokea kati ya Samia na kina Dovutwa na mzee Rungwe.

Unaambiwa upinzani kwenye nafasi ya uraisi ni mkali mno haijawai kutokea
Kama Mungu yupo na majeshi yapo basi aliepushe hili. Bila Tundu Lissu mie sitapiga kura wala kusimamia uchaguzi
 
Itakuwa ni mchuono na kampeni za vituko vya siasa tu na kuishia kwenye uchaguzi wa vioja. Tuseme kamapeni zitakuwa ni full burudani za wasanii wa kila aina ya muziki, waimba injili, bongo fleva, singeli, kwaya, hip hop, dansi, taarabu, bongo muvi, komedi na wapuuzi wengine wengi wenye haiba za kichawa. Mzee wa ubwabwa atakuwa anachekesha wananchi na sahani zake za ubwabwa, dovutwa kama kawaida yake atasindikiza na kuishia kuangukia pua. Uchaguzi wa mwaka huu kwa kweli utakuwa wa ajabu kuwahi kutokea tangu uhuru. Wameambiwa wauhairishe ili reform ifanyike lakini wanashupaza shingo. Tutaona vituko zaidi, muda ufike haraka tushuhudie abrakadabra za uchaguzi huo
 
Watanzania jiandae Kwa kampeni za kufa mtu, kampeini za kiushindani.

Mchuano utakuwa mkubwa haijapata kutokea kati ya Samia na kina Dovutwa na mzee Rungwe.

Unaambiwa upinzani kwenye nafasi ya uraisi ni mkali mno haijawai kutokea
Mzee wa ubwabwa anachukua nchi mapema sana
 
Dovutwa na Rungwe ili iweje?🤔 msikilize Lissu👇
 
Ni mwendo wa kulamba asali tu 😃
1000030864.jpg
 
Ushindi kama ule wa Kagame 98.9%
Watanzania jiandae Kwa kampeni za kufa mtu, kampeini za kiushindani.

Mchuano utakuwa mkubwa haijapata kutokea kati ya Samia na kina Dovutwa na mzee Rungwe.

Unaambiwa upinzani kwenye nafasi ya uraisi ni mkali mno haijawai kutokead
 
Sura ya uchaguzi wa mwaka huu tayari imeishajipambanua na kujifaragua. Kinachoenda kufanyika ni ili ionekane tu uchaguzi umefanyika na vyama vingi vimeshiriki na huenda vikapewa wabunge wawili watatu ili kuzuga kuwa uchaguzi ulikuwa huru na haki. Wapiga kura watakaojitokeza kwa wingi ni wanachama wa chama tawala, hawa watahamasishwa wajitokeze kwa wingi kwenye kampeni na hatimaye kwenye kupiga kura kwa wagombea wao. Vyama vingine vitakavyoshiriki vinaenda kusagulasagula tu vipate kura mbili tatu na hata kupewa wabunge na madiwani wa mchongo ionekane wamepambana hasa na wameshinda. Kwa hali ilivyo kama CHADEMA haitashiriki au ikashiriki bila muafaka ndani ya chama hicho wapiga kura wengi hawatajitokeza kwenye kamapeni na kwenye kupiga kura. Idadi ya wapiga kura itashuka sana
 
Kuna vyama hata sijui vilipataje usajili maana naona hata wagombea wao ni vibabu na havina mbadala na ni tangu tuwe na sera ya vyama vingi 1992 vipo tu. Ni bora viunge mkono nia ya chama tawala tu
 
Watanzania jiandae Kwa kampeni za kufa mtu, kampeini za kiushindani.

Mchuano utakuwa mkubwa haijapata kutokea kati ya Samia na kina Dovutwa na mzee Rungwe.

Unaambiwa upinzani kwenye nafasi ya uraisi ni mkali mno haijawai kutokea
kama hali hii ya kina lissu kutoshiriki uchaguzi mkuu, samia atapata ushindi wa mserereko kwa kura za wanachama wa chama chake tu. Kina rungwe na dovutwa kama kawaida yao watasindikiza na kuishia kuangukia pua, labda safari hii waonewe huruma waachiwe wabunge na madiwani wawili watatu au hata mmoja nao wajione wamo kwenye demokrasia. Kuna lile genge la chadema la G55 wanataka kugombea, Lissu yuko ndani, inawezekana genge hilo likagombea na kupata ubunge wakatinga bungeni na kuonekana mambo yalikuwa sawa uchaguzini mpaka wapinzani (wa mchongo) wameshinda. Utakuwa ni uchaguzi wa aina yake usiokuwa na mvuto wala hamasa ya kweli. kampeni zitapooza sana. Wanachi wamekata tamaa kushiriki chaguzi za abrakadabra
 
Back
Top Bottom